CCM waanza kumgeuka Rais Magufuli

CCM waanza kumgeuka Rais Magufuli

Mbowe ameshindwa kulipa kodi billicanas na kufukuziliwa mbali kwa sababu uchumi mgumu.


Hata hili ufipa hamuelewi??
Haya, rudi kwenye mada. Mbunge wa CCM ashindwa kujizuia na kusema hali ya uchumi chini ya serikali ya JPM ni mbaya sana! Changia hoja hiyo
 
Bandarini mizigo imepungua na wafanyabiashara wamekimbia bandari yetu...sasa tushauri tufanye nini?

Naona ili madereva wa malori waendelee kupata kazi Serikali iwaachie wafanyabiashara wapite bila kulipa kodi bandarini...ili uchumi ukue na sie mama ntilie huku mitaani tuonje mema ya Serikali yetu...

Hii itafanya UKAWA wafurahi na kuipenda Serikali yetu. Pia Serikali iache kuwabana mafisadi ili hayo mafisadi yalete pesa mtaani yajenge majumba na sie mafundi ujenzi tupate kuonja mema ya duniani...kuyaacha mafisadi kutafanya UKAWA waiunge mkono Serikali...

Serikali iache kuwabana watumishi wake ili wafanye kazi wanavyotaka na kwa uhuru na wapeane maposho ambayo yatasaidia kukuza uchumi mitaani. Maana mitaani pesa imeadimika. Watumishi hao wazembe wakiachwa wataipenda Serikali na Rais wetu mpendwa..
 
wabunge wa fisiem wanachoongea cha kweli nisalamu tu.mambo vipi? atakujibu poa. vingine vyote uongo mtupu.

Hata hiyo salamu anakuwa anakudanganya... Make kwa uhakika mambo ni poa kwake yeye mwenyewe!
 
He! Leo hii mmeanza kumkubali huyo Mlinga? Kwa nini sasa hamkumuelewa wakati ule?
Ujue kwamba watu hawapendi au ku.chukia mtu kwa uzawa, kabila, dini, rangi ama imani yake ya kisiasa, bali vitendo na matamshi yake. Ukiamua kuwa shetani watu watakulaani tu! Wewe endelea kufata upepo
 
Nilijua amechangia anayejielewa kumbe huyo wa sanamu ya Diamond!
Yaani hata mimi nimechefuka kukuta hivyo mkuu Gide MK hivi kweli achangie yule wa nkasi,wa mtela, wa bange au huyu wa diamond...halafu mtu uchukulie kwa uzito si matumizi mabaya ya energy
 
Wachumi wa Tanzania,mamlaka ya TRA,wanashindwa kufahamu umuhimu wa uzukaji wa Pesa wao wanachokifiria ni kupandisha kodi ndio ukuwaji wa uchumi na mapato,kila siku tunasikia kodi za maajabu zinawekwa sehemu tafauti kuanzia bandarini,Utalii nk

Kupandishwa huko kwa kodi za maajabu zimefanya biashara nyingi kufungwa, watalii wamepungua kuja Tanzania ,haya yote wanaifanya Tanzania kukosa mamilioni ya mapato.

Mambo yote hayo bado utasikia wachumi wetu bado wakiema "kama watu hawawezi kulipa wafungiwe au waondoke tu au hatuwezi kukosa watalii watakuja tu,tunataka watalii wenye hadhi...bla bla bla"

Ushauri wangu serikali ipunguze kodi zinazowaumiza wananchi,kufanya hivo itawasaidia watanzania kuweza kunufaika katika biashara zao,kwani watanzania wakizidi kufungua biashara serikali itazidi kukusanya kodi,mizigo itazidi kumiminika bandarini...

Kinachoendelea hivi sasa hakuna mzunguko kila kitu kimekwama.,muuza vitumbua hawezi kuuza vitumbua hakuna mnunuzi,Nyumba za wageni hakuna wa kulala,Baa zimefungwa hakuna mywaji kwa sheria za kipuuzi...nk

Sasa serikali ifikirie kama sekta zote hizo zitafungwa ua wataamua kupunguza wafanyakazi,mtanzania wa maisha ya chini atafanya nini,vipi watanzania watalisha familia zao...

kama hali itaendelea hivi tusubiri makubwa,,, "This is the begining of the end".....

Serikali ifikirie kuwawezesha raia wake sio kuwaadhibu kwa visasi nakejeli,ikifanya hivyo tutafika tunapotaka kwenda....
 
Taarifa za Benki Kuu zilizopo kwenye tovuti yake (Quarterly Economic Review na Monthly Economic Review) kwa robo ya mwisho ya mwaka 2015 (Oktoba – Desemba 2015 ) zinaonesha kuwa kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa ilikuwa 9%. Katika robo ya kwanza ya mwaka 2016 (Januari – Machi 2016) kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa ilishuka hadi kufikia 5.5%.
Hali kama hii ni ya kawaida sana hasa ukiangalia ilikuwa tumekabiliwa na uchaguzi mkuu. Kushuka huku kwa muda inawza kuwa imetokana:-
1. Matumizi makubwa yaliotumika katika kipindi hicho kuyakabili "mashughuliko" ya uchaguzi
2. Hofu ya wafanya biasharana kuchukua tahadhari na hivyo shughuli kubwa za kibiashara husimama au kudorora.Hali hii itatengemaa siku chache zijazo.
 
Back
Top Bottom