CCM Taifa Ikemee Vijana wake, Vinginevyo...

CCM Taifa Ikemee Vijana wake, Vinginevyo...

Nafikiri kuna mