Hivi mume wake ndio nani hapo kwenye safu ya juu ya CCM kiasi cha kutuletea maafa hivi huyu mama, kweli anajisikiaje hivi sasa na damu hizi kwenye blausi yake?
Mdondoaji elewa Kama ni ugonjwa cause yake imechangiwa na Mary Chatanda. Hii ndiyo source ya ugomvi uliopelekea CHADEMA kupanga maandamano yaliyovurugwa na polisi. Kama mary Chatanda asingekubali kutumika kimabavu kupiga kura batili basi uchaguzi ungekuwa wa halali na yasingetokea yaliyotokea. jaribu kutumia ubongo basi ndugu yangu usipende ushabiki kwani usipende kulazimisha kushiriki dhambi inayoepukika kwa kushabikia wauaji
Ok I can see your point but I fail to undestand it nikuulize kama CCM wamechakachua kwanini Chadema wasiende mahakamani? Na Mary amefanya lipi ambalo limesababisha raia wasio hatia kufa? I am lost but I do not see any logical reasoning hapa huu ushabiki usiofaa kukubalika katika jamii yetu. Hebu fafanua zaidi mkuu.
Ok I can see your point but I fail to undestand it nikuulize kama CCM wamechakachua kwanini Chadema wasiende mahakamani? Na Mary amefanya lipi ambalo limesababisha raia wasio hatia kufa? I am lost but I do not see any logical reasoning hapa huu ushabiki usiofaa kukubalika katika jamii yetu. Hebu fafanua zaidi mkuu.
Huyu Mary Chatanda aliyesababisha mauaji ya watu sita arusha na majeruhi 11 bado anatonesha kidonda ambacho bado kibichi. Kitendo cha kukosa aibu na kuja hadharani kwa kuanza na kuwakashifu viongozi wetu wa dini na kutamba kwamba uchaguzi wa Meya hautabatilishwa uko pale pale na eti yeye ni diwani halali wa Arusha ni matusi ya nguoni. huku ni kukosa adabu na tunahoji huo ujasiri anautoa wapi wakati bado sisi tunaomboleza vifo vya wenzetu na mazishi bado hayajafanyika. Kukosa hekima ni ugonjwa mbaya kwani huyu mama hana chembe ya hekima wala adabu wakati huu ufumbuzi wa tatizo unatafututwa. Wakati tayari serikali imekubali kujadiliana kutatua tatizo yeye ana complicate tatizo. Huyu mama anatakiwa ashughulikiwe akome ili ajue kwamba watu wana uchungu na arudi kwao tanga kwani vurugu ikitokea ni rahisi kwenda kwao tanga na kuacha watu wa arusha wakiteseka. ametoa wapi ujasiri wa kuongea wakati mwenyekiti wa CCM mkoa aliona vema kukaa kimya. nafikiri bado anahitaji kushikishwa adabu kwa gharama yoyote. Akamuuzlize Dc Elizabeth Minde aliyebomoa vibanda vya wafanya biashara kilichotaka kumkuta. Ilibidi Minde awekewe body guard la sivyo walikuwa wammalize fasta na ilibidi aombe kuhama Arusha kabisa kwa usalama wake. Huyu mama yeye ni nani asifikiri watu ni wajinga na kwamba hawako kusikiliza upuuzi bali kumsikiliza mtu anayetoa solution na siyo kushabikia mauaji.
Mimi nafikiri si yeye tu bali hata makanisa ya arusha kusema hawamtambui meya wa arusha ni 'ujinga' maana kiongozi wa kisiasa hatakiwi kutambuliwa na viongozi wa dini fulani. hii inachochea vuguvugu la kidini maana waislam nao wametoa tamko kulaani viongozi wa chadema kwa kusababisha vurugu mkoani kwao. sasa tunaenda wapi?
maandamano yalikuwa na maana na umuhimu gani, wakati lengo lilikuwa kufanya mkutano ili kutoa dukuduku la uchaguzi meya na nini chadema watafanya kupata meya halali kwa mtazamo wao
Tuzingatie maneno ya busara hapa chini kabla ya kutoa misimamo yetu. nimenukuu ktk thread ya jana.
