Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,963
- 6,693
Katibu wa Idara ya Fedha na Uchumi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jamal K. Ali, amemwomba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi wa masuala ya fedha ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa mujibu wa mamlaka yake kisheria.
Akizungumza wakati wa mapokezi ya wajumbe wa Sekretarieti ya CCM Taifa yaliyofanyika katika Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma, Jamal amesema ukaguzi huo utasaidia kuwaweka wazi Watanzania kuhusu matumizi ya fedha zinazokusanywa na chama hicho.
Soma Pia: Mnyika afafanua tuhuma za Heche na matumizi ya fedha za ToneTone
Jamal amedai kuwa fedha zinazochangwa na wanachama na wananchi zinatumika kwa maslahi binafsi ya baadhi ya viongozi wa CHADEMA, hali ambayo imechangia kupungua kwa imani ya baadhi ya wanachama kwa viongozi wao.
Akizungumza wakati wa mapokezi ya wajumbe wa Sekretarieti ya CCM Taifa yaliyofanyika katika Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma, Jamal amesema ukaguzi huo utasaidia kuwaweka wazi Watanzania kuhusu matumizi ya fedha zinazokusanywa na chama hicho.
Soma Pia: Mnyika afafanua tuhuma za Heche na matumizi ya fedha za ToneTone
Jamal amedai kuwa fedha zinazochangwa na wanachama na wananchi zinatumika kwa maslahi binafsi ya baadhi ya viongozi wa CHADEMA, hali ambayo imechangia kupungua kwa imani ya baadhi ya wanachama kwa viongozi wao.