CCM yataka vyama vyenye uzalendo

CCM yataka vyama vyenye uzalendo

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2017
Posts
1,605
Reaction score
1,957




KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Bashiru Ally amesema Tanzana inahitaji vyama vya siasa vitakavyozingatia uzalendo na kuwaunganisha wananchi wote.
Dk Ally ameyasema hayo katika ukumbi wa Shule ya Fidel Castro Pemba alipozungumza na viongozi wa CCM wa mikoa ya kisiwani Pemba.
Amesema vyama vinatakiwa kuweka mbele maslahi ya Taifa na si matakwa ya viongozi. Alisema misingi ya uzalendo ni muhimu kwani itawaunganisha wananchi na kurudisha dhana ya uzalendo kupenda nchi na wananchi wake.
“Tanzania inahitaji vyama vya siasa ambavyo vitaweka mbele uzalendo wa nchi kuunganisha wananchi na kuleta maendeleo,” amesema.
Kwa mfano, amesema uzalendo uliooneshwa na viongozi waasisi wa Taifa, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Amani Karume unatakiwa kuigwa ukiwa ni urithi wa taifa letu.
“Wana CCM mnatakiwa kuiga mfano wa waasisi ambao waliweka mbele maslahi ya taifa kwa kujenga Tanzania ambayo leo imekuwa kimbilio la wengi ikiwemo wageni,” amesema.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Dk Abdalla Juma Mabodi amesema, kazi kubwa ya CCM Zanzibar sasa ni kuimarisha chama kwa kuingiza wanachama wengi ikiwemo vijana.
“Kazi kubwa tunayoifanya ni kuimarisha Chama Cha Mapinduzi kupitia Jumuiya zake na kuingiza wanachama wengi zaidi,” amesema.
Dk Bashiru yupo Pemba ikiwa ziara yake ya kwanza Zanzibar tangu alipoteuliwa kukiongoza chama hicho.
 
Uzalendo upi wa kununua wapinzani kisha kututia hasara za Uchaguzi?

Uzalendo upi wa kupiga risasi wakosoaji

Uzalendo upi huo wa kujenga taifa lenye chuki na manung'uniko.

Uzalendo upi kuweka maslahi ya chama mbele kuliko Taifa?
 
Hivi vyama vya upinzani na haswa Cuf na Chadema malengo yao si kuunganisha Watanzania viko kinyume nimejaribu kusoma katiba na ilani ya chama cha UDP kimekaa vizuri na kinaweza kuwa chama kikuu siku za usoni.
Mbona kwenye teuzi za ukuu wa wilaya cjakuona wakati ulitaja listi ya watu hatari au nimekufananisha bwana Kilio a.k.a. musiba

Sent using Jamii Forums mobile app
Jenga hoja kijana penda taifa lako.
 
Masikini Bashiru Ally ! akili yote kaiacha mlango wa kuingilia Lumumba !
 
Cuf kinastawi kwa kupitia mgongo wa kuwatenganisha wazanzibari,bila hivyo Cuf ingefutika huko visiwani.
 
Cuf kinastawi kwa kupitia mgongo wa kuwatenganisha wazanzibari,bila hivyo Cuf ingefutika huko visiwani.
Cuf inapata wawakilishi Unguja na Pemba wakati ccm inaambulia unguja tu , nani anayewatenga wazanzibar
 
Unapoona adui yako anayekuchukia kiasi cha kukutakia kifo anakushauri jinsi ya kuendenda, basi kuwa macho maana inawezekana kuna mtego.
 
Huyu Bashiru ilitosha kubaki pale UD kuficha udhaifu wake!kimsingi Ccm ni chama kama vingine hakina hati miliki na taifa hili! Uzalendo sio kiupenda serikali ya ccm,tunaipenda nnchi iwe inaongozwa na ccm au la!kutofautiana namna ya kuongoza nnchi kwa Bashiru ndio kukosa uzalendo! Huyu ndio engine ya ccm, uzalendo unatafsiriwa na msomi kwa jinsi hiyo. Tuna safari ndefu sana.
 
Back
Top Bottom