Cha kuokota sio cha kuiba

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,305
Mzee Ngowi na Bi Sikitu ni wapenzi walio pendana toka shuleni wakiwa watoto, mpaka wakaoana. Baada ya kustaafu waliamua kurudi kuishi eneo waliloushi zamani walipokuwa wadogo, na kusoma.

Siku moja walikuwa wanasherehekea miaka 40 ya ndoa yao. Hivyo waliamua kutembelea shule yao waliposomea zamani ili kusherehekea miaka 40 yao ya ndoa.

Wakishikana mikono, walitembea kwenda shuleni kwao. Geti la shule lilikuwa halijafungwa, hivyo wakaingia na kwenda kwenye dawati lao la zamani walilokuwa wanatumia ambalo Mzee Ngowi alikuwa ameandika "Nakupenda, Sikitu."

Baada ya kumaliza kusherekea wakaanza safari ya kurudi nyumbani kwao, lakini njiani wanakuta begi likiwa halina mwenyewe.

Bi Sikitu anaokota begi ilo na kuangalia kuangalia ndani, na kukuta begi limejaa hela. Hakutaka kupoteza muda akalibeba, wakaendelea na safari mpaka nyumbani kwao.

Wakiwa nyumbani Mzee Ngowi akasema, "Tunapaswa kurudisha begi la watu."

Bi Sikitu akasema, "Cha kuokota sio cha kuiba, hata hivyo aliyeokota ni mimi." akafunga begi vizuri na kulihifadhi juu ya paa lao.

Siku inayofuata, maafisa wawili wa polisi walikuwa wakizunguka jirani wakitafuta pesa na wakagonga mlango wao.

"Samahani, je, mmoja wenu aliona begi lililodondoka kutoka kwenye gari la kubeba pesa jana?"

Bi Sikitu akasema, "Hapana."

Mzee Ngowi akasema, "Anawadanganya, amelificha juu kwenye paa."

Bi Sikitu akasema, "Msimuamini anaanza kuzeeka."

Maafisa wakageuka kwa Mzee Ngowi na kuanza kumhoji.

Mmoja wao akasema: "Tuambie hadithi kutoka mwanzo ilivyokuwa."

Mzee Ngowi akasema, "Vizuri, wakati Sikitu na mimi tukiwa tunarudi nyumbani kutoka shuleni jana."

Afisa wa polisi wa kwanza akageuka na kumtazama mwenzake na kusema, "Tuondoke hapa tukatafute mahali pengine."

Mwisho

Credit - Lil Dee
 
Ugai gai au kona kona.
Screenshot_20240115-223918_1.jpg
 
Yani polisi badala ya kusikiliza hadi mwisho wao 😂😂😂😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom