mpinga shetani
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 3,234
- 959
Acha wampitishe iwe advantage kwa UKAWA
Akili ya mende. Huyo akipita upinzani unakufa ndani ya wiki moja. Atatumia upanga Mbowe Lema na mijinga yote ya sampuli hiyo ni kaburini
Acha wampitishe iwe advantage kwa UKAWA
Acha wampitishe iwe advantage kwa UKAWA
ni kweli kijana...maana hata NCCR alisafiria nyota ya babake....Makongoro Nyerere?!
Raisi wa nchi ndio head of state, ndio amiri Jeshi mkuu, namaanisha ndio mtu mwenye maamuzi ya mwisho juu ya masuala mengi muhimu ya taifa. Mtu kama huyu ni vyema tukamfahamu vizuri ili tumwamini na kumkabidhi taifa.
Nataka kujua;
Iko wapi rekodi ya utendaji uliotukuka wa Makongoro Nyerere?
Ni wapi alikoonyesha uchapakazi na maamuzi yasiyoteteleka ili tumkabidhi nchi?
Ni lini alishawahi kuchukua hatua au hata kupaza sauti tuu juu ya ufisadi ukiacha sasa Kwa vile tu Ana nia ya uraisi?
Ni kipi hasa alichonacho Makongoro hadi ukadhani anaweza kuongoza taifa letu?
Makongoro ni mtu asiyeaminika, alishawahi kuhama CCM na kugombea ubunge kupitia NCCR Mageuzi, nini kilimtoa CCM na nini baadae kikamrudisha?, je hatuwezi kufikiri kuwa ni mtu asiye na msimamo anayeangalia tu ni wapi iliko fursa?
Taifa linahitaji mtu atayeweza kilikwamua pale lilipokwama, ni yapi maono(vision) ya Makongoro ya kulikwamua taifa?
Vipaumbele vya Makongoro ni nini?, au Hana vipaumbele anasubiri ilani ya Chama itakachokisema na yeye afuate hicho?!! Je kiongozi wa aina hiyo ni kiongozi mwenye maono?
Kutokuwa na kashfa siyo sifa pekee ya kuwa kiongozi bora, anahitajika mtu anaweza kutenda, mwenye uthubutu, mwenye maono, mwenye maamuzi na asiyesita kukemea kila anachoamini siyo sahihi, Makongoro Hana sifa hizi zote!
Mwisho kabisa, Makongoro hana umaarufu au sifa yeyote Kwa wananchi zaidi ya "kusafiria nyota ya baba yake".
Makongoro Nyerere?!
Raisi wa nchi ndio head of state, ndio amiri Jeshi mkuu, namaanisha ndio mtu mwenye maamuzi ya mwisho juu ya masuala mengi muhimu ya taifa. Mtu kama huyu ni vyema tukamfahamu vizuri ili tumwamini na kumkabidhi taifa.
Nataka kujua;
Iko wapi rekodi ya utendaji uliotukuka wa Makongoro Nyerere?
Ni wapi alikoonyesha uchapakazi na maamuzi yasiyoteteleka ili tumkabidhi nchi?
Ni lini alishawahi kuchukua hatua au hata kupaza sauti tuu juu ya ufisadi ukiacha sasa Kwa vile tu Ana nia ya uraisi?
Ni kipi hasa alichonacho Makongoro hadi ukadhani anaweza kuongoza taifa letu?
Makongoro ni mtu asiyeaminika, alishawahi kuhama CCM na kugombea ubunge kupitia NCCR Mageuzi, nini kilimtoa CCM na nini baadae kikamrudisha?, je hatuwezi kufikiri kuwa ni mtu asiye na msimamo anayeangalia tu ni wapi iliko fursa?
Taifa linahitaji mtu atayeweza kilikwamua pale lilipokwama, ni yapi maono(vision) ya Makongoro ya kulikwamua taifa?
Vipaumbele vya Makongoro ni nini?, au Hana vipaumbele anasubiri ilani ya Chama itakachokisema na yeye afuate hicho?!! Je kiongozi wa aina hiyo ni kiongozi mwenye maono?
Kutokuwa na kashfa siyo sifa pekee ya kuwa kiongozi bora, anahitajika mtu anaweza kutenda, mwenye uthubutu, mwenye maono, mwenye maamuzi na asiyesita kukemea kila anachoamini siyo sahihi, Makongoro Hana sifa hizi zote!
