MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,330
Huyu Mary Chatanda aliyesababisha mauaji ya watu sita arusha na majeruhi 11 bado anatonesha kidonda ambacho bado kibichi. Kitendo cha kukosa aibu na kuja hadharani kwa kuanza na kuwakashifu viongozi wetu wa dini na kutamba kwamba uchaguzi wa Meya hautabatilishwa uko pale pale na eti yeye ni diwani halali wa Arusha ni matusi ya nguoni. huku ni kukosa adabu na tunahoji huo ujasiri anautoa wapi wakati bado sisi tunaomboleza vifo vya wenzetu na mazishi bado hayajafanyika. Kukosa hekima ni ugonjwa mbaya kwani huyu mama hana chembe ya hekima wala adabu wakati huu ufumbuzi wa tatizo unatafututwa. Wakati tayari serikali imekubali kujadiliana kutatua tatizo yeye ana complicate tatizo. Huyu mama anatakiwa ashughulikiwe akome ili ajue kwamba watu wana uchungu na arudi kwao tanga kwani vurugu ikitokea ni rahisi kwenda kwao tanga na kuacha watu wa arusha wakiteseka. ametoa wapi ujasiri wa kuongea wakati mwenyekiti wa CCM mkoa aliona vema kukaa kimya. nafikiri bado anahitaji kushikishwa adabu kwa gharama yoyote. Akamuuzlize Dc Elizabeth Minde aliyebomoa vibanda vya wafanya biashara kilichotaka kumkuta. Ilibidi Minde awekewe body guard la sivyo walikuwa wammalize fasta na ilibidi aombe kuhama Arusha kabisa kwa usalama wake. Huyu mama yeye ni nani asifikiri watu ni wajinga na kwamba hawako kusikiliza upuuzi bali kumsikiliza mtu anayetoa solution na siyo kushabikia mauaji.