Umeeleka vyema mwanatanzania,hapa tunazungumzia Tanzania,yeyote mwenye uchungu na nchi hii huweka maslahi yake pembeni na kuangalia mustakabali wa taifa letu.
Umeeleweka kwa sababu ni dhahiri isiyo na shaka kuwa taifa la Tanzania lipo ktk ombwe kubwa la kiuongozi.Leo hii nchi inaharibika na hakuna wa kumvesha paka kengele.
Leo hii wanainchi wametambua umuhimu wa kuunganisha pamoja nguvu zao na kupigania uhuru wa pili wa Taifa hili tajiri kwa raslimali ila ni masikini wa kutupwa hapa duniani.
Wanawanchi hii wamebaini janja ya watawala na wasomi uchwara wanaopenda vitu na vyeo badala ya kutumia elimu zao kuiokoa nchi yetu,badala yake wanajitajilisha na kujilimbikizia mali wao na watoto wao kana kwamba taifa hili ni mali yao.
Daima tutakukumbuka kambarage jemedali wetu makini na baba wa taifa,wapo tulioupokea usia wako wa kuweka mbele maslahi ya taifa,tunakukumbuka kwa kuongoza kwa mfano hukujilimbikizia mali,hukujaza vilaza,mashemeji,makuwadi ikulu,Hukupendelea wapambe wako,watoto wako wala marafiki wa watoto wako na kuwapa nyadhifa serikalini ilhali uwezo hawana.hukuigeuza nchi kuwa mali ya kundi la wachache wasiozidi hata asilimia 10% wanaonufaika na kuzitumia mali za nchi wanavyotaka.
Mwalimu yote uliyoyapigania na kuyatenda tumeyaona na watawala wa leo wameshindwa kuvaa viatu vyako,daima utakumbukwa na kuenziwa.
Ni kweli anguko la CCM ni dhahiri na halina kificho,kujilidhisha kuwa kuna mwenye uwezo wa kuzuia anguko hili ni kujidanganya kwani maumivu vijijini yamekithili na waswahili hunena ukiona tabu na mateso yanazidi ujue ukombozi uko karibu,wanawanchi wanausubiri ukombozi kwa hamu kubwa.