CCM’s svengali hold

Can I ask you,what the hell power or authority to decide that the case was a bogus one?

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Immediate after Mbowe's release SSH played smart. Unleashed the beast out of the Chairman
 
Umekosea sana aisee. Yeye ndo alipaswa aje kwako kukuona

Hili linaweza likawa sahihi, lakini approach zinatofautiana mkuu..

Huwezi jua alienda kuzungumza yapi? Labda alienda kumchana kuwa Mkuu umenizingua, au Samia aliomba msamaha..

Kwasababu maongezi yao hayakuwa wazi kwa 100%
 
Hata kama inaenda mrama, wapinzani are not capitalizing on it!

Very disappointing.
Pole ndugu, ila sijui ni kwa nini unatamani kasi hiyo.
Mbowe alikuwa na mawasiliano kamili na uongozi wa juu waCHADEMA ambapo waliweka mipango na taratibu za kuonana na wanachama.
Wale waliyokuwa wametokea mahakamani nao walielezwa walipofika pale makao makuu.
CHADEMA pamoja na kupitia vishindo vingi bado yahitaji umakini katika maamuzi na sio papara ili tu 'kufurahisha' watu. AMEN
 

Mwendazake alifanyaje. Adui wa Wapinzani yupo ndani. Huyu Mbowe sio msafi kwa wanachadema wenzake kama unavyotaka kuremba hapa. Sio rahisi kuwa mwenyekiti wa chama cha Siasa kwa miaka 20 Ukiwa sauber ohne blemish.
 
Nikusahihishe, Mh Mbowe hajasamehewa maana hakua na hatia , Bali amefutiwa mashtaka. Kumbuka alikuwa anajiandaa kwenda kujitetea mahakamani ndio nolle prosequi ikaletwa.
Ndio maana nikasema Yaani wanakutengenezea kosa harafu wanakusamehe na wewe unawasifia harafu wanakutumia
 

Sharti ni kwamba awe upande wa Samia na mwiko kufanya upinzani wenye lengo la kumuharibia Samia, hilo lilikuwa sharti ambalo lilichukuwa muda Mbowe kulikubali sasa mwishowe kakubali baada ya akina Askofu Shoo kufwatwa labda hata walindugaiwa, kasamehewa akilivunja anakamatwa tena kurudishwa ndani kesi kuanza upya, nchi ilishaoinduliwa hii hamjui tu au hamtaki kukubali labda.

Baada ya Mbowe kuuza, chadema will never be the same again kuanzia sasa hivi, Mbowe atakuwa kama Zito Kabwe, subiri utaona hata watamkampenia Samia!
 
Kesi ilifunguliwa July 2020 na Mbowe akakamatwa July 2021???

Only in Tanzania where you’ll find this kind of fuckery [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
File lilifunguliwa July 18, 2020 na Swila,Kingai DCI et al kipindi Cha JPM.

Walinzi wa Mbowe walikamatwa na kubambikiwa madawa ya kulevya, na silaha na sare za JWTZ mwezi August, 2020 kipindi Cha JPM.

Walinzi wa Mbowe waliandikishwa maelezo ya uongo kuwa wamekiri na kumtaja Mbowe kuhusika na ugaidi mwezi August 2020 kipindi Cha JPM.

Mashahidi karibia wote waliandikishwa maelezo mwaka 2020 kipindi Cha JPM.

Lengo likawa kumkamata Mbowe na kumfungulia mashtaka soon baada ya uchaguzi, na haikuwa Mbowe tu ilikuwa Bali ilikuwa waunganishwe Tundu lissu na Godbless Lema.

Taarifa zikavuja, Tundu lissu alivyosikia Kuna kesi pending alikimbilia ubalozi wa Ujerumani then akakimbia nchi.

Lema aliposikia polisi wanamsaka akakimbia akavuka mpaka wa Kenya then akaenda Canada.

Na Mbowe akakimbia nchi akaenda zake Dubai, ndiyo kipindi alichokaa sana nje ya nchi akarudi ashadungwa chanjo ya Corona na ndiyo maana hata wasaidizi wa Samia walimwambia Samia kuwa Mbowe alikimbia nchi ni kweli alikimbia, amerudi JPM akiwa hoi.

Sasa katika mazingira haya huwezi kubisha kuwa aliyesuka hii kesi ni Magufuli. Samia ameingia Ikulu katika mazingira ambayo hakuwa hata amejianda hivyo alikuwa anahitaji muda ku cope na vitu vingi. Huku chini wasaidizi wake wakiwa tayari Wana ushahidi waliopika Kwa maelekezo ya Mwendazake. Amekuja kushtuka kesi ishafunguliwa na wakamdanganya kuwa wanao ushahidi wa kutosha.
 
Mandela alifungwa miaka 27 na alipotoka gerezani akatangaza amani kwa watesi wake. Ilimpa umaarufu na kule kusamehe kukawafanya wazungu waliomfunga waonekane wajinga. Ni imani ya kiwango cha juu sana waliyonayo ni wachache sana.
 
Kwa hiyo Samia alikuwa anakubaliana na Magufuli katika kumkamata Mbowe, siyo?
 
