BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
CCM yaanika vyanzo vya bajeti ya uchaguzi 2010
Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 28th November 2009 @ 23:59
Habari Leo
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeweka hadharani mkakati wake wa kupata fedha za kugharamia Uchaguzi Mkuu ujao ambapo kuna uwezekano Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho, Rais Jakaya Kikwete akahusika kutembelea mikoa kuhamasisha harambee ya kukichangia chama hicho.
Aidha, chama hicho pia kinapanga kutumia hazina ya wanachama wake karibu milioni nne, kujipatia karibu Sh bilioni 40 kupitia mchango wa Sh 10,000 kwa kila mwanachama. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) Uchumi na Fedha, Amos Makalla, alitoa mkakati huo mwishoni mwa wiki na kuwataka wana CCM nchini kote kujiandaa kujitolea kukichangia chama fedha ili kifanikishe uchaguzi huo.
Akielezea mikakati hiyo mjini Songea mwishoni mwa wiki, Makalla ambaye alipokea maandamano yaliyoandaliwa kusherehekea ushindi wa chama hicho kilichojinyakulia asilimia 97 ya viti vya vitongoji na vijiji katika Mkoa wa Ruvuma, kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika hivi karibuni, pia alitamba kuwa CCM itaendeleza ushindi wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu 2010.
Katika hotuba yake hiyo, Katibu huyo alieleza kwa undani mikakati mitatu ya idara yake itakayopendekezwa katika vikao vya chama hicho hivi karibuni kama njia ya kukipatia chama fedha kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi huo.
Mikakati hiyo inahusisha kuchangisha michango hiyo ya Sh 10,000 ambayo ni ya hiari kwa wanachama, kufanya harambee za mikoa na kuhamasisha michango mingine kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu za mkononi.
"Hapa nina maanisha kama mwanachama mmoja mmoja wa CCM akichangia elfu kumi tena alipe kidogo kidogo kwa miezi sita, chama kina uhakika wa kupata Sh bilioni 40," alisema Makalla.
Amewata viongozi wa mikoa na wilaya kuimarisha kamati zao za uchumi na kuandaa harambee za mikoa na ikibidi katika harambee hizo, mgeni rasmi awe Mwenyekiti wa Taifa na kuhimiza maandalizi hayo yaanze sasa.
Kuhusu njia ya kutuma ujumbe kwa njia ya simu, Makalla alisema si muda mrefu chama kitazindua utaratibu utakaotumika mara baada ya kufanyika vikao hivyo.
Amewataka Watanzania wenye mapenzi na CCM kujitokeza kwa wingi kutuma ujumbe mara baada ya uzinduzi huo kwani kufanya hivyo ni kukijenga chama chao.
Amewahakikishia wanachama kuwa CCM itashinda uchaguzi ujao kwa kishindo kwa sababu ya mikakati kabambe ambayo wameanza kujiandaa nayo.
Ameipongeza serikali kupeleka muswaada bungeni wa uwazi wa mapato na matumizi wa vyama vya siasa wakati wa uchaguzi na kuongeza kwamba muswaada huo umekuja muda muafaka sana na utasaidia vyama kuwa wazi katika mapato na matumizi.
Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 28th November 2009 @ 23:59
Habari Leo
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeweka hadharani mkakati wake wa kupata fedha za kugharamia Uchaguzi Mkuu ujao ambapo kuna uwezekano Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho, Rais Jakaya Kikwete akahusika kutembelea mikoa kuhamasisha harambee ya kukichangia chama hicho.
Aidha, chama hicho pia kinapanga kutumia hazina ya wanachama wake karibu milioni nne, kujipatia karibu Sh bilioni 40 kupitia mchango wa Sh 10,000 kwa kila mwanachama. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) Uchumi na Fedha, Amos Makalla, alitoa mkakati huo mwishoni mwa wiki na kuwataka wana CCM nchini kote kujiandaa kujitolea kukichangia chama fedha ili kifanikishe uchaguzi huo.
Akielezea mikakati hiyo mjini Songea mwishoni mwa wiki, Makalla ambaye alipokea maandamano yaliyoandaliwa kusherehekea ushindi wa chama hicho kilichojinyakulia asilimia 97 ya viti vya vitongoji na vijiji katika Mkoa wa Ruvuma, kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika hivi karibuni, pia alitamba kuwa CCM itaendeleza ushindi wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu 2010.
Katika hotuba yake hiyo, Katibu huyo alieleza kwa undani mikakati mitatu ya idara yake itakayopendekezwa katika vikao vya chama hicho hivi karibuni kama njia ya kukipatia chama fedha kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi huo.
Mikakati hiyo inahusisha kuchangisha michango hiyo ya Sh 10,000 ambayo ni ya hiari kwa wanachama, kufanya harambee za mikoa na kuhamasisha michango mingine kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu za mkononi.
"Hapa nina maanisha kama mwanachama mmoja mmoja wa CCM akichangia elfu kumi tena alipe kidogo kidogo kwa miezi sita, chama kina uhakika wa kupata Sh bilioni 40," alisema Makalla.
Amewata viongozi wa mikoa na wilaya kuimarisha kamati zao za uchumi na kuandaa harambee za mikoa na ikibidi katika harambee hizo, mgeni rasmi awe Mwenyekiti wa Taifa na kuhimiza maandalizi hayo yaanze sasa.
Kuhusu njia ya kutuma ujumbe kwa njia ya simu, Makalla alisema si muda mrefu chama kitazindua utaratibu utakaotumika mara baada ya kufanyika vikao hivyo.
Amewataka Watanzania wenye mapenzi na CCM kujitokeza kwa wingi kutuma ujumbe mara baada ya uzinduzi huo kwani kufanya hivyo ni kukijenga chama chao.
Amewahakikishia wanachama kuwa CCM itashinda uchaguzi ujao kwa kishindo kwa sababu ya mikakati kabambe ambayo wameanza kujiandaa nayo.
Ameipongeza serikali kupeleka muswaada bungeni wa uwazi wa mapato na matumizi wa vyama vya siasa wakati wa uchaguzi na kuongeza kwamba muswaada huo umekuja muda muafaka sana na utasaidia vyama kuwa wazi katika mapato na matumizi.