CCM wamepataje Namba yangu?

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
Mimi ni mteja wa Vodacom (T)LTD. Mara kwa mara napokea matangazo ya promosheni ambayo yanatumwa na Voda au kupitia mifumo ya taarifa nilizojisajili rasmi kama "Clouds Kwanza" nk.

Imeniaribia mudi yangu saaana, nimesikitika sana, nimehuzunika sana na nimekereka sanaaaa kupokea ujumbe huu wa "Kutoa ni moyo unaweza! kuchangia CCM kwa kutuma neno CC Kwenda namba 15377........!. Nichangie CCM, eti CCM ambayo haikuwahi hata siku moja kutumia utaratibu huo kuhamasisha kuchangia maendeleo ya wananchi masikini huko vijijini, leo inataka tena kura!.

Cha ajabu huu ujumbe umetumwa na kampuni ya "PUSH MOBILE" ambayo hata sijawahi kuisikia masikioni mwangu kabisa na sijui ipo wapi na imepataje namba yangu ya simu na inanufaikaje na zoezi hili.

Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, achia mbali CCM ambayo ni Serikali na nilidhani ndio ilipaswa ihakikishe taarifa zangu binafsi kama namba ya simu zinatumika kwa ridhaa yangu lakini inaonekana imehusika kukihuka hilo kwa lengo la kujinufahisha.

Kama utaratibu wa makampuni ya simu sasa upo hivi wa kutoa taarifa za wateja pasipo ridhaa ya mteja husika, kwa nini tusiamini kuwa haya makampuni ya simu yanatumia kinyume cha taratibu taarifa zetu binafsi?. Na kama ndio voda imetoa namba yangu kwa huyo mdudu "PUSH MOBILE" or CCM, je hakuna uwezekano wa kunikata fedha juu kwa juu hata nisipochangia kama sms inavyotaka??..

Nimekereka sana na jambo hili la kutuanika wateja.
 
Ushauri wangu ni kuwa kwanza uwashitaki Vodacom kwa kwa Mamlaka ya Mawasiliano TCRA
 
Mimi ni mteja wa Vodacom (T). Mara kwa mara napokea matangazo ya promosheni ambayo yanatumwa na Voda au kupitia mifumo ya taarifa nilizojisajili rasmi kama "Clouds Kwanza" nk.

Imeniaribia mudi yangu saaana, nimesikitika san, nimehuzunika sana na nimekereka sanaaaa kupokea ujumbe huu wa "Kutoa ni moyo unaweza! kuchangia CCM kwa kutuma neno CC Kwenda namba 15377........!. Nichangie CCM, eti CCM ambayo haikuwahi hata siku moja kutumia utaratibu huo kuhamasisha kuchangia maendeleo ya wananchi masikini huko vijijini, leo inataka tena kura!.

Cha ajabu huu ujumbe umetumwa na kampuni ya "PUSH MOBILE" ambayo hata sijawahi kuisikia masikioni mwangu kabisa na sijui ipo wapi na imepataje namba yangu ya simu na inanufaikaje na zoezi hili.

Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, achia mbali CCM ambayo ni Serikali na nilidhani ndio ilipaswa ihakikishe taarifa zangu binafsi kama namba ya simu zinatumika kwa ridhaa yangu lakini inaonekana imehusika kukihuka hilo kwa lengo la kujinufahisha.

Kama utaratibu wa makampuni ya simu sasa upo hivi wa kutoa taarifa za wateja pasipo ridhaa ya mteja husika, kwa nini tusiamini kuwa haya makampuni ya simu yanatumia kinyume cha taratibu taarifa zetu binafsi?. Na kama ndio voda imetoa namba yangu kwa huyo mdudu "PUSH MOBILE" or CCM, je hakuna uwezekano wa kunikata fedha juu kwa juu hata nisipochangia kama sms inavyotaka??..

Nimekereka sana na jambo hili la kutuanika wateja.


sijuimkama umenishinda mimi kukereka!!
 
I wish I could know kama kuna linaloweza kufanyika juu ya hili kisheria

namaba zetu si personal property? na si private unless nimeridhia mwenyewe kuifanya public?

Ngoshwe tupo wengi tunaokwazwa na hii kitu............
 
I wish I could know kama kuna linaloweza kufanyika juu ya hili kisheria

namaba zetu si personal property? na si private unless nimeridhia mwenyewe kuifanya public?

Ngoshwe tupo wengi tunaokwazwa na hii kitu............

