Uchaguzi 2020 CCM tutafanya makosa makubwa kama tutajaribu kuzibeza hoja za Tundu Lissu

mcoloo

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
918
1,401
Tundu Lissu tayari ameshaonyesha wazi kuwa ni mwiba mchungu kwa CCM kuelekea kwenye kampeni, kwa muda mfupi aliopanda kwenye majukwaa yasio rasmi kwa ajili ya kampeni ameoneka kuwa Ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kujenga hoja zitakazo wabadilisha wengi mawazo hata kwa WanaCCM wenyewe.

Huyu Tundu ana uwezo mkubwa sana wa kujieleza, kujenga , na kutetea hoja kuliko watu wanavyo fikiria.

Na kwa vile Watanzania wa leo wengi hawana tena ushabiki wa vyama kama zamani, ni rahisi sana kuoambanua kile anacho kusema Lissu na yale yaliyotokea miaka mitano iliyo pita Kisha wakachukua hatua ambazo zitaweza kuishangaza hata CCM ambao wanadhani wanaweza kuhodhi utawala milele.

Ni ukweli ulio wazi tu kwamba kwa vyama vyote vya siasa watu wao watakaopanda kwenye majukwaa ya kampeni wasipojipanga vizuri Tundu atawagaragaza vibaya sana kwa hoja.

Kuna hoja dhaifu inayotolewa na makada wengi wa CCM kwamba urais hauwezi kutolewa kwa mtu kama huruma kwa sababu tu eti alipata shambulio la kupigwa risasi; huo ni udhaifu wa kujenga hoja na hilo litweza kuamsha hisia na kuwakumbusha wengi juu ya kipindi kigumu walichopitia Watanzania hapo nyuma.

La msingi kwa CCM msimbeze Lissu na kujaribu kupambana naye, bali mjipange kupambana na hoja zake ambazo kwa hakika zitakuwa kama msumari wa moto kwenye kidonda kibichi.
 
In fact CCM inatakiwa wajikite kwenye hoja. Tena hoja zilizoshiba. Ila strategy za kumtumia propaganda kama za Musiba, au vyombo vya dola kwa namna yoyote ile vitakuwa na athari mbaya kwa CCM.

Hata kitendo cha kuzuia mikutano ya siasa kwa hii miaka mitano, awali kilionekana kama kitaibeba CCM, lakini sasa ni dhahiri kuwa ulikua uamuzi mbaya. JPM alizoea kusifiwa tuuu, na wananchi walizoea kusikia upande mmoja. Bora angewaachia wapinzani wawe wanamkosoa kipindi chote hicho baadhi ya hoja zao za kukosoa aidha zingezoeleka kwa wananchi au angezifanyia kazi.

Sasa wambizani wataingia na rundo la hoja mbichiiii. Ambazo zinaweza kushangaza watu.

JPM alijisahau kama atarudi tena kuomba kura. Kuna watu wengi wameumizwa, wanasubiri watoe hukumu yao kwenye sanduku.
 
Kwa hakika Kuna mambo ni surprise aisee,nimeshangaa Sana kwamba eti kwa miaka 5 tu, tumekopa zaidi ya Trilioni 40!(Kama hii ni kweli) hii nchi tutakuwa tumerogwa haki ya Mungu, hivi kweli tunakopa pesa nyingi kiasi hicho zinakwenda wapi? Ndiyo haya madaraja, barabara, ndege na vivuko?

Kama ndiyo ina maana kila kitu tunafanya kwa kukopa? Makusanyo yetu yaliyoongezeka yanakwenda wapi?

Kama kweli haya yametokea, (kukopa zaidi ya trilioni 40 kwa miaka 5 tu) itakuwa ni UHUJUMU UCHUMI WA KIWANGO CHA JUU ZAIDI HAPA NCHINI!
 
CCM haiwezi kuwa na hoja! Miaka mitano ya mauaji, mateso, matusi, kejeli, upotezwaji watu, kufukuza wafanyakazi (ingawa hili ni kundi la hovyo kabisa), ubambikiwaji kesi, kuwatesa watu kwa kisingizio cha money laundering etc ni vitu ambavyo CCM haina njia ya kuvibadilisha.

