CDM yamhenyesha Pinda uingereza


Yaani wewe ndo muongo wa kupindukia. Waziri mkuu yuko Londoni na kwa taarifa yako jana kwa macho yangu nimemuona akihojiwa na Salim Kikeke wa BBC kuhusu swala la mpaka wa Tanzania na Malawi. Punguza kukurupuka ndugu. Wewe sasa ndo unapaswa kuwa mkweli.
 

Scolari... wakati mwingine acha longolongo ... nikiwa mmoja wa waliohudhuria mkutano huo naweza kusema kwa uwazi kwamba neno Chadema lilitamkwa mara moja tu na kwa utani...Pinda pia aliisema chadema kwa fumbo moja la wapenda maandamano... wakati wote wa mkutano...watu walikuwa zaidi ya 15.. kwa idadi yangu kama zaidi ya 50 hivi...

Pinda aliongelea zaidi mambo ya maendeleo ya Tanzania na tukampa ushauri kwamba hao wawekezaji wanaokuja huko nyumbani wakubalishwe ki mkataba kuwafundisha ujuzi wa kazi watanzania wanaofanya kazi katika makampuni yao... iwe katika gas, madini au utalii... yaani compusory Knowledge transfer...

mambo mengine yaliyozungumziwa ni kuhusu suala la amani kwa ujumla wake.... mambo ya ufisadi na azimio la Arusha.. Rapid transport system , ajali katika barabara zetu za Tanzania na ubora wa vyombo vya usafirishaji hasa mabasi yetu tunavyoyaona kama chinja chinja..., mambo ya muungano wa mkataba.. mambo ya sensa kwa sisi wa ughaibuni... suala la kumaliza uchakachuaji kwenye chaguzi zetu kwa kuwa na automatic vote counter... na mengine mengi...

sikuona hata moja ambapo pinda alihenyeshwa...niweke wazi kwamba nina mlango wa kupenda mawazo mbadala ya Chadema na katika hili Pinda apewe haki yake...Vinginevyo chadema itaanza kupunguza watu kama sisi tunaopenda mawazo yao ...

Nilitaka kumuuliza pinda ni kwa nini kasi ya maendeleo ya Tanzania haiendani na muda wa ccm madarakani au ni kwa nini kama ccm wameshidwa wasingatuke kama baba wa taifa .. lakini sikupewa nafasi hata baada ya kunyoosha mkono kwa muda mrefu... ni matumaini yangu wakati mwingine tutapewa nafasi kama hiyo....
 

Afadhali umejisemea ukweli. Kwa hiyo ni Ukweli CDM imemnyima usingizi kiasi hata cha kuisema kwa mafumbo! Yawezekana nawe umekuja kidiplomasia hapa kujaribu kuuficha ukweli kwa kujifanya unahusudu mawazo ya CDM wakati sio.
 

Mkuu idadi hiyo unatoa ujumbe alioambataba nao pamoja na maafisa wa ubalozi au ni wote kwa pamoja? Vyovyote itakavyokuwa unataka kusema PM wa Tanzania kweli akiitisha mkutano wanakuja 50 wewe unaona hao ndio wengi au vipi. Kwanini kwanza kwenye vyama vyote hakutaja CDM. Mleta uzi amefuatilia idadi na akaweka wazi uchahce wa walioitika. Yeye alukwa interested na number of audience.Wewe ulikuwa interested na nini? kwanini ulihesabu watu kama your principle objective ilikuwa kumsikiliza PM. After all the guy is unpopular and disrespected deputy of dishonoured boss. How can you leave your house when it's burning. Sikia maaskofu wa KKKT wameamua kupostpone their meet ili waje waone kilichotokea na kutoa one of the briliant remarks. Uongozi ni hivyo sio ziara zisizokuwa na tija
 