Unatoka jela, badala ya kukutana na kuongea na watu waliosimama na wewe muda wote huo ambao uliporwa uhuru wako, wewe unaenda moja kwa moja kuonana na kucheka cheka na mtu aliyekusababishia madhila yote hayo uliyoyapitia katika hizo siku 200 na kitu.
Huenda wanafahamiana labda..
 
Kwa hiyo Samia alikuwa anakubaliana na Magufuli katika kumkamata Mbowe, siyo?
IGP , DCI na wateule wengine hawaripoti Kwa makamu wa Rais wanaripoti Kwa Rais, makamu wa Rais anafanya majukumu Yale anayopewa tu na Rais, na siyo lazima ashirikishwe Kila kitu.

Hivyo inawezekana kabisa kuwa alikuwa hata hajui kinachoendelea given the fact kwamba JPM alipenda Mama samia ashughulike na baadhi ya vitu tu kama kumwakilisha kwenye vikao na mikutano mbalimbali ya kimataifa, Magufuli ndiyo chanzo Cha addiction ya Samia ya kusafiri nje[emoji23][emoji23][emoji23]
 

Don’t frustrate yourself over nothing.

Nitazungumzia kimoja tu. Mwaka jana mara baada ya SSH kuapishwa kuwa Rais wa JMT na kumalizika msiba, Mbowe/CHADEMA waliomba kukutana naye mapema wamueleze madukuduku yao na kumpa ushauri. Walishughulika sana kupata appointment hiyo bila mafanikio. Aliwakacha.

Ilipodhihirika kuwa Rais hataki kuwapa heshima hiyo, Mbowe akazindua mikutano kuhusu katiba mpya kwa nguvu moja. Mama SSH akarespond kuwa katiba mpya baadaye; anafufua uchumi kwanza. Mbowe akasisitiza hakuna kurudi nyuma. Ndipo akatekwa Mwanza na kupotea kwenye radar. The rest is history.

Jana jioni nilipoona video ya mama SSH akiwa na Mbowe Ikulu akiongea kama yuko na VIP state guest, I couldn’t help drawing a huge sigh of wonder.

Vyovyote utakavyochukulia, jua kuwa ule ni ushindi mkubwa sana kwa Mbowe. HATIMAYE kaipata ile appointment aliyoipania sana ya kuwa na exclusive tête-à-tête na Rais wa JMT iliyokuwa beamed all over the world. Tena Rais mwenyewe ndiye aliyemualika na kufacilitate kumtoa jela toka kuwa mtuhumiwa wa ugaidi hadi kumfanya VIP state guest. Amekuwa distinguished kabisa na political players wengine nchini. Kaingia level nyingine.

Ni kweli kalipa gharama kubwa sana kuipata hiyo appointment; miezi 8 jela ya kudhalilishwa na kina Kingai na askari magereza. Wewe unaweza kumuona zuzu. Mimi nilivyomu-observe Mbowe kwa muda sasa naamini ni achievement kubwa sana kwake, worthy the cost!

Bila shaka, mahasimu wake huko CCM, upinzani na kwenye vyombo vya dola GANZI iliwapata walipomuona ghafla akipokelewa Ikulu na Rais kwa heshima na bashasha zote hiyo jana. What else could he ask for?
 
You can put on as much lipstick on a pig and it will still be a pig!

Mbowe kakamatwa na kufungwa kipindi Samia ni Rais.

Huo ndo ukweli.
 
You can put on as much lipstick on a pig and it will still be a pig!

Mbowe kakamatwa na kufungwa kipindi Samia ni Rais.

Huo ndo ukweli.
Kwamba amekamatwa kipindi Samia ni Rais hakuna anayebisha, lakini angekamatwa kama kusingekuwa na huo ushahidi uliopikwa Kwa maelekezo ya mwendazake?

Na Je mama alipaswa kufanyaje pale alipoambiwa na wasaidizi wake wenye dhamana kwamba Wana ushahidi usio na shaka kwamba Mbowe ni gaidi?

Mwisho wa siku utagundua Mama Samia hakuwa na option zaidi ya kufuatilia kinachoendelea mahakamani ndiposa akagundua ni ushahidi wa mchongo akaanza kutafuta exit plan.
 
Katika mambo yote 16, kosa la Mbowe ni moja tu?! Alafu makosa ya ccm 15, unawasifu! Huna utu wala ubinadamu, unafanana na shujaa wako mwendakuzimu!
 
Katika mambo yote 16, kosa la Mbowe ni moja tu?! Alafu makosa ya ccm 15, unaosifu! Huna utu wala ubinadamu, unafanana na shujaa wako mwendakuzimu!
Na amekuwa akimsifu JPM kipindi chote ambapo alikuwa akikandamiza demokrasia kipindi Cha JPM Mbowe Kabomolewa bilcanas, kuharibiwa shamba lake, kufungiwa gazeti lake la Tanzania daima, kufukuzwa kwenye Jengo la NHC ambalo kiasili ni Mali yao, kutajwa kwenye madawa ya kulevya na makonda, kuvamia na wasiojulikana na kusingiziwa alikuwa amelewa , kufungiwa akaunti yake na pesa zake kuchukuliwa.

Baada ya kufanya yote hayo watawala walikuwa wamebakisha option Moja tu kumpoteza Mbowe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…