CCM walibadilishwa na kardinali pengo - serikali 2

CCM walibadilishwa na kardinali pengo - serikali 2

Status
Not open for further replies.
Katavi, kuna moja kati ya haya mawili; huenda wewe ndiye mwenye upumbavu au umekurupuka bila kuelewa the logic behind my comment

mkatoliki sio mkristo..ndio logic yako.. logic ina definition nyingine siku hizi?
 
Last edited by a moderator:
Kama hili nalo unahitaji kujibiwa basi mjadala huu ni mkubwa sana kwako!!!!

Ukubwa wa mjadala inamaanisha haujibiki au ? Nimeomba ufafanuzi wa namna kadinali Pengo alivyoibadili Ccm !
 
Tatizo ni kwamba kuna watu wanadhani wanalijua Kanisa kumbe hata chembe hawajui.....
 
mleta mada ni mpuuzi, kwanza kkkt wapo wengi kuliko waroma! hakuna ukweli wowote hapa zaidi ya siasa za kizandiki
 
Yanmkini hapo kuna ukweli. Binafsi sikufulahishwa na kuweka wazi msimamo wake. Na kwa kuwa yeye ni kiongozi mkuu wa dini na dini kubwa, kama ilivyo sentesi inayotolewa na Mh Rahis mahali popote pale haijalishi ni mahali gani, kichama au serikali, inachukuliwa kama agizo kwa watu walioko chini yake. Kwa mantiki hiyo hiyo na kwa vyovyote vile tamko la Kadinali Pengo na lilivyotangazwa na vituo mbali mbali vya habari, msimamo wake yamkini ulitafsiriwa na serikali kama ni tamko la kanisa.

Kadinali Pengo sio msemaji wa kanisa katoliki,
Kanisa katoliki hutoa matamko yake kutipitia baraza la maaskofu, alichotamka kadinali ni maoni yake binafsi maana kuwa kiongozi wa kanisa hamkumnyimi kutoa maoni juu ya muundo anaoutaka, ninachoshauri tu ni kuwa viongozi wa dini wachunge maneno yao na hasa wakati kama huu ili kuepusha upotoshaji unaoweza kutokea kwa kutumia kauli zao.
kuna askofu mmoja yuko dodoma kweny BMK ameonesha ushabiki wa ajabu kwa ccm, badala ya kusimamia anachokiamini, anakemea matusi ya upande wa waliowachache kana kwamba waliowengi hawatukani wala kuwadhalilisha wenzao. Tuache njaa na kutumika tutawagawa wananchi,
 
Mtoa maada cjui amesoma na kuelewa mpaka darasa la ngap! Maana heading na alichoandika ndan Hamna relation kbsa, kawabadilsha VP? Wap na Ln? Maoni ya pengo cyo ya kanisa katoliki na ictoshe mwenyekiti WA binge kaonana na pengo na sheikh mkuu muft ili watoe ushaur kwa yale yanayotokea bungen, mbona maoni ya muft hamyasemi au yy hakuongea neno? Jaribu kufikur kwa kutumia ubongo wako
 
Msipende kuchochea chuki ambazo hazipo kabisa.... Mnapokuwa mna jambo la kulishughulikia lazima muwe na focus..... Hapa tunazungumzia Zanzibar na Tanganyika na Serikali ya muungano.
Mtali.
Mchochezi ni Lukuvi.
Wakati suala limefikia kiongozi mwandamizi serikalini kwenda kuwaambia kanisani kuwa ni kwa ajili ya Ukristo ndiyo maana CCM wanaungangania mfumo wa serikali mbili basi kama kanisa halioni umuhimu wowote wa kujiweka mbali na kauli za kina Lukuvi ujue kuna tatizo hapo.

...Kanisa lazima litoke pangoni vinginevyo ndiyo uchochezi wenyewe huo.
 
Mimi ni mkristo mkatoliki nalijua kanisa langu kwa undani kabisa. Masimamo wa kuipinga tume ya WARIOBA ni shinikizo la KARDINALI Pengo kwa maslahi ya kanisa katoliki huko Zanzibar. Ni kweli matukio mabaya yamefanyika na serikali ya CCM kushindwa kuyashughulikia na hata kutoa majibu. Kumekuwa na juhudi ZA kuidhibiti zaidi Zanzibar. Tukumbuke JK alishawambia CCM wajiandae kisaikolojia kupokea serikali 3 na kusaini rasimu zote. Mnajiuliza maswali nini kimetokea na Watu kubadilika ghafla hata wale waliokuja pamoja mfano wajumbe wenye nguvu wa Zanzibar ? Nawapa jibu hapo. Binafsi nimewaelimisha viongozi wangu wa dini falsafa ya ukristu ya kwenda pole pole kama alivyoshauri Gamaliel kwenye kitabu cha matendo ya mitume. Kuikandamiza Zanzibar sio kuimarisha ukristu . Kama alivyolia LYatonga MRema 2005 kwa KIlaini na Mimi nalia Leo kwa Askofu wangu KARDINALI Pengo. Umeiharibu Tanzania. Amani kwanza serikali baadae.
[h=2]Askofu Kakobe kuzungumzia muundo wa Muungano katika Neno la Pasaka 20.4.14[/h]
Taarifa zilizopatikana kutoka kwa waumini wanaosali katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), linaloongozwa na Askofu Mkuu Zachary Kakobe, zinaeleza kwamba, Jumapili iliyopita katika Ibada Kuu ya Kanisa hilo, lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge, Dar-Es-Salaam, karibu na Mlimani City; Mzee wa Kanisa anayehusika na matangazo, alitangaza kwamba, katika Ibada Kuu ya Sikukuu ya Pasaka, Jumapili hii tarehe 20.4.2014, Askofu Kakobe atahubiri Neno la Mungu, ambalo pamoja na mambo mengine ya rohoni, litazungumzia pia juu ya mustakabali wa nchi yetu, hususan kuhusu Bunge Maalum la Katiba, linaloendelea na vikao vyake, mjini Dodoma. Hata hivyo, taarifa za uhakika zilizopatikana jana, kutoka kwa baadhi ya Viongozi wa Kanisa hilo, zinafafanua kwamba, Askofu Kakobe, atachukua muda mrefu zaidi katika mahubiri yake, kuzungumzia juu ya muundo wa Muungano unaoifaa nchi yetu.

Ibada Kuu ya Pasaka katika Kanisa hilo, itaanza saa 3 kamili asubuhi, na kumalizika saa 6.30 mchana. Hata hivyo, kwa kuzingatia Kanuni za Maadili ya Mavazi, za Kanisa hilo; Viongozi hao wa Kanisa, wamewakumbusha watu wote watakaohudhuria, kumheshimu Mungu kwa mavazi watakayoyavaa. Watakaovaa vimini, jeans, milegezo, na nywele bandia; hawataruhusiwa kuingia katika Nyumba hiyo ya Mungu. Vilevile, wanawake hawapaswi kuvaa suruali, na wanatakiwa kufunika vichwa vyao. Vivyo hivyo, wanaume hawakubaliki kuingia Kanisani humo, wakiwa wamevaa kofia.​
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom