Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Mara, Chacha Heche, amesema kuwa hadi sasa chama pekee cha upinzani chenye uwezo wa kuibana CCM kisiasa na kulazimisha mawazo mapya ni CHADEMA pekee, akisisitiza kuwa hakuna chama kingine cha upinzani chenye ushawishi na nguvu sawa na CHADEMA.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa programu ya CHADEMA Family jijini Musoma, Heche amesema: “Mshindani anayeweza kusababisha CCM ilale iwaze uchaguzi ni CHADEMA pekee, hakuna chama kingine.”
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuhusu Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Heche ameendelea kueleza kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakijaribu kulinganisha harakati za sasa na TANU, lakini kwa mtazamo wake, CHADEMA imepitia mapambano makali zaidi kuliko chama chochote cha kisiasa kilichopata kutokea nchini.
Heche amelenga kufafanua kuwa uhuru wa pili unaozungumzwa na CHADEMA ni pamoja na uhuru wa kweli wa wananchi kuchagua viongozi wanaowataka kupitia uchaguzi huru na wa haki.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa programu ya CHADEMA Family jijini Musoma, Heche amesema: “Mshindani anayeweza kusababisha CCM ilale iwaze uchaguzi ni CHADEMA pekee, hakuna chama kingine.”
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuhusu Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Heche ameendelea kueleza kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakijaribu kulinganisha harakati za sasa na TANU, lakini kwa mtazamo wake, CHADEMA imepitia mapambano makali zaidi kuliko chama chochote cha kisiasa kilichopata kutokea nchini.
Heche amelenga kufafanua kuwa uhuru wa pili unaozungumzwa na CHADEMA ni pamoja na uhuru wa kweli wa wananchi kuchagua viongozi wanaowataka kupitia uchaguzi huru na wa haki.