Sina uhakika sana kama kuna "data protection law" kwa Bongo. Lakini katika mazingira kama haya, ni dhahiri kabisa kuwa iwapo makampuni ya simu yanaweza kutoa namba za wateja kwa mtu wa tatu (third party), naona ipo hatari kubwa hata kwa zile taarifa zetu nyingine binafsi ulizotoa wakati wa kujisajili kwa kuhamasishwa na badae kulazimishwa na Serikali kupitia TACRA zikawa zinatumika kinyume na matakwa yetu au malengo husika.

Hakuna usalama tena hapa..unaweza kukuta hao wa makampuni ya simu au wafanyakazi wa makampuni hayo wanamwanga taarifa zetu hovyo au kuzitumia visivyo, kwani kwa mfumo wa nchi ambayo haina sheria ya kulinda taarifa binafis, (Data Protection legislation) hili linawezekana kabisa.
 
Sina uhakika sana kama kuna "data protection law" kwa Bongo. Lakini katika mazingira kama haya, ni dhahiri kabisa kuwa iwapo makampuni ya simu yanaweza kutoa namba za wateja kwa mtu wa tatu (third party), naona ipo hatari kubwa hata kwa zile taarifa zetu nyingine binafsi ulizotoa wakati wa kujisajili kwa kuhamasishwa na badae kulazimishwa na Serikali kupitia TACRA zikawa zinatumika kinyume na matakwa yetu au malengo husika.

Ulipojiunga na mtandao wako (uliponunua SIM Card) uliomba wakupe terms and conditions? Kama hujui terms and conditions za huduma, then huna haki ya kulalamika.

Mimi nimeshafanya kwa kipinidi kirefu kama VAS (Value Added Service) Provider. Na Push Mobile is just my business peer. TCRA wanatoa leseni ya SMS Broadcasting ambayo inamruhusu licensee kutuma ujumbe kwenda kwenye random number.

In short, it's purely legal!

Tatizo watanzania hatuulizii hizi terms and conditions, mpaka pale matatizo kama haya yananapotokea.
 
Ulipojiunga na mtandao wako (uliponunua SIM Card) uliomba wakupe terms and conditions? Kama hujui terms and conditions za huduma, then huna haki ya kulalamika.

Mimi nimeshafanya kwa kipinidi kirefu kama VAS (Value Added Service) Provider. Na Push Mobile is just my business peer. TCRA wanatoa leseni ya SMS Broadcasting ambayo inamruhusu licensee kutuma ujumbe kwenda kwenye random number.

In short, it's purely legal!

Tatizo watanzania hatuulizii hizi terms and conditions, mpaka pale matatizo kama haya yananapotokea.

Mhhhhhhhhhh! ati umesemaje? mbona wakati nanunua hamkunipa terms and conditions?
 
Haya makampuni ya simu ndio yanakosea yanapotuma sms hizo utadhani kila mtu ni mwanachama wa CCM.
 
Haya makampuni ya simu ndio yanakosea yanapotuma sms hizo utadhani kila mtu ni mwanachama wa CCM.

Nina uhakika kina Dr. Slaa, Mbatia, Mbowe Et al hawajapata hizi sms. So lazima kuna some form of control.
hivi kama wanaopata hizi sms wakaamua kuchangia, manoti yatakayopatikana si yatapitiliza ile ceilling iliyowekwa kwenye sheria ya uchaguzi?

Ila wajinga ndio waliwao, Kipindi cha uchaguzi mtaona sisiemu wanamwagama mahela mkiuliza yametoka wapi, mnaambiwa kwenye hii promosheni ya changia sisiem. Kumbe.................................
 
Siku hizi kuna sehemu nyingi ambayo unajikuta unawacha number yako... Siyo lazima uwe umeregister sehemu unavyo wacha bussiness card yako sehemu, kwenye website na vitu vingine kibao tu...

Ni kama unaenda kwenye mikutano unaacha details zako alfu unakuta uko kwenye mailing list fulani tu... Wewe cha kufanya ni ignore hizo msg na wala zisikupe shida. Na siyo kama tuna database fulani ya kuonyesha wewe ni CCM au CHADEMA kwa hiyo yote ni trial and erroe.

POLENI SANA...
 
Hiyo kampuni ya Push Mobile inatafuta hela kupitia hizo message na wanagawana na CCM percent fulani. Ni njia ya kutafuta hela hawana lolote.
 
Nina uhakika kina Dr. Slaa, Mbatia, Mbowe Et al hawajapata hizi sms. So lazima kuna some form of control.
hivi kama wanaopata hizi sms wakaamua

Watu wanaohusika na hizi bulky sms delivery wana exclude namba za watu wakubwa, viongozi wa serikali na mabosi wao maana namba zao wengi zinafahamika. Makabwela ndio wanatumiwa.

