Hivi hizi jumuiya za chama zina nini? Kwanini huyu tycoon Milionea wa kutupa Mkono analia na kutapatapa ili apewa kazi ngumu ya kuongoza jumuiya ya wazazi?
Hivi katika karne hii mwanachama yeyoyote anaweza ku threaten chama kikubwa kama CCM na watu eti wakahaha kuwa akiwekwa pembeni wengine waendeleze uongozi basi chama kitatikisika au kufa?
Kama baba wa Taifa, J.K. yerere mwasisi wa chama alifika mahala akang'atuka na chama hakikutikisika na sasa hata katangulia mbele ya haki lakini chama kipo na kinaendelea kuwepo sembuse Mkono????????? kweli?????? Eti ana siri? Hivi nani mwenye siri nyingi za chama kati ya Mkono na aliyekuwa Chief campaigner wa rais wetu; aliyewahi kuwa Waziri n.k lakini anafika mahali anasema imetosha wengine waendelee!
Basi, fuateni sauti za watani wenu wa jadi wanaomshangilia Mkono, kuwa huyu jamaa ni kiboko kwamba ana MVUTO na kweli chama kitaendelea sana.
Kidumu chama cha mapinduzi
Ni mimi,
mwanachama nisiye na fedha nyingi wala siri za chama.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.