Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Klabu ya Simba kupitia kwa Mtendaji Mkuu wao (CEO) Barbara Gonzalez, amethibitisha kuwa hadi kufikia sasa wamepokea simu nyingi sana kutoka klabu kadhaa zikiwemo vigogo wa Afrika Wydad na Raja, zikimuhitaji nyota Pape Ousmane Sakho ambaye jana usiku alitwaa Tuzo ya goli bora la CAF 2022.
"Ukweli ni kwamba Simba SC tumepokea simu nyingi sana, klabu kadhaa tangu jana usiku wamekuwa wakihitaji tumalize biashara, wengine wanamfuata mchezaji wakitaka tumalizane, presha ni kubwa sana kiukweli ila mwisho wa siku zinazipima"
"Viongozi wake wa Senegal wanashangaa na wanauliza kwanini anacheza Tanzania.! walikuwa wanamwambia anapaswa kuondoka sasa na ni lazima aondoke akacheze mbele zaidi ya hapo"
"Utamaduni wetu kama Simba ni kuwapa fursa wachezaji wetu, ikitokea wamepata ofa nzuri hakuna shida, nikikuambia nina ofa zaidi ya mbili kwa ajili ya mchezaji Sadio Kanoute utakubali? Wachezaji wetu wengi wana ofa kutoka nje, ila ni lazima tukae chini tutafakari"
"Simba bado hatujamaliza usajili, hata hapa Morocco kuna baadhi ya wachezaji nafuatilia, nisingependa kutaja idadi ila tuna maingizo mapya tunakamilisha". CEO Barbara Gonzalez.
"Ukweli ni kwamba Simba SC tumepokea simu nyingi sana, klabu kadhaa tangu jana usiku wamekuwa wakihitaji tumalize biashara, wengine wanamfuata mchezaji wakitaka tumalizane, presha ni kubwa sana kiukweli ila mwisho wa siku zinazipima"
"Viongozi wake wa Senegal wanashangaa na wanauliza kwanini anacheza Tanzania.! walikuwa wanamwambia anapaswa kuondoka sasa na ni lazima aondoke akacheze mbele zaidi ya hapo"
"Utamaduni wetu kama Simba ni kuwapa fursa wachezaji wetu, ikitokea wamepata ofa nzuri hakuna shida, nikikuambia nina ofa zaidi ya mbili kwa ajili ya mchezaji Sadio Kanoute utakubali? Wachezaji wetu wengi wana ofa kutoka nje, ila ni lazima tukae chini tutafakari"
"Simba bado hatujamaliza usajili, hata hapa Morocco kuna baadhi ya wachezaji nafuatilia, nisingependa kutaja idadi ila tuna maingizo mapya tunakamilisha". CEO Barbara Gonzalez.