Lakini kwa hizi, nadhani hata wakina Kabwe wamepata ... chokochoko za kisiasa si unajua tena!
 
clouds kwanza ni clouds fm waliofunga ndoa ya kufa na kuzikana na ccm......................clouds fm wameanza uhuni wa kuhack yaani kuiba nambali za watu na kuwatumia ujumbe na kuwatoza zaidi ya tsh.300 kwa meseji moja..................mi niliisha lalamika hapa jamvini waungwana walinisaidia japo nilijua walikuwa wadau wa clouds kwani tupo nao jamvini kwa hiyo yule asiyekuwa aware wanazidi kumla kichwa.........................
 
Mi nafikiri haya makampuni yametushoka leo nimepoke nyingine eti nimpigie kura sijui nani...CPWAA! huyu tena ni nani jamani? Naacha kazi zangu kusoma sms! nakutana na CPWAA!! jana nimepata na leo tena!
 
mimi ni mteja wa vodacom (t)ltd. Mara kwa mara napokea matangazo ya promosheni ambayo yanatumwa na voda au kupitia mifumo ya taarifa nilizojisajili rasmi kama "clouds kwanza" nk.

Imeniaribia mudi yangu saaana, nimesikitika sana, nimehuzunika sana na nimekereka sanaaaa kupokea ujumbe huu wa "kutoa ni moyo unaweza! Kuchangia ccm kwa kutuma neno cc kwenda namba 15377........!. Nichangie ccm, eti ccm ambayo haikuwahi hata siku moja kutumia utaratibu huo kuhamasisha kuchangia maendeleo ya wananchi masikini huko vijijini, leo inataka tena kura!.

Cha ajabu huu ujumbe umetumwa na kampuni ya "push mobile" ambayo hata sijawahi kuisikia masikioni mwangu kabisa na sijui ipo wapi na imepataje namba yangu ya simu na inanufaikaje na zoezi hili.

Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, achia mbali ccm ambayo ni serikali na nilidhani ndio ilipaswa ihakikishe taarifa zangu binafsi kama namba ya simu zinatumika kwa ridhaa yangu lakini inaonekana imehusika kukihuka hilo kwa lengo la kujinufahisha.

Kama utaratibu wa makampuni ya simu sasa upo hivi wa kutoa taarifa za wateja pasipo ridhaa ya mteja husika, kwa nini tusiamini kuwa haya makampuni ya simu yanatumia kinyume cha taratibu taarifa zetu binafsi?. Na kama ndio voda imetoa namba yangu kwa huyo mdudu "push mobile" or ccm, je hakuna uwezekano wa kunikata fedha juu kwa juu hata nisipochangia kama sms inavyotaka??..

Nimekereka sana na jambo hili la kutuanika wateja.

kitu kinachoitwa taarifa za siri kwa mteja hakika tanzania hakipo.
Hamna siri katika nchi hii.
Wizi wizi wizi mtupu
 
mimi siku niliyopokea hiyo msg nikaifuta kwa hasira na matusi mazito....kama mwekiti wa chama chao angekuwepo pale angeamrisha mkuu wa majeshi na vijana wake wanishughulikie....ili nipate plasta.
i hates CCM, na watu wake woote, na mambo yake yoote na Viongozi wake woote.....nimeapa kuwa nifie kwenye ballots ikiwa nitaipigia kura yangu.
makampuni ya simu yanatupa fedheha kwa mambo yao haya, kwa mfano mimi namba yangu ya tigo ni hii 071712345.. nawaombeni sana Tigo msiruhusu upuuzi huo kuja kwenye namba hiyo.....
 
"push mobile" si ni kampuni ya Peter Noni yule wa kesi za BOT na EPA? Hujamsikia huyu jamaa?
Hiyo ni kitu ya kawaida sana kwenye makampuni ya simu hasa hawa wenye simu za KADI. Kutokana na kununua kadi yako mtaani, unakuwa huna mkataba wowote na hao wenye kampuni ya simu. Kama kampuni au mtu binafsi una mkataba nao na unalipia kwa mwezi simu yako, basi wakati unaweka sahihi, unaweza kuandikiana nao kabisa kuwa HUTAKI MATANGAZO YOYOTE kwako. Na wakivunja masharti basi unawapandisha kwa Pilato kudai haki yako ya kukuletea neno CCM wakati wee kampuni yako haitaki kabisa kuhusiana siasa kwa mfano.

Mie sijapata kabisa matangazo na namba yangu ni +255 Sefeni fo wah, dabo zero dabo zero hwaan whaa.
 
Back
Top Bottom