Scolari... unataka kupata yaliyojili kwenye mkutano au unataka malumbano? sipendi kuongelea kunyimwa usingizi kwa pinda maana sina uhakika kama ni kweli alinyimwa usingizi... kama ni kweli aulizwe yeye maana sijaona au kusikia kwamba hakulala kabla ya mkutatao huo..isipokuwa toka kwako...sina sababu ya kuja hapa kidiplomasia au kuficha ukweli au kwamba ni pretender wa kuhusudu mawazo ya chadema au ccm au yako... maana nikiwa kama unavyotawa wewe ... na wewe pia utakuwa vivyo hivyo kama mimi kutaka kupata kilichojili mkutano kwa kusema kwamba alihenyweshwa...

kusemwa mtu kwa mafumbo ni tafsiri yangu ladba Great thinker watasema wapenda maandano ni cuf au uamsho au nccr... haina maana ni chadema...acha tabia ya upotoshaji.. ni kweli kwamba ccm wamekaa madarakani muda mrefu na wamechokwa na current generation lakini ni ukweli kwamba pia wana wapenzi wao kama chadema na wengineo...

Mimi ni independent na huwezi kunilazimisha niwe chadema au ccm au cuf au uamsho na wengineo ...kuna mazuri yao chadema, ccm na wengineo pia kuna mabaya yao... pia hata wewe ni unaonekana (kwa tafsiri yangu) kama ni ccm vile maana ni mpotoshaji wa kilichojili mkutanoni...


labda nikuulize...ulikuwepo mkutanoni? je unayapinga niliyoyasema hapo juu kwamba yalizungumziwa? au unataka/kupenda malumbano yasiyokuwa na taja ladba kwa wakosa kazi?
 

Nimetoa au kukisia idadi kwa kuangalia viti ambavyo vilikuwa vimejaa... pia labda utupe uniform definition ya neno uchache.. je ni wawili , watatu , ishirini au ni 50...? kama ni hao 20 out 45 mili.. yes ni wachache.. kama ni 50 in a given space au ukumbi ulipofanyika mkutano huo.. basi hao ni wengi...ukweli ni kwamba palijaa na wengine walisimama...muulizeni machibya wa BBC atawapa maana nilimuona ndani yake na alipewa muda wa kuuliza swali...

haya mengine ya pinda being unpopular.. it doenst matter to me.. maana hata wewe ukiwa na kazi kama yake waweza kuwa unpopular vilevile ... I am just looking forward siku tukipata mtu mwenye kuleta maendeleo tunayoyataka bila mizengwe ....kuanzia kwa Raisi.makamu na pm mwenyewe...
 


Nyie wote mlikuwepo kwenye huo mkutano? Siasa bana.
 
Nyie wote mlikuwepo kwenye huo mkutano? Siasa bana.

Najibu kwa nafsi yangu kwamba nilikuwepo... ndio maana nimeweza kusema kilichotokea ... je wewe ulikuwepo?
 

Scolari... wakati mwingine acha longolongo ... nikiwa mmoja wa waliohudhuria mkutano huo naweza kusema kwa uwazi kwamba neno Chadema lilitamkwa mara moja tu na kwa utani...Pinda pia aliisema chadema kwa fumbo moja la wapenda maandamano... wakati wote wa mkutano...watu walikuwa zaidi ya 15.. kwa idadi yangu kama zaidi ya 50 hivi...

Ukisoma hayo hapo juu ni maneno yako mwenyewe. Umesema kuwa Pinda ilitamka CHADEMA mara moja tu na pia ukasema aliisema kwa fumbo moja tu la wapenda maandamano. Sasa mbona unajikoroga mwenyewe kuwa hajaitaja na kusema wapendaa maandamano kunaweza kumaanisha chama chochote wakati ushaitaja CHADEMA mwenyewe?

Kwa nini basi hilo neno moja lisiwe CUF, NCCR, CHAUMA ama CHAUSTA? Acha kutuzuga!
 
Najibu kwa nafsi yangu kwamba nilikuwepo... ndio maana nimeweza kusema kilichotokea ... je wewe ulikuwepo?

Orait. kumbe unajibu kwa nafsi yako. Whether or not ningekuwepo nisingejibu subjectively kama wewe.

Mh. Pinda alikutana na Watanzania waishio Uingereza dhumuni likiwa ni kuzungumzia mustakabali wa maendeleo ya nchi kisiasa, kiuchumi, n.k.

It does not matter whether or not huo mkutano ulikuwa wa kisiasa. Kinacho-matter ni whether or not alizungumzia mambo ya kisiasa kwenye huo mkutano hata kama ulikuwa ni wa kidini.
 

Hivi siku hizi wapenda maandamano maana yake ni Chadema? hii ilikuwa tafsiri yangu...

au Mtu (pinda) akitaja Chadema kwenye mikutano ya watanzania kwa ujumla wake ni criminal au civil offence.. na nilazima awataje akina CUF, NCCR, CHAUMA ama CHAUSTA? Mzugaji ni wewe kwa ku-report vivyo- sivyo ! mimi nilihudhuria tu kama independent bystander.
 

ok.. ningesema hizi...Mh. Pinda alikutana na Watanzania waishio Uingereza na kuzungumzia mustakabali wa maendeleo ya nchi kisiasa, kiuchumi, n.k. It does not matter whether or not huo mkutano ulikuwa wa kisiasa. Kinacho-matter ni kwamba whether or not alizungumzia mambo ya kisiasa kwenye huo mkutano hata kama ulikuwa ni wa kidini.

Sikuzumgumza 'subjectively' intentionally lakini kwa kujibu yaliyoulizwa na scolari...
 
Reactions: EMT
Hizo zinaitwa Tantararira wafuasi wa Chadema Uingereza hawazidi 20 kina Chilisosi, Uingereza Watanzania wengi ni Wapemba nao wamejiripuwa.

Sidhani kama unajua unachoongea au upo kwenye majonzi baada ya Ponda kukamatwa! kwanza unafahamu UK yote acha England kuna watanzania wangapi jumla??Kama hujui nitakupatia statistics za Watanzania wote waliopo UK!
 

Diffusion of responsiblity

  1. The bystander needs to notice that an event is taking place, but may fail to do so and not provide help;
  2. The bystander needs to identify the event as some form of emergency. The situation may be ambiguous, preventing from help being given;
  3. The bystander needs to take responsibility for helping, but might avoid taking responsibility by assuming that some body else will (diffusion of responsibility);
  4. The bystander needs to decide on the appropriate helping response, but may not believe themselves to be competent to do so;
  5. The bystander needs to implement that response, but this may be against their interest to do so, specially in dangerous situations.
 
Hayuko kisiasa? Sasa anafanya nn huko huku UAMUSHO NA PONDA wanatumaliza na vurugu. Aje huku aongee na hawa mbwa wa ponda watulie.
 
Kiwanda At Work.

Umeona eh? Watu watatu wanadai walikuwa kwenye huo mkutano lakini wanatoa versions tatu toufauti. Bora mie niweke picha. Picture speaks louder than words. Hao watu walio kwenye mkutano hawazidi 15 kweli?



Mh Waziri Mkuu aliongozana na mkewe akisalimia na Balozi wa Tanzania nchini uingereza Peter Kallaghe mara baada ya kuwasili Ubalozini





Mh waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza na watanzania.

Mh Waziri Mkuu akifananua Jambo.

Dr Hamza akisema machache

wakati wa maswali na Majibu.

Balozi wa Tanzzania nchini uingereza Mh Balozi Peter Kallaghe akimkaribisha Mama Tunu Pinda kabla Mh Waziri mkuu kuongea na watanzania.

Watanzania wakifuatilia hotuba ya Mh Waziri Mkuu.

Watanzania wakimsikiliza Mh waziri Mkuu.

Mh Waziri Mkuu akisalimiana na baadhi ya watanzania baada ya mkutano



 
Ukweli husemwa:

Wewe ndiyo umekurupuka bila kuisoma post yake vizuri. Amesema, Waziri Mkuu hayuko UK kwa shughuli za kisiasa na wala hajafanya mkutano wa kisiasa.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…