CCM tupo katika mwanguko mkubwa

CCM tupo katika mwanguko mkubwa

w
Embu weka hapa ushaidi kama kweli wewe ni mwana ccm . Hizi ni propaganda za kitoto . Hata mimi naweza kujisemea ni mwana TADEA kwa manufaa fulani wakati sio kweli mwana TADEA.
Hii ndiyo shida ya kilichokuwa chama changu toka TANU.
Wengi tumejiengua kutokana na kushindwa kwa juhudi zetu za kukikosoa chama tukiwa ndani kwani kila tulipofanya hivyo tuliishia kuitwa "Wasaliti" au "Wamenunuliwa".
Pole pole chama kinawapoteza wanachama wenye moyo wa dhati na kujaza mamluki toka upinzani.
Binafsi nilihamia upinzani baada ya kuchukizwa na tabia mbovu za viongozi walioonekana dhahiri kuzidiwa hoja na wapinzani haswa CHADEMA.
Kwa hakika watanzania tumechoka na muda unaopotezwa na wabunge na mawaziri akiwemo Waziri Mkuu kuhangaika na kupeleka mashambulizi kambi ya upinzani na kwa njia hiyo kuupaisha umaarufu wao!
Najua wapo watakaobeza hoja hii lakini mambo yakiendelea hivi nina mashaka kama chama changu cha kale kitamudu hata kuunda kambi ya upinzani.
Mi natabiri mambo yakiendelea hivi itakuwa vigumu kupata hata wabunge 20 katika bunge lijalo.
Hivi ni kipi mtakachowadanganya wananchi mkafanikiwa? Matumizi ya Polisi kukisaidia chama kila mmoja anayaona, hongo za kununua mashabiki wa kuhudhuria mikutano yenu zinapokelewa hadi na wapinzani, utekaji nyara na kuteswa kwa walio kinyume chenu kuko wazi mno na karibu kila mtanzania wakiwemo makada wanafahamu ni nani anayehusika! Wakati nyinyi mnahangaika kuudanganya umma eti ni CHADEMA mitaani kote watu wanawasema ni Usalama wa
Taifa kwa maelekezo ya CCM!
Sijui kama yupo hata kingozi mmoja wa CCM anayesoma kijitabu cha Hayati Baba wa Taifa - mwasisi wa chama chenu cha "Tujisaihishe".
Muda ukifika ugonjwa utajitokeza hadharani na kuwaumbua kweupee!
 
Huyo jamaa aitwae 'Bungeni' ni mtu aliyetoroka toka kule CHIT-CHAT wanakofungiwa na PAW siku zote Wana-JF ambao bado wapo katika mcha kato wa kupewa uwezo na staha wa lugha kushiriki vema katika jukwaa la siasa.

Chonde mvumilie kidogo atarudishwa kule kwenye ukurasa wao baadaye kidogo.

Yaani we jamaa sikuoendi na unaudhi ile mbaya............ningekuwa mwanao ningeona aibu kukuita baba au mama. Ni aibu kwa mzazi mwenye akili za hivi kizazi hiki na muda huu.
 
ati umesema wewe ni mwanachama mwandamizi????
kadi yako namba ngapi vile???????????
 
mkuu umenena ukweli mtupu.maneno yako yamenigusa sana ingawa mimi ni mfuasi wa cuf.cjawahi kuona chama tawala kikijenga chuki kwa wananchi kama sasa.acheni wajichimbie kaburi lao wenyewe.
 
we mburula unadhani bado kuna mtu anapenda kujionesha kuwa yeye ni ssm wale wanaotumia makalio kufikiri na kichwa kukaa ndiyo wanaweza kujitapa kuwa wao ni ssm zaidi ya hapo uongo! stuka utajikuta upo mwenyewe maana kama ungekuwa na aikil kaagalie hapa jamii ambao tupo watu wa digital na wasomi
Embu weka hapa ushaidi kama kweli wewe ni mwana ccm . Hizi ni propaganda za kitoto . Hata mimi naweza kujisemea ni mwana TADEA kwa manufaa fulani wakati sio kweli mwana TADEA.
 
Kamuulize mwigulu nchemba
madelu ndio atakwambia umakini wa ccm sio ukurupuke na njaa zako za
kulipwa kwa thred na post uje uwahadae watu humu.mleta mada shame on
you!

shame on you too! unamtegemea mwigulu kujua umakini wa ccm, kweli wewe mbulula na taburalasa! are u conscious au unaropoka tu?
 
Kweli nimeamini JamiiForums vilaza ni wengi, mtu kakurupuka huko anadai yeye ni CCM bila ya uthibitisho wowote na watu wanakubali.

CCM kamwe haiwezi kuwa na mwanachama mchumia tumbo kama huyu mleta thread.
 
Wewe wa wapi?...

unamshangaa bungeni wakati hajui kama wanaanguka pamoja na kupeana ushauri wa ndani kwa ndani.

ile kansa ya CCM aliyoisema Mwl Nyerere enzi ile ndio ina-manifest, na kama tujuavyo kansa kwenye hatua za mwisho haitibiki, huduma pekee ni kupunguza maumivu tu...huyu bungeni anapunguza maumivu tu, ila kansa ndio hiyo tena
 
shame on you too! unamtegemea mwigulu kujua umakini wa ccm, kweli wewe mbulula na taburalasa! are u conscious au unaropoka tu?

Wewe ndiyo wa kuulizwa kama akili yako ni timamu. Ni bora mtu anayemwamini mtu anayemwona kuliko wewe unayemwamini huyu mwanzisha thread aliyejificha nyuma ya keyboard. Nikikwambia mimi ni baba yako mzazi utakubali?
 
upuuzi mtupu,ccm iko imara kuliko wakati wa mchonga. Muanzisha uzi ni kijana wa slaa,kitengo cha tindikali

kwa uelewa wangu mdogo kwa kila anaiyeiunga mkono ccm atakuwa amejazwa kinyesi kichwani
 
Kamuulize mwigulu nchemba madelu ndio atakwambia umakini wa ccm sio ukurupuke na njaa zako za kulipwa kwa thred na post uje uwahadae watu humu.mleta mada shame on you!

Hapo kwenye nyekundu umeonesha unaipenda ya Mwigulu, ya Serukamba vip au ni baabu kubwa na unaiogopa!!!
 
Ccm kwa sasa ndio ipo imara kuliko wakati mwingine wowote ule..mtahangaika sana
Una akili au matope? Nipe bei yako nikununue maana njaa yako imehamia kichwan. kikombe hiki kiniepuke kweli kuna vijana hawaihurumii hii nchi
 
Ccm haina mda mrefu itaanza kutumia maneno ya mmiliki wa twanga pepeta"kuchanika kwa janvi sio mwisho wa maongezi"kuja kutahamki bendi ishakimbiwa na waimbaji wote
 
Waambie hao,maana wamesahau kama wanatakiwa kuihoji serikali,wanaamua kuwadhibiti wapinzani,wanaiacha serikali inapeta tu.Hapo kwa mawaziri hasa wale wavivu wanajisikia poaaaa,maana si wanajua kazi ya wa bunge sasa ni kuwa wajibu wapinzani?
 
Back
Top Bottom