Hata vyeti fake, bado kungelikuwa na njia mbadala ya kutoa adhabu kuliko hii aliyoifanya Jiwe!
 
Tundu Lissu amewashika pabaya.
Sisi wananchi hatuli mandege Wala madaraja ya baharini.
Vijijini hakuna maji, mnanunua mandege ya Nini badala ya kuboresha huduma za maji?
Kaombeni kura kwenye kiwanda Cha Boeing na Cha Airbus
Viongozi wako Ile siku ya Uhuru walivyoenda jijini mwanza kwaajili ya kuomba maridhiano walikodi maji ya bahari ya Hindi kwenda Mwanza?

Halafu watu tukisema Upinzani wa Tz umejaa wanafiki wa Taifa hili mnatunanga.
 
Mleta mada Ni hoja zipi unazo mpigia mapambio huyu TL ambazo haziwezi kujibiwa kirahisi?.

"Miundo mbinu ya Tanzania iliyopo imejengwa na Wajerumani" TL

"Serikali ya Magufuli haijafanya lolote jipya ilililofanya nikupeleka mbuga ya wanyama chato" TL

"Kupinga ushoga nikutengeneza mazingira ya kutengwa na umoja wa mataifa kwa kukiuka haki za binadamu" TL

"Tanzania Corona bado ipo Sana na Hali si shwali" TL.

"Hakuna sheria inayosema usiongeze Neno/Maneno katika Wimbo wa Taifa" TL

Mkuu kwa upupu huu wa TL Wachana na kujibiwa na watu wazima above 18, hata under18 Alie ishia lasaba anaweza kujibu hoja hizo dhaifu na Tena zingine atazipuuza maana hazina Maana. Sasa sijui Ni hoja gani unazosimea.
 
Umesahau msemo kuwa, raisi wa nchi hii hapatikani kwa makaratasi ya kuwekwa kwenye box?. Wewe endelea kubwabwaja tu.

Utanishawishi endapo utanambia kuwa chadamu mna katiba mpya na tume yenu ya uchaguzi siyo ile ya Dodoma. Fomu ya kugombea upewe Dodoma makao makuu ya CCM alafu ukabidhiwe Ikulu Dodoma makao makuu ya CCM? Ikulu yenyewe ndiyo imeanza kujengwa hata mjui inajengwaje ... Endeleeni kuota mchana.
 
Mleta mada Ni hoja zipi unazo mpigia mapambio huyu TL ambazo haziwezi kujibiwa kirahisi?.

"Miundo mbinu ya Tanzania iliyopo imejengwa na Wajerumani" TL

"Serikali ya Magufuli haijafanya lolote jipya ilililofanya nikupeleka mbuga ya wanyama chato" TL

"Kupinga ushoga nikutengeneza mazingira ya kutengwa na umoja wa mataifa kwa kukiuka haki za binadamu" TL

"Tanzania Corona bado ipo Sana na Hali si shwali" TL.

"Hakuna sheria inayosema usiongeze Neno/Maneno katika Wimbo wa Taifa" TL

Mkuu kwa upupu huu wa TL Wachana na kujibiwa na watu wazima above 18, hata under18 Alie ishia lasaba anaweza kujibu hoja hizo dhaifu na Tena zingine atazipuuza maana hazina Maana. Sasa sijui Ni hoja gani unazosimea.
Kwamba hakujenga Uwanja wa ndege chatle au hajapeleka Mbuga ya wanyama kwao? Lisu anasema hii kuwajulisha mabwege wanaoaminishwa kuwa anapambana na ufisadi kumbe porojo tu!
 
Umesahau msemo kuwa, raisi wa nchi hii hapatikani kwa makaratasi ya kuwekwa kwenye box?. Wewe endelea kubwabwaja tu. Utanishawishi endapo utanambia kuwa chadamu mna katiba mpya na tume yenu ya uchaguzi siyo ile ya Dodoma. Fomu ya kugombea upewe Dodoma makao makuu ya CCM alafu ukabidhiwe Ikulu Dodoma makao makuu ya CCM? Ikulu yenyewe ndiyo imeanza kujengwa hata mjui inajengwaje ... Endeleeni kuota mchana.
Wapiga kura ni wananchi wote sio ccm pekee.

Jiwe na genge lake wajiandae kisaikolojia... watafute kazi nyingine tuu
 
Mleta mada Ni hoja zipi unazo mpigia mapambio huyu TL ambazo haziwezi kujibiwa kirahisi?.

"Miundo mbinu ya Tanzania iliyopo imejengwa na Wajerumani" TL

"Serikali ya Magufuli haijafanya lolote jipya ilililofanya nikupeleka mbuga ya wanyama chato" TL

"Kupinga ushoga nikutengeneza mazingira ya kutengwa na umoja wa mataifa kwa kukiuka haki za binadamu" TL

"Tanzania Corona bado ipo Sana na Hali si shwali" TL.

"Hakuna sheria inayosema usiongeze Neno/Maneno katika Wimbo wa Taifa" TL

Mkuu kwa upupu huu wa TL Wachana na kujibiwa na watu wazima above 18, hata under18 Alie ishia lasaba anaweza kujibu hoja hizo dhaifu na Tena zingine atazipuuza maana hazina Maana. Sasa sijui Ni hoja gani unazosimea.
Ni hizo tu ulizozisikia kutoka kwa Tundu Lissu? Ngoja nikukumbushe...

1. Kwa miaka 5 tu serikali ya awamu ya tano imekopa zaidi ya Trilioni 40, (kama Ni kweli zimekwenda wapi?) Hoja hii inapaswa kujibiwa kwa sababu tumeambiwa mara zote kuwa makusanyo yameongezeka na miradi yetu inatumia fedha za ndani

2. Ujenzi wa Hydroelectric power kule rufiji sio jambo jipya, (japo ni zuri) kwani kuna wengine walishajenga mabwawa kama hayo na yanafanya kazi mfano, Kidatu, Mtera n.k

3. Ujenzi wa reli si Jambo jipya (japo ni zuri), kwani reli zilijengwa na watangulizi wengine, mf.TAZARA NA RELI YA KATI na waliondoka baada ya muda wao kuisha, kwa hiyo hoja kwamba yeye aongezewe muda kwa sababu hizo ni dhaifu sana

4. Kukanyagwa kwa sheria mbali mbali, ikiwemo kuwadhulumu wafanyakazi haki zao za kimsingi kama kuwaongezea mishahara, kuwapandisha madaraja (vyeo) uhamisho, kusinyaa kwa ajira n.k haya yote ameyakanyaga bila huruma,kinyume Cha sheria!

Hayo ni baadhi tu ya mengine mengi ambayo Tundu Lissu ameyazungumzia na yanapaswa kujibiwa kwa hoja, unaweza kutusaidia kujibu kwa niaba ya chama chako?
 
Kwa hakika Kuna mambo ni surprise aisee,nimeshangaa Sana kwamba eti kwa miaka 5 tu, tumekopa zaidi ya Trilioni 40!(Kama hii ni kweli) hii nchi tutakuwa tumerogwa haki ya Mungu, hivi kweli tunakopa pesa nyingi kiasi hicho zinakwenda wapi? Ndiyo haya madaraja, barabara, ndege na vivuko?

Kama ndiyo ina maana kila kitu tunafanya kwa kukopa? Makusanyo yetu yaliyoongezeka yanakwenda wapi?

Kama kweli haya yametokea, (kukopa zaidi ya trilioni 40 kwa miaka 5 tu) itakuwa ni UHUJUMU UCHUMI WA KIWANGO CHA JUU ZAIDI HAPA NCHINI!
Hili moja tu la 40.5 trillion majibu hana ya value for money......
 
CCM haiwezi kuwa na hoja! Miaka mitano ya mauaji, mateso, matusi, kejeli, upotezwaji watu, kufukuza wafanyakazi (ingawa hili ni kundi la hovyo kabisa), ubambikiwaji kesi, kuwatesa watu kwa kisingizio cha money laundering etc ni vitu ambavyo CCM haina njia ya kuvibadilisha.
Hata vyeti fake, bado kungelikuwa na njia mbadala ya kutoa adhabu kuliko hii aliyoifanya Jiwe!
Watazitoa wapi hizo hoja sasa hao CCM???
 
Back
Top Bottom