Mwisho kabisa, Makongoro hana umaarufu au sifa yeyote Kwa wananchi zaidi ya "kusafiria nyota ya baba yake".
Tuwe wawazi juu ya hili.UKAWA wao wenyewe hawapendi kuteuliwa kwa lowasa.sababu.
1:anakubalika licha ya kwamba anakashfa ya rudhwa
2:kuteuliwa kwake ni pigo kwa ukawa(kutoteuliwa kwake ni faida kwa ukawa)
Takribani ikiwa imesalia wiki moja vikao vya juu vya maamuzi ndani ya chama hicho kukaa na kupitia na hatimaye kupitishwa kwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, tayari makundi yanayohasimiana yameanza kujipanga kukabiliana juu ya kile kinachoitwa udhaifu wa mwenyekiti katika kusimamia chama kikanuni na taratibu nyinginezo. Huku ikijulikana wazi kuwa mmoja wa wagombea tayari ameshakiteka nyara chama hicho kikongwe barani Africa, ni dhahiri sasa mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndg Jakaya Kikwete ameshasalimu amri na kukubalia na hali halisi iliyopo na tayari amebariki kile kinachoitwa mwenye nguvu apitishwe. Huku watendaji wa chama wakijinasibu mikoani kuwa chama hakitampitisha mla rushwa au mtu mwenye kashfa, hali ni tofauti katika shughuli ya kutafuta udhamini. Huku kambi ya Edward Lowassa ikiwa tayari na uhakika wa kupitishwa katika vikao vya chama kutokana na kuwaweka mfukoni mwake takribani wajumbe wengi kuanzia CC, NEC na mkutano Mkuu, kambi nyingine zimeazimia kuungana ili kukabiliana na hali hiyo, taarifa za ndani zinaeleza kuwa Membe, Pinda, Mwandosya, Makongoro, Wassira na Sumaye tayari wamekuwa na vikao vya kujadili kuunganisha nguvu ili kukabiliana na gharika ya Lowassa na katika majadiliano yao wameongelea nini cha kufanya iwapo mwenyekiti atakubali Lowasa apitishwe kiubabe licha ya kuonekana amevunja taratibu za chama toka mapema na katika zoezi linaloendelea, na inasemekana mmoja wa watia kutoka Kanda ya ziwa alitoa pendekezo la kujitenga na Chama na kuungana na upinzani ili kuonyesha kutokubaliana na jinsi mambo yanavyoendeshwa ndani ya chama. Wazo hilo lilileta msuguano na kupata upinzani toka kwa Pinda na ndipo Sumaye alipo sema hatakubaliana kuona fisadi, mwizi akipitishwa na Chama Chake hivyo ni bora wazo la mtoa hoja lifanyiwe kazi. Na mwisho wakakubaliana kufanya kikao cha mwisho wiki ijayo ili kabla kufikia mwafaka wanatakiwa waongee na JK ili kujua nini kinaendelea. Nitawapa mrejesho ijumaa ijayo.
Hayo ni maoni yako binafsi, lakini CCM wanajua nin wana fanya, na Kama unabisha subiri July 12, formula ya kumuondoa huyo mtu ni X,5,3,1. Yaan kwa formula hiyo hawez kupita nakuhakikishia, sisi wenyew tunajua, Kama tuliweza kumuondoa Sita, hamna mtu alieamini Kama kigezo kile kingetumika, so now kuna Vitu tushaplan kwa kutumia iyo formula juu hapo yaan hawez pita nakwambia, Jana usiku wazee wamekutana kazi ishakamilika.
Na hakuna presha Kama unavozania.
