CCM wamepata wapi ujasiri wa kupinga ufisadi mwaka huu

CCM wamepata wapi ujasiri wa kupinga ufisadi mwaka huu

nitonye

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2011
Posts
7,349
Reaction score
3,908
Kipindi kirefu serikali ya CCM imekuwa ikituhumiwa kulinda mafisadi pamoja na kelele zote kutoka kwa wapinzani. Sasa mwaka huu umekuwa wimbo wao hadi kuahidi kuwaundia mahakama ya mafisadi kana kwamba mahakama zetu hazina ubavu wa kuwahukumu wala rushwa. Napata mashaka wanaposema mafisadi wameanza kukimbia ccm najiuliza wameenda wapi na ni akina nani? Ufisadi wao ni upi kwa hao waliokimbia wamekwapua kiasi gani serikalini, na imekuwaje wanawaacha mafisadi wanakimbia bila kukamatwa na vyombo vya dola je wamekimbia nchi au bado wapo?
 
Mimi nashauri waachane na haya ya kifisadi. Watueleze watatutoaje hapa tulipo kwa sasa? Elimu bure itatolewaje, kushusha bei ya saruji kodi tutapata wapi, kufufua reli ya kati mikakati ikoje, kupima ardhi yote ya Tanzania itafanyikaje na katiba yetu ya babu Warioba tutaipataje.
 
Haina ubavu wa kupinga ufisadi.wachukue hatua tuone.waanze na escrow na ule mgao kupitia stanbic.vinginevyo ni maigizo!
 
Anza Tibaijuka,Ngereja,Chenge na wale mlo ficha majina yao benk ya stambec,waondoe kwenye kinyan'ganyilo cha ubunge,hapo kura yangu utapata ukifanya hayo,la sivyo utaisoma namba!
 
Eti ufisadi nasikia mpaka Yusuf Manji fisadi wa EPA amepitishwa kugombea ccm.Hivi pesa za EPA zilizorudishwa ni kiasi gani na ninani walizirudisha? Hivi Escrow lile fungu la Stanbic ni nani walikula?
 
Halafu mafusadi wote wa EPA wameachiwa!
 
lakini ''list of shame'' mbona bado iko palepale inapungua taratibu saana.?
 
Kipindi kirefu serikali ya CCM imekuwa ikituhumiwa kulinda mafisadi pamoja na kelele zote kutoka kwa wapinzani. Sasa mwaka huu umekuwa wimbo wao hadi kuahidi kuwaundia mahakama ya mafisadi kana kwamba mahakama zetu hazina ubavu wa kuwahukumu wala rushwa. Napata mashaka wanaposema mafisadi wameanza kukimbia ccm najiuliza wameenda wapi na ni akina nani? Ufisadi wao ni upi kwa hao waliokimbia wamekwapua kiasi gani serikalini, na imekuwaje wanawaacha mafisadi wanakimbia bila kukamatwa na vyombo vya dola je wamekimbia nchi au bado wapo?


Tumepulizia dawa ya kunguni, hatujachoma kitanda.
 
tuanze na makufuri mwenyewe aliuza nyumba za serikali kwa maslahi ya nani, na kwanini watumishi wa serikali sasa wanapanga, je gharama hizo analipa nani, je mauzo ya hizo nyumba serikali imefaidikaje?
 
mambo haya tuyaache tufanye uchaguzi mwenye hela awekeze tupate kodi na ajira kama ni rostam lowassa riziwani,dewji tuache kukumbatia wageni na kujifanya tu masikini ,inaniuma sana Dangote kupewa hekari maelfu kujenga bandar na kiwanda cha sementi ambayo ina soko lisilo kubwa na kubaki tukiwakandia kina mengi rostamNingekua rais ningefanya kama JK na EPA ila ningewaambia watangaze hizo hela kisha waunde umoja kisha nawapa fursa nawakata kodi na vijana wanaajiriwa
 
Kipindi kirefu serikali ya CCM imekuwa ikituhumiwa kulinda mafisadi pamoja na kelele zote kutoka kwa wapinzani. Sasa mwaka huu umekuwa wimbo wao hadi kuahidi kuwaundia mahakama ya mafisadi kana kwamba mahakama zetu hazina ubavu wa kuwahukumu wala rushwa. Napata mashaka wanaposema mafisadi wameanza kukimbia ccm najiuliza wameenda wapi na ni akina nani? Ufisadi wao ni upi kwa hao waliokimbia wamekwapua kiasi gani serikalini, na imekuwaje wanawaacha mafisadi wanakimbia bila kukamatwa na vyombo vya dola je wamekimbia nchi au bado wapo?

Don't you know that the head of Fisadi is a candidate of Ukawa?
 
Back
Top Bottom