Kati ya Rais na PAC ni yupi alikuwa mwongo ? Rais alisema mpaka Escrow account inafungwa kwa mujibu wa ripoti ya CAG mlikuwa na pesa 202 Billions PAC wanasema mlikuwa na 306 Billions na ndio pesa zilizoibwa, Rais alisema kabla ya kufunguliwa kwa account ya Escrow IPTL walikuwa wanapeleka invoices zao Tanesco nao walikuwa wanalipa moja kwa moja kwa IPTL, baada ya Tanesco kuhisi wanalaliwa na IPTL ikabidi watoe notice kwa IPTL juu ya kutokubaliana na malipo hayo hivyo basi wakalazimika kufungua Escrow ili Tanesco badala ya kuzipeleka pesa zile IPTL waziweke kwenye account hiyo ya Escrow , lakini kwa mashart kwamba IPTL wataendelea kusubmit invoices zao kwa Tanesco za kiwango kilikile kilichokubaliwa na Tanesco kwa mujibu wa hukumu ya ICSID,si vinginevyo mpaka swala lao litakapopatiwa ufumbuzi.kwa muda wa miaka saba hapakuwa na ufumbuzi juu ya swala lile kwa uelewa wangu mdogo IPTL haikuwa na wajibu wa kukokotoa viwango vipya vya capacity charges kwa sababu hawakuwa na madai, bali Tanesco ndio walipaswa kufanya kazi hiyo na kuwapa IPTL ambao nao wangeipitia na kuikubali ama kuikataa, lakini hata wangekubali bado wangelazimika kukubaliana ni lini viwango hivyo vipya vianzie(Mwaka). sasa kwa miaka saba hapakuwa na viwango vipya na kwa nini IPTL asisema kwamba pesa zile ni zake kama ilivyokuwa awali kabla ya kufunguliwa account hiyo ya Escrow? jiweke wewe katika nafasi hiyo ya IPTL, hivi ungesema pesa ile iendelee kubaki kwenye account ya Escrow wakati huo pia unaendelea kutoa huduma?.
Kwa mtazamo wangu kosa kubwa limefanyika kwa Tanesco kushindwa kukokotoa viwango vipya, hata PAC nao walishindwa kuwashauri Tanesco ama kuwasaidia kukokotoa viwango hivyo vipya maana mpaka wanatoa ripoti yao hawakuonyesha endapo viwango vipya vingekokotolewa Tanesco ingeweza kuokoa kiasi gani,alafu katika ulimwengu huu wa utandawazi sio jambo jema kushawishi wengine wakubaliane na mawazo yako kwa matusi , kejeli, na hata vijembe bali hoja pekee ndio zitafanya watu wakubaliane na wewe, hivi leo ukisema Rais ni mbumbumbu kwa sababu tu alichosema wewe haukkubaliani nacho, una hakika gani kwamba yale unayoyaamini wewe wote wanakubaliana nayo? mizani gani ambayo wewe umeitumia kupima uzito wa hoja zako na kuona kwamba zina unzito kuliko za Rais?.