Not in use
Member
- Jan 15, 2014
- 6
- 2
Mkutano mkubwa wa na wa kihistoria wa uzinduzi wa Kampeni za Udiwani wa CHAMA CHA MAPINDUZI kata ya Sombetini utafanyika leo soko la Mbauda.
Kipenzi cha watu, homa ya CHADEMA Mwigulu Lameck Nchemba Naibu Waziri wa fedha atafungua kampeni hizi pamoja na viongozi wengine wa mkoa.
Mama yetu Mh.Chatanda atatema cheche. Baada ya hapo tutafanya maandamano mji mzima .Rasmi tumekuja kuizika CHADEMA Arusha.
Kaa mkao wa kula nakuletea live yatakayojiri.
-------------------------------
Kipenzi cha watu, homa ya CHADEMA Mwigulu Lameck Nchemba Naibu Waziri wa fedha atafungua kampeni hizi pamoja na viongozi wengine wa mkoa.
Mama yetu Mh.Chatanda atatema cheche. Baada ya hapo tutafanya maandamano mji mzima .Rasmi tumekuja kuizika CHADEMA Arusha.
Kaa mkao wa kula nakuletea live yatakayojiri.
-------------------------------
Naibu Katibu Mkuu CCM Tanzania Bara Mh;Mwigulu Nchemba ameshawasili Jijini Arusha Mchana huu akitokea Kiteto na Babati kwaajili ya Uzinduzi wa Kampeni za Udiwani zinazoendelea nchi nzima,Chaguzi hizi ni ndogo kwaajili ya kujaza nafasi za Madiwani waliojiuzulu na wengine kufariki.
![]()
Naibu Katibu Mkuu CCM Mh:Mwigulu Nchemba akiwa ameambatana na Mgombea wa Udiwani Kata ya Sombetini WIlaya ya Arusha ndugu David,Hapa akiwa kwenye maandamano kutokea Ofisi za chama hapa Sombetini kuelekea Viwanja vya Mkutano,Kulia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha.
Mh:mwigulu Nchemba akipata mapokezi mazito kutoka kwa maelfu ya wananchi waliomiminika Viwanja hivi vya Soko la Mbauda kwaajili ya Mkutano wa hadhara wa kampeni za Udiwani.![]()
![]()
Mapokezi yanaendelea hapa Soko la Mbauda kwaajili ya kuanza mkutano wa hadhara.
![]()
Sehemu ya Mamia ya Wananchi wakiwa tayari kusikiliza Mkutano huu wa hadhara kwaajili ya Kampeni za Udiwani kata ya Sombetini jijini Arusha.
![]()
Wananchi wanaendela kumiminika kwenye viwanja hivi vya soko la Mbauda kwenye Mkutano wa Hadhara wa CCM kumnadi mgombea wa CCM kwenye Kinyang'anyiro cha Udiwani.