Chacha Wangwe Kuyafikisha Mahakamani magazeti Kwa Kumchafulia Jina

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
Naomba niwashirikishe taarifa hii ambayo nimeipata jana. Pamoja na kuwa binafsi siungi mkono mtindo wa kuyapeleka mahakamani magazeti(ila naunga mkono kama njia zote zikiwa zimepitiwa na bado ukweli ukashindwa kuandikwa) lakini naamini habari hii itajibu maswali ambayo wajumbe humu waliniuliza siku kadhaa zilizopita baada ya kueleza upande wa pili wa sarafu ya yaliyotokea Tarime. Tuendelee kujadili

Natoweka tena...

JJ

 
Huu utaratibu wa waandishi kuandika habari bila kuwemo mkutanoni ni kawaida huku bongo wala sioni cha ajabu.

Tatizo ni pale unapoandika habari za uongo!!

GO GO Chacha!
 
Wangwe, kwa mwanasiasa hakimu ni wananchi. Badala ya kusumbuka mahakamani, wewe chapa kazi na wananchi ndio wataamua nani mwongo.

Kuna case chache sana za siasa ambazo kuna umuhimu wa kwenda mahakamani, lakini kadri ninavyoisoma hii case naona kwenda mahakamani ni kupoteza muda tu.

Any way uamuzi ni wa Wangwe mwenyewe, lakini kwa mimi hii trend ya kila mtu kukimbilia mahakamani hata kwa madai ya kisiasa naona ni kupoteza muda tu.
 
Huu utaratibu wa waandishi kuandika habari bila kuwemo mkutanoni ni kawaida huku bongo wala sioni cha ajabu.

Tatizo ni pale unapoandika habari za uongo!!

GO GO Chacha!

Kuandika bila kuhudhuria, nani anakuwa source ya information zako. Utaandika mawazo yanayotokana na msimamo wa anayekusimulia na siyo matukio halisi.

Anyway, ukisoma habari hii na ile iliyotoka awali kuna kutofautiana sana kana kwamba ni matukio tofauti.
Nani anasema kweli na yupi kaongopa?
Akishtaki leo haki yake anaweza kuipata hata mwaka 2011 ndo mambo ya mahakama zetu.

Nadhani kukanusha kunatosha bila kulazimika kwenda mahakamani!
 
Wangwe chapa kazi,wala usiende mahakamani,hayo magazeti yalishaadhibiwa na wananchi,ni magazeti yanayotumiwa na mafisadi.achana nao,siye tulijua huo ulikua udaku tu.
 
...hii mambo ya wanasiasa wetu so called KUCHAFULIWA JINA inaniacha hoi sana,hivi chacha anafikiri nani anajari jina lake eti limechafuliwa? anafikiri wananchi hawana akili mpaka waanze kuangalia jina lake chafu au safi....ni kabunge tuu ka huko sijui tarime kanafikiri kila mtu anakafuatilia na kukaona ka maana sana mpaka kuchafuliwa jina,pumbaf sana chacha na umaarufu hautafutwi magazetini bora tuu uendelee kufanya kazi huu usafi wa jina lako tuachie wananchi wako wa Tarime...kwani press release haitoshi mpaka uende mahakamani? haya mambo ya cheap popularity na kujiona miungu mtu ndio hatuyataki
 
sasa kuchafuliwa majina na waandish eeh, wale wengine mafisadi wameelezwa ukweli.

hapa waandishi wakurupukaji, kule wamepasua jipu
 
We Koba, kutukana siyo vizuri sasa. Wewe toa hoja zako, sisi tutaziona na kuzipima. Mbona unamtukana tena huku ukitambua kuwa ni Mbunge wako? Elewa kuwa kuchaguliwa kwake na wananchi kuwawakilisha ni heshima kubwa.
 
...wewe Si kitiyi hapo juu PUMBAF sio tusi na mjomba wako Chacha wangwe needs to grow up na ugomvi wake na mwenyekiti wa kijiji na magazeti asiende kutujazia kesi zisizo na kichwa wala mguu kwenye mahakama zetu...kwani nakuuliza wewe Si kitiyi PRESS RELEASE haitoshi kwa issue ndogo kama hii mpaka uende mahakamani?
 
Kaka Wangwe,salamu na pole na majukumu,
Ama baada ya salamu napenda kuchangia kuhusu uamuzi wako wa kwenda mahakamani kushtakiwa kuhusu "kuchafuliwa" jina.Binafsi nadhani huna haja ya kwenda mahakamani,kwanza kwa sababu si kila kitu lazima uende mahakamani,pili swala hili sidhani kama lina uzito sana kiasi hicho kama ambavyo baadhi ya watu wanakushari,ebu jaribu kuweka mizani sawia na utazame matokeo,yaani kwenda mahakamni kutakujenga/kukubomoa kiasi gani kuliko kutokwenda?
Kwa sasa nadhani jina lako bado ni safi hivyo huhitaji kulichafua kwa mambo ya kimahakama.Hakimu wenu ni sisi wananchi,tazama mfano wa Zitto Kabwe,Mbunge mwenzio,ni kweli kafukuzwa bungeni kwa kuhoji maslahi ya Taifa,kaiitwa muongo,n.k. lakini hakuonesha reaction yoyote ile bali wananchi ndo wamesimama kwa niaba yake na hali yote ya kisiasa inayoendelea hapa nchini chanzo ni yeye.Hivyo na wewe jaribu kufikiri kwanza,kwenda mahakamani kutapunguza umaarufu wako zaidi ya kukujenga.Isitoshe kwa watu wenye akili hiyo habari wala haikutugusa kwani tulijua kwa nini iliandikwa na ni kwa nini ikawa kwa magazeti hayo na ndo sababu haikupata uzito wowote kabisa.
Wewe chapa kazi 2010 sio mbali wananchi ndio watakaohukumu...kumbuka kina Ditto,Nyali wanavyopeta kutokana na Mahakama hizi hizi...

NAWASILISHA
 
Sawa, hata mimi sishauri kwenda mahakamani sioni umuhimu wowote, kwanza jambo lenyewe siyo zito hadi aamue kwenda mahakamani. Mimi hoja yangu ilikuwa juu ya neno pumbafu, mimi naliona kama tusi. Kama siyo tusi basi sawa.
 

Unavunja heshima yako (kama iliwahi kuwepo) kwa kutumia lugha kali ya matusi namna hiyo.
Unaweza kufikisha ujumbe kwa kutumia maneno ambayo yanastahili kwenye sehemu kama forum. Katumie lugha hizo nyumbani kwako na siyo hapa!!!!!!!
 
Unavunja heshima yako (kama iliwahi kuwepo) kwa kutumia lugha kali ya matusi namna hiyo.
Unaweza kufikisha ujumbe kwa kutumia maneno ambayo yanastahili kwenye sehemu kama forum. Katumie lugha hizo nyumbani kwako na siyo hapa!!!!!!!

.....nafikiri kuna kitu unatafuta kutoka kwangu,subiri uone!
 
Hakuna cha kutafutwa hapa, ulichoharibu wewe ni kutumia lugha chafu. Unatakiwa kuwasilisha ujumbe wako kwa kutumia kichwa na si kutumia moyo: Kichwa kinatawaliwa na hekima na busara, bali moyo hutawaliwa na hisia (emotions).
 
hamna hoja nyie...katukanwa EL,JK na mawaziri wote hakuna kitu mlisema leo huyo chachacha kidogo tuu kashtuliwa hapa mnakuja juu kama tsunami...hamna deal nyie wanazi!
 
hamna hoja nyie...katukanwa EL,JK na mawaziri wote hakuna kitu mlisema leo huyo chachacha kidogo tuu kashtuliwa hapa mnakuja juu kama tsunami...hamna deal nyie wanazi!
Kuna tetesi hizo kuwa walimuhonga lakini bado alikuwa na nia ya kuipeleka hoja ya Barrick bungeni.Wakati anaondoka,alienda kumuaga Sitta, ambaye alimwambia awe makini,lakini hakurudi na hoja haikuwakilishwa...Lakini cha ajabu ccm na mapandikizi wanasambaza uzushi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…