CCM yaibwaga CHADEMA katika Umeya jiji la Mwanza

Mkuu jiji la Mwanza limegawanywa hivi karibuni kama ifuatavyo:Kuna halmashauri ya Jiji la Mwanza na pia Halmashauri ya manispaa ya ilemela,kuhusu meya wa ilemela stay tuned mkuu
Hakuna meya Wawil, ilemela watatoa mwenyekiti Wa manispaa
 
tusubiri reliable sources

Mkuu hakuna reliable source itakayo kuja na matokeo tofauti na haya,ukweli unabaki palepale tu kwamba Halmashauri ya jiji la Mwanza imerejea tena mikononi Mwa CCM, CDM tuchange karata zetu tena kwa ajili ya manispaa ya Ilemela.
 
toa mchanganuo vizuri ccm wana madiwani 7 chadema wana madiwani 6 na mbunge 1 cuf madiwani 2 sasa naomba mchanganuo wa kura zako idadi yao wote ni 16 ila kwa kura zako wamevuka idadi je kuna alieongezwa
 
Mgombea wa kiti cha umeya katika Halmashauri ya jiji la Mwanza kupitia CCM na diwani wa kata ya Mkolani Ndg Stanslaus Mabula, ameshinda kiti cha umeya kwa jumla ya kura 11 dhidi ya mgombea wa CHADEMA diwani wa kata ya Mahina Ndg Charles Chinchibera aliyepata kura 8.

Source: Mimi mwenyewe nipo eneo la tukio.

sinaskia nape na wenzake jana usiku walikuwa lakairo hotel wakipanga wanunue umeya kwa sh. Ngapi so wamefika bei.! Ccm hovyooooo.! Ndo chama linakufa hivyo ngoja hela chafu zamafisadi zipigwe pini tuone jeuri yenu magamba nyie
 
Wanabodi,

Leo tarehe 28 2012 unafanyika Uchaguzi wa Meya pamoja ni Naibu Meya wa Halamashauri ya Jiji la Mwanza.

Kamati ya utendaji ya Chadema Nyamagana, kushirikiana na kamati za madiwa wa Chadema zimekamilisha mchakato wa kupata wagombea nafasi ya Umeya na Naibu Meya. Diwani wa Kata ya Maina, Charles Chibara, amepitishwa kuwa mgombea Umeya wa Halamashauri ya Jiji la Mwanza, Chadema wamefanya makubaliano na chama cha CUF ili wapate wingi wa kura na kumpitisha Diwani wa CUF Kata ya Mirongo Daudi Mkama, kuwa mgombea wa nafasi ya Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Siasa aina adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu Chadema wanawaita CUF ni CCM B sababu wameshirikiana na CCM Zanzibar sasa Chadema sijui wataitwaje huko Mwanza.

haiwezekani mkuu CUF washirikiane na CHADEMA, CUF iwapigie kura mgombed wa CCM ili kuwatia adamu siku nyingine watajifunza kuacha kutukana vyama vingine.
 
Back
Top Bottom