Kadogoo said
Re: Maaskofu watoa tamko la kumkataa meya Arusha
Kanisa heri linyamaze na kufunga mdomo maana kila nikikumbuka mauaji ya kimbari Rwanda huwa nasikitika sana Kanisa linapoongelea juu ya haki! kila nikikumbuka mauaji ya Mwembechai Dar, na kauli alieitoa Padri Lwambano kuwa Serikali iwashugulikie Waislamu wa Msikiti wa Mwembechai na siku ya pili Polisi waliitikia wito huo na kuuwa wananchi wenzetu! nasikitika tena Kanisa kuhubiri haki!
Kila nikikumbuka mauaji ya raia huko visiwani na kauli ya Muadhama Kardinali Pengo kuwa waliouliwa na Polisi huko Zenji ndio wabebe lawama kwa kutokutii amri ya Serikali ya kutokuandamana!!
Sasa, leo Kanisa na Baraza la Maaskofu watakuwa na ubavu gani wa kujitokeza na kulaani mauaji ya Arusha?
Kuna watu wengine wapumbavu watakao fikiri kuwa mimi nafurahia mauaji ya Arusha lakini kwa hakika kila binaadamu mwenye hisia hatafurahia kitendo hicho cha Askari wetu kufyatua risasi za moto na kuua wananchi! ni tendo la kulaaniwa lakini sio Maaskofu wajitokeze leo ghafla na kutoa kilio cha kinafiki! kwanza waombe msamaha kwa maovu waliofanya huko nyuma kwa kuunga mkono maamuzi ya Serikali ya Benjamin Mkapa ya kuuwa raia wa nchi hii na ndipo wafungue ukurasa mpya wa kudai haki za wananchi kinyume chake itakuwa vigumu kuelewa lengo la Kanisa ni nini!
Anko Sam said
Re: maaskofu watoa tamko la kumkataa meya Arusha
Originally Posted by zomba https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ya-wa-ccm-arusha-post1460753.html#post1460753
Hawa maaskofu ndio kiini cha chokochoko, fitna na uzabizabina. Kuna zaidi wanachokijuwa?
Haya, wamkatae meya, sasa wamkatae ana chaguo la mungu. Si walioteshwa?
"Zomba mimi nakushangaa sana, maana siku hizi UMEHARIBIKA KABISA, kwani huko nyuma haukuwa hivyo"
George Jinasa said
Re: Maaskofu wamkataa meya wa CCM Arusha
kwa kulaani vurugu na mauwaji yaliyotokea Arusha mimi ninawapongeza mababa Askofu kwa dhati. Ili hili la kutomtambua Meya mimi nakuwa mgumu kukubaliana nao kwa sababu nyingi. Kwanza, ninauhakika kwamba Maaskofu hawakushiriki katika uchaguzi wa Meya. CCM wanadai Meya wao alishinda. Chadema wanadai Kura zilichakachuliwa. Msimamizi wa uchaguzi alimtangaza mgombea wa CCM kuwa mshindi. Sasa kama Chadema anasema ukweli au CCM anasema ukweli sijua Maaskofu wametumia kigezo gani kubaini. Naamini hawawezi kusema kwa mgombea wa Chaedema alipata kura ngapi na wa CCM alipata kura ngapi tofauti na alivyotangaza msimamizi. Maana, kumbukumbu za kura bado ziko mikononi mwa msimamizi wa uchaguzi.Sababu ya pili ni kwamba usahihi na uhalali wa matekeo umezua mgogoro kati ya CCM na CHADEMA. Maaskofu ni wetu sote. Wanasikiliza maungamo kwa waumini wao walio CCM, CHADEMA, CUF na vyama vingine. Ingekuwa ni busara zaidi kwao kama wangetaka uhalali wa matokeo hayo uchunguzwe na vyombo venye mamlaka ya kufanya hivyo kuliko kuunga mkono upande mmoja kati ya pande zinazogombana.
Makanisa na taasisi nyingine katika sehemu nyingine duniani zinachukua nafasi ya usuluhishi, Kristo anasema "Heri wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu". Kanisa linapoteza sifa hii ya upatanishi kwa kuchukua nafasi katika pande zinazogombana. Tunaelewa pia kwamba taasisi za kidini ni kama wazazi. Wanaweza mara nyingine kutoa sauti ya kukosoa. Lakini hilo linahitaji kufanyika kwa hekima na busara sana hasa pale pana pande mbili zenye ushawishi mkubwa zinapovutana.
