Scolari... wakati mwingine acha longolongo ... nikiwa mmoja wa waliohudhuria mkutano huo naweza kusema kwa uwazi kwamba neno Chadema lilitamkwa mara moja tu na kwa utani...Pinda pia aliisema chadema kwa fumbo moja la wapenda maandamano... wakati wote wa mkutano...watu walikuwa zaidi ya 15.. kwa idadi yangu kama zaidi ya 50 hivi...
Pinda aliongelea zaidi mambo ya maendeleo ya Tanzania na tukampa ushauri kwamba hao wawekezaji wanaokuja huko nyumbani wakubalishwe ki mkataba kuwafundisha ujuzi wa kazi watanzania wanaofanya kazi katika makampuni yao... iwe katika gas, madini au utalii... yaani compusory Knowledge transfer...
mambo mengine yaliyozungumziwa ni kuhusu suala la amani kwa ujumla wake.... mambo ya ufisadi na azimio la Arusha.. Rapid transport system , ajali katika barabara zetu za Tanzania na ubora wa vyombo vya usafirishaji hasa mabasi yetu tunavyoyaona kama chinja chinja..., mambo ya muungano wa mkataba.. mambo ya sensa kwa sisi wa ughaibuni... suala la kumaliza uchakachuaji kwenye chaguzi zetu kwa kuwa na automatic vote counter... na mengine mengi...
sikuona hata moja ambapo pinda alihenyeshwa...niweke wazi kwamba nina mlango wa kupenda mawazo mbadala ya Chadema na katika hili Pinda apewe haki yake...Vinginevyo chadema itaanza kupunguza watu kama sisi tunaopenda mawazo yao ...
Nilitaka kumuuliza pinda ni kwa nini kasi ya maendeleo ya Tanzania haiendani na muda wa ccm madarakani au ni kwa nini kama ccm wameshidwa wasingatuke kama baba wa taifa .. lakini sikupewa nafasi hata baada ya kunyoosha mkono kwa muda mrefu... ni matumaini yangu wakati mwingine tutapewa nafasi kama hiyo....