Takribani ikiwa imesalia wiki moja vikao vya juu vya maamuzi ndani ya chama hicho kukaa na kupitia na hatimaye kupitishwa kwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, tayari makundi yanayohasimiana yameanza kujipanga kukabiliana juu ya kile kinachoitwa udhaifu wa mwenyekiti katika kusimamia chama kikanuni na taratibu nyinginezo. Huku ikijulikana wazi kuwa mmoja wa wagombea tayari ameshakiteka nyara chama hicho kikongwe barani Africa, ni dhahiri sasa mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndg Jakaya Kikwete ameshasalimu amri na kukubalia na hali halisi iliyopo na tayari amebariki kile kinachoitwa mwenye nguvu apitishwe. Huku watendaji wa chama wakijinasibu mikoani kuwa chama hakitampitisha mla rushwa au mtu mwenye kashfa, hali ni tofauti katika shughuli ya kutafuta udhamini. Huku kambi ya Edward Lowassa ikiwa tayari na uhakika wa kupitishwa katika vikao vya chama kutokana na kuwaweka mfukoni mwake takribani wajumbe wengi kuanzia CC, NEC na mkutano Mkuu, kambi nyingine zimeazimia kuungana ili kukabiliana na hali hiyo, taarifa za ndani zinaeleza kuwa Membe, Pinda, Mwandosya, Makongoro, Wassira na Sumaye tayari wamekuwa na vikao vya kujadili kuunganisha nguvu ili kukabiliana na gharika ya Lowassa na katika majadiliano yao wameongelea nini cha kufanya iwapo mwenyekiti atakubali Lowasa apitishwe kiubabe licha ya kuonekana amevunja taratibu za chama toka mapema na katika zoezi linaloendelea, na inasemekana mmoja wa watia kutoka Kanda ya ziwa alitoa pendekezo la kujitenga na Chama na kuungana na upinzani ili kuonyesha kutokubaliana na jinsi mambo yanavyoendeshwa ndani ya chama. Wazo hilo lilileta msuguano na kupata upinzani toka kwa Pinda na ndipo Sumaye alipo sema hatakubaliana kuona fisadi, mwizi akipitishwa na Chama Chake hivyo ni bora wazo la mtoa hoja lifanyiwe kazi. Na mwisho wakakubaliana kufanya kikao cha mwisho wiki ijayo ili kabla kufikia mwafaka wanatakiwa waongee na JK ili kujua nini kinaendelea. Nitawapa mrejesho ijumaa ijayo.
Kuna hoja nyingi nimeorodhesha, ingekuwa vizuri ukazijibu zote kuliko kujibu moja tu, hata hiyo moja uliyojibu, majibu hayajajitosheleza.ni kweli kijana...maana hata NCCR alisafiria nyota ya babake....
Hata hao wagombea wote wanapenda kumtaja sana babake katika mikutano yao...
Huwezi fahamu mengi juu yake kuhusu kukemea ufisadi maana umekuja juzi katika siasa hizi...ila waulize wajumbe wa NEC wakuibie siri za mikutano yetu.
Vikao vyetu hufanyika ndani ya chama, kuchambana ndani kwa ndani....ni kama ndani ya familia, ugomvi wa baba na mama watoto wasijue.
Mme/mke ukijua mwenzio kakusaliti sio wayasema hadharani kulinda heshima...ila mwawajibishana ndani.
Huku site watu tunawaangalia.....kumbukeni maskini wengi hawahadaiki sasa hiv
Watanzania walilewa Nyerere na bado wana hang over ya Nyerere, Baadhi wanadhani yeyote kutoka ukoo wa Nyerere anafaa!Wavivu wa kufikiria na wenye uwezo wa mdogo wa kufikiria wanaamini eti kwa kuwa Makongoro Nyerere ni mtoto wa hayati Julius Nyerere na kwa kuwa Nyerere anaheshimika sana nchini basi hicho ni kigezo tosha cha yeye kuwa rais wa JMT
haa haa lengo kuingiza wapiga kura wenye mlengo wa mgombea yuleee...
Jakaya fanya ufanyavo wa Tanzania hawamtaki Mgombea wako, Rafiki yako, Mwanamtandao wa Zamani na mchezaji mwenzako wa Basket ball, Mjeshi mwenzako mstaafu, mteule wako alieongoza moja ya mihimili ya serikali,Iache Demokrasia ichukue mkondo wake.
Kufuatia kupanda kwa joto la kumsaka mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia CCM na songombingo la Zanzibar, Kamati Kuu ya CCM (CC) imeitishwa kwa dharura. Nyaraka za kikao hicho zinaonesha kuwa CC itajadili songombingo la Zanzibar na kuanza kupanga nondo za kuchambua na kuchuja watiania wa CCM. Kikao hicho cha dharura kinatazamiwa kuongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete na kitafanyika Dodoma.
Kulingana na taarifa nilizonazo,kikao kitafanyika kesho.CC inagusia pia malalamiko ya rushwa toka kwa watiania waliorejesha fomu. Yametolewa malalamiko lukuki yachomayo kama mkuki hasa juu ya wakati wa kusaka wadhamini mikoani. Ni kutoka kwa watia nia wenyewe. Wapo waliowasilisha nyaraka na shahidi nyinginezo kushuhudia rafu za baadhi ya watiania.JF will be the first to know kitakachojiri kikaoni!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam