CCM: Tutajidanganya Hadi Lini?

CCM: Tutajidanganya Hadi Lini?

Usikurupuke kujibu bila kusoma post nzima. Ni nini mapungufu ya hii post? Au unataka sisi tukuelewe vipi? Ni wapi mtambuzi amesema yeye ni chadema? Wakati mwingine jaribu kujibu hoja sio kukurupuka na kuanza kuitaja taja chadema. Dr slaa amefuata nini tena kwenye hii post?
Ndugu yangu Mchambuzi kutoka Mtaa wa Ufipa Kinondoni Zipo aina tatu za Propaganda
1.Yellow
2.Black
3.White
Wewe upo namba 2,ni propaganda ya adui kujivika sura ya kirafiki na akakushauri!
Binafsi nimekugundua unatoka Mtaa wa Ufipa kwenye nyumba ya kupanga Kinondoni,washauri viongozi wako wa Chadema ambao naamini baadhi ni vichaa kama Godbless Lema,Dr Slaa ambae juzi alitaka kumzoea Profesa Baregu akampiga stop!
 
Kwangu mimi, Mchambuzi nakuchukulia kama Mwl. wangu, najifunza mambo mengi toka kwako hata kama uko na magamba, kiukweli ID yako inasadifu unayoyafanya hongera sana. Ninachokubalinana na wewe ni kwamba leo hii, hata kama chama kingine kikingia madarakani, utawala hautakuwa wa mteremko kama vijana wa Lumumba wanavyotaka kujidanganya. Nina ushahidi wa baadhi ya maeneo ambayo CDM inaongoza vijiji lakini wenyeviti wake wamefukuzwa uongozi na kurudisha CCM kutokana na ubadhilifu, kwahiyo anayekupinga na kukutukana kuwa unasaidia wapinzani hiyo ni shauri yake lakini ukweli ni kuwa zama za sasa ni tofauti
 
Huyo njaa inamsumbua tu wala hayo si mawazo yake.
Wajinga na wehu ni sehemu ya viumbe wa Mungu wetu mwema.

MCHAMBUZI, amefanya uchambuzi basic na mwenye uhai na uwezo wa kusoma basi asome kwa faida ya chama cha Mapinduzi.
 
Ninyi watu wa Lumumba mnashauriwa mnajishaua! Hilo ndo tatizo lenu. Akili zenu kuna mtu anazikontroo.
mkuu umetumia mwezi mzima kuandika hii makala , amabayo imenichukua dakika mbili, kuona ni ya kijinga...
 
Mchambuzi, that's another master-piece article by you, kudos!

In the cold light day I love the fact they will merely attack, vilify and threaten you and thus miss-out the remedy you provide therein.

So let them alone. They're jet-speed in that destruction-lane, so let none of us stop them now!
 
Uzuri ni kwamba nimeshajadili kwa kina aina yenu ya wana lumumba katika bandiko namba moja;

Lakini naomba nikuulize tu - Je, kauli ya Mwalimu Nyerere mwaka 1987 miaka nane kabla Chadema kuzaliwa alikuwa katika kundi gani la hizo propaganda? Kwani mada yangu msingi wake ni maneno ya Mwalimu 1987, ambayo yanazidi kunifungua macho, hata kama mshindani wa CCM ingekuwa ni Chama cha soka Tanzania (TFF);

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Wala hatarudi huyu kukujibu. He would rather label you or call you a funny name than engage you in an honest debate.
Hapo ndipo walipo CCM leo. Kwao ni vijembe tu, kejeli na matusi.
 
mkuu umetumia mwezi mzima kuandika hii makala , amabayo imenichukua dakika mbili, kuona ni ya kijinga...


Hiii kweli stroke,inaonesha aujasoma hata kidogo,hizi buku 7 za lumumba,zitawapa uchizi safari hiii.
 
...KOLIMBA yeye alisema kwa ufupi lakini kwa maana kubwa sana "CHAMA CHA MAPINDUZI HAKINA DIRA/KIMEPOTEZA MWELEKEO", hawakumruhusu afafanue alimaanisha nini,kama wangempa nafasi ya kumsikiliza na kuyafanyia kazi mawazo yake,leo CCM ingekuwa na nafuu fulani...
 
Mkuu Mchambuzi nikupe hongera sana kwa kuendelea kuweka wazi na kushauri pale unapoona inafaa kwa mustakabali wa taifa letu.

Tatizo kubwa linalowakabili watawala wetu na hao vijana wa Lumumba ni kuwa hawataki kuambiwa ama kuona mtu yeyote akiongea ukweli. Kwao wanachotaka kwa sasa ni kuona wanaabudiwa na kunyenyekewa ili waendelee kutawala na kuchota rasilimali za taifa kwa faida yao na familia zao na si vinginevyo.

Ni jambo la kusikitisha na kutia aibu kuona kijana mwenye akili timamu kabisa anakubali kupumbazwa na kushabikia mambo ya kijinga na yasiyokuwa na tija yoyote kwake binafsi na taifa ili tu apate shilingi elfu kadhaa (tano, saba au hata kumi) ambazo hazimsaidii lolote kwa maisha yake ya baadaye.
 
Nimependa uchambuzi wako. Tatizo nadhani vijana wengi wa CCM (isipokuwa vijana kama Bashe) wanafikiria kupitia MATUMBO! We mcheki kama mdogo wangu Nape au Mzee Steven Wasira! Matumbo makubwa na wanataka kuyalinda yaendelee kupata neema kupitia utawala unaoonekana kupoteza muelekeo. Najua vijana wengi wa CCM wataona ulichokiandika ni upuuzi ila siri nikuambie ni kuwa "HAWASOMI MSTARI KWA MSTARI" yaani wao ni heading tu, na kutoa conclusion wewe ni mpinzani wa CCM ndani ya CCM "mfano wa akina Mwigulu"
 
Mchambuzi this article is a masterpiece written in plain language to fit all of us except for some unique fools such as Mwigulus, Napez and Kinanaz, i recommend this article to be read by all politicians on daily basis immediately after getting off bed to start their political activities of the day.
 
Ndugu yangu Mchambuzi kutoka Mtaa wa Ufipa Kinondoni Zipo aina tatu za Propaganda
1.Yellow
2.Black
3.White
Wewe upo namba 2,ni propaganda ya adui kujivika sura ya kirafiki na akakushauri!
Binafsi nimekugundua unatoka Mtaa wa Ufipa kwenye nyumba ya kupanga Kinondoni,washauri viongozi wako wa Chadema ambao naamini baadhi ni vichaa kama Godbless Lema,Dr Slaa ambae juzi alitaka kumzoea Profesa Baregu akampiga stop!
We have known Mchambuzi for quite a long time as a good CCM supporter. Na amesimama kidete kuitetea CCM wakati wowote. Na ninyi mlimuunga mkono kwa kauli zake za kuitetea CCM. Leo kwa kuwa amewapa ukweli mchungu, mmegeuka na kumwita CHADEMA?

Nakushauri mambo yafuatayo Mlengo wa Kati: La kwanza jibu hoja ya Mchambuzi kutokana na quotation za mwalimu Nyerere! Je huoni kwamba aliyosema Nyerere yanatimia kutokana na watanzania kukosa matumaini? Pili jibu hoja ya Mchambuzi kuhusu adui mkubwa wa CCM? Kwanini CCM mnaendelea kuwa na mtizamo finyu wa kuamini kwamba CHADEMA ndiyo adui mkubwa wa CCM hivi sasa na si matumaini yaliyopotea ya watanzania?

Na je mnaupokea ushauri wa Mchambuzi kwamba mkubali kuendesha siasa za kistaarabu na kutunga kanuni na sheria zinazoruhusu demokrasia ya kweli kwa kuwa ipo siku na ninyi mtakuwa chama cha upinzani?

Tunawaona tu mnavyoandika katiba, mmeng'ang'ania kuweka vipaumbele vya CCM huku mkisahau kwamba vipengele mnavyoviweka vya kuuumiza upinzani, vitawaumizeni wenyewe miaka mitatu tu ijayo hapo mtakapokuwa mpo upande wa upinzani.

CCM chukueni ushauri wa mtambuzi kwa faida ya nchi na ya chama chenu.
 
Mchambuzi, nimeisoma makala yako kwa umakini mkubwa, na nakiri kuwa kuna mambo nimejifunza, ingawa hayakuwa mageni sana lakini yameniongezea maarifa.

Ndani ya chama chetu CCM, kwanza kabisa hatujabadili mfumo wa siasa, hii ina maana siasa zetu ni zile za chama kimoja kikiwa mamba na vyama vingine vikiwa dagaa.

Lakini kumbe ukweli ni kuwa, siasa ya hapa nchini imebadilika, inataka kuona ahadi zikitekelezwa na sio ahadi zikibadilishwa tarehe, kwa mfumo huu wa siasa ni changamoto kwa viongozi wanaounda serikali.

Kikubwa ninacho kiona kuhusu viongozi wanaounda serikali ni udhati wa kutumikia taifa, hapa nakiri kuwa viongozi wengi wa CCM wanaounda serikali hii ya Kikwete wengi ni weupe, nikimaanisha ni wachovu kiutendaji. Kama tungekuwa na baraza la mawaziri lililo sheheni watu kama dr. Mwakyembe, dr. Kagasheki and the like, hali ingekuwa si haba katika kutekeleza ilani ya chama.

Katika kasi ambayo CHADEMA wanalipeleka taifa, katika hali ya kuwaaminisha wananchi kuwa serikali ya CCM inapaswa kuwapa zaidi ya inachokitoa kwa jamii, na ukweli ni kwamba, CHADEMA wana hoja za kuthibitisha kauli zao hizi, hoja zenyewe ni kama ufisadi, misamaha ya kodi, matumizi makubwa ya fedha kwenye shughuli za kawaida n.k, basi serikali yangu kwa kipindi hiki kifupi ijitahidi kuendana na kasi ambayo CHADEMA wanaaminisha watu, jambo ambalo lipo ndani ya uwezo wa serikali.

Hapa naona kabisa serikali yangu inalazimishwa kukata viuno kwenye ngoma wanayoipiga CHADEMA, kama vijana wameyapokea mapambano na kuungana na jitihada za CHADEMA katika kuleta mabadiliko, hii hiwe changamoto ndani ya serikali ili kukinusuru chama chetu kwenye uchaguzi mkuu wa 2015.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi this article is a masterpiece written in plain language to fit all of us except for some unique fools such as Mwigulus, Napez and Kinanaz, i recommend this article to be read by all politicians on daily basis immediately after getting off bed to start their political activities of the day.
Maybe it should be recommended for publication in one of the most reputable news papers.
 
Umeandika mambo ya maana sana mkuu.ya maana sana.ya maana sana.narudia tena ya maana mno.nina uhakika wewe si mtu wa kawaida sema tu tunatumia ID's humu.kuna tatizo moja tu ambalo linanisikitisha sana.ukiangalia baadhi ya post humu utagundua kuwa hatuna jamii iliyotayarishwa kwa hayo uliyoyaeleza hapo juu.Nina wasiwasi hata tukibadilisha uongozi hatuta meet expectation zetu kwa sababu jamii imejaa "vichwa vya lumumba".wengine wako Chadema,wengine CUF n.k lakini sera zao ni zile zile.hawajionyeshi kwa vile hawajapata playground na resources.naona kazi kubwa sana.kazi ya ku-shape jamii na viongozi wake kwa wakati mmoja.hii inagusa mfumo wetu wa elimu na uongozi kwa kila level yaani hata balozi wa nyumba kumi!mimi naona tunahitaji mageuzi makubwa ndani ya misingi ya jamii yetu halafu jamii hiyo itautengeneza uongozi huko juu na kuzalisha watu watakaoyaishi maneno yako ya hekima nyingi.pia ni lazima kuwe na mfumo unaondaa viongozi kutoka chini.ndugu yangu nikuambie ukweli hadi leo siamini kwamba very ordinary people wasio na talents zozote za kuongoza,wahuni tu wa mtaani wameweza kupenya system nzima ya chama na serikali hadi kuwa viongozi wakuu hivi!hata huu uzi wako unaweza kupewa nafasi ya kuzungumza na viongozi wa ngazi za juu sana wasikuelewe kabisa!hii inatisha.hatuwezi kuwa na mfumo wa kupata viongozi ulio vulnerable kwa kila mtu hata mwizi wa mifukoni hivi!we have a serious problem!siwashangai wanaokuponda humu na wengine kukwambia wanasikia usingizi wakisoma huu uzi.hawa ni reflection nzuri ya jamii ambayo inataka mabadiliko bila kuelewa njia na gharama ya kuyapata.lakini ndio hawa hawa (wanaosikia usingizi ) watakuwa mawaziri na marais baadae!kazi tunayo!
 
Dah we jamaa una akili aisee!
Kama unatendaga kama unavyofikiri bado Taifa lina think tanks nyingi
Mungu akupe uhai Mchambuzi

Hilo gazeti naweza pata scanned copy?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom