Scolari Ndenga
JF-Expert Member
- Aug 4, 2008
- 271
- 43
Waziri mkuu Pinda amefanya ziara isiyokuwa na miguu wala kichwa nchini Uingereza. Akiwa huko alipata habari za uwepo wa mkutano wa wanachadema uliongozwa na Wenje amabye ni mkurugenzi wa mambo ya nje wa CDM na Munishi ambaye ni katibu Mkuu wa BAVICHA.
Habari zilizovuja zinasema Pinda aliamua kumshinikiza Balozi wa Tanzania Uingereza kuitisha mkutano wa wana CCM kwa mgongo wa jina "WATANZANIA" siku ya Jumanne ya terehe 16/10/2012 ubalozini baada ya kusikia CHADEMA wamekutana ijumaa iliyopita na kuazimia kuisambaratisha CCM Uingereza.
Katika mkutano huu walijitokeza watu wasiozidi 15 na taarifa za ndani zinadai Pinda ametamka ndani ya kikao hicho kuwa CHADEMA ni "KIBOKO" kwani siku za nyuma walizoea kupata mapokezi makubwa yenye mbwembwe kama viongozi wa serikali lakini baada ya CDM kujikita nje kwa siku za hivi karibuni , hali hiyo imetoweka na kuwaduaza viongozi wa serikali.
Ikumbukwe wiki tatu zilizopita, makamu wa rais Gharibu Bilal alifanya ziara kama hiyo nchini Uingereza na kuambulia patupu.
Viongozi wa CDM walifanya mkutano wao tarehe 12/10/2012 jijini London na kukusanya idadi kubwa ya watu kutoka miji ya Reeding, Birmingham na London na baadhi ya watanzania waishio huko walijiunga na CDM.
Source: Mtanzania aliyekuwapo mkutanoni kwenye ubalozi wa Tanzania London.
Habari zilizovuja zinasema Pinda aliamua kumshinikiza Balozi wa Tanzania Uingereza kuitisha mkutano wa wana CCM kwa mgongo wa jina "WATANZANIA" siku ya Jumanne ya terehe 16/10/2012 ubalozini baada ya kusikia CHADEMA wamekutana ijumaa iliyopita na kuazimia kuisambaratisha CCM Uingereza.
Katika mkutano huu walijitokeza watu wasiozidi 15 na taarifa za ndani zinadai Pinda ametamka ndani ya kikao hicho kuwa CHADEMA ni "KIBOKO" kwani siku za nyuma walizoea kupata mapokezi makubwa yenye mbwembwe kama viongozi wa serikali lakini baada ya CDM kujikita nje kwa siku za hivi karibuni , hali hiyo imetoweka na kuwaduaza viongozi wa serikali.
Ikumbukwe wiki tatu zilizopita, makamu wa rais Gharibu Bilal alifanya ziara kama hiyo nchini Uingereza na kuambulia patupu.
Viongozi wa CDM walifanya mkutano wao tarehe 12/10/2012 jijini London na kukusanya idadi kubwa ya watu kutoka miji ya Reeding, Birmingham na London na baadhi ya watanzania waishio huko walijiunga na CDM.
Source: Mtanzania aliyekuwapo mkutanoni kwenye ubalozi wa Tanzania London.