Ningewashauri mababa Askofu na viongozi wa dini zingine siku nyingine tujitahidi kuepuka kuchukua nafasi fulani katika pande zinazovutana. Safari bado ni ndefu kwa hali inavyoonesha na mchango wa taasisi za dini unategemewa sana katika kuiweka nchi yetu katika amani. Watanzania bado tunaheshimu sana dini zetu na viongozi wetu wa dini.
kagumyamuheto said
Re: Maaskofu wamkataa meya wa CCM Arusha
Pengine ile dhana ya UDINI ndipo inapoonekana hapa. Mbuni kaficha kichwa kwa muda mrefu huku kiwiliwili chote kikiwa nje sasa kaamua kutokeza kichwa hadharani. Mbona hawakutoa tamko pale dereva wa ccm pale maswa alipouawa na chadema?? Au pale hakuna haki ya kuishi?? Na je, uchaguzi wa meya umefanyika januari??? Why now??
Nasikia harufu ya kumwagika damu kama ile ya rwanda!! Unapoona maaskofu nao wanachanganya dini na siasa ujue ni hatari. Kwani nafasi ya umeya ni ya kuhubiri kanisani???. Au kuwa meya lazima uthibitishwe na kanisa??. Ni kweli taratibu zilikiukwa katika kumpata meya kwani mahakama hazipo?? Taratibu zipi zimefuatwa??
Nasikia harufu ya damu!. Jk andaa jeshi liwe tayari tayari! Nasi pia tupo tayari.
MSAUZI said
Re: Maaskofu wamkataa meya wa CCM Arusha
Hawa Maaskofu wenu ni wanafiki,si ndo hawa waliowahi kusema Kikwete kachaguliwa na Mungu?
Anonymous said
Re: Maaskofu watoa tamko la kumkataa meya Arusha
Originally Posted by Kadogoo https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...amkataa-meya-wa-ccm-arusha-4.html#post1462746
Kanisa heri linyamaze na kufunga mdomo maana kila nikikumbuka mauaji ya kimbari Rwanda huwa nasikitika sana Kanisa linapoongelea juu ya haki! kila nikikumbuka mauaji ya Mwembechai Dar, na kauli alieitoa Padri Lwambano kuwa Serikali iwashugulikie Waislamu wa Msikiti wa Mwembechai na siku ya pili Polisi waliitikia wito huo na kuuwa wananchi wenzetu! nasikitika tena Kanisa kuhubiri haki!
Kila nikikumbuka mauaji ya raia huko visiwani na kauli ya Muadhama Kardinali Pengo kuwa waliouliwa na Polisi huko Zenji ndio wabebe lawama kwa kutokutii amri ya Serikali ya kutokuandamana!!
Sasa, leo Kanisa na Baraza la Maaskofu watakuwa na ubavu gani wa kujitokeza na kulaani mauaji ya Arusha?
Kuna watu wengine wapumbavu watakao fikiri kuwa mimi nafurahia mauaji ya Arusha lakini kwa hakika kila binaadamu mwenye hisia hatafurahia kitendo hicho cha Askari wetu kufyatua risasi za moto na kuua wananchi! ni tendo la kulaaniwa lakini sio Maaskofu wajitokeze leo ghafla na kutoa kilio cha kinafiki! kwanza waombe msamaha kwa maovu waliofanya huko nyuma kwa kuunga mkono maamuzi ya Serikali ya Benjamin Mkapa ya kuuwa raia wa nchi hii na ndipo wafungue ukurasa mpya wa kudai haki za wananchi kinyume chake itakuwa vigumu kuelewa lengo la Kanisa ni nini!
Mkuu asante sana namie nakumbuka hilo tamko na siku mauaji ya mwembechai yalipotokea hakuna Tamko hata moja la maaskofu lilitokea kulaani leo hii wanaleta unafiki wao wa kulaani mauaji ya Arusha. Hakuna mtu anayeyafurahia haya ila tunakemea unafiki wa maaskofu kwa vile kuna muislamu pale juu leo wanajitia vimbembele kukosoa wajiangalie kwanza kabla ya kusema otherwise jamii hasa ya waislamu haijasahau makovu waliyoyaacha kipindi kile cha mwembechai.....
You're lost YES that is why you're Lost in whatever you contribute. We have to find you before we elaborate anything to make your nonsense comments sensible.
Nyani haoni kundule na hilo ndo tatizo lako na we dont have time in this forum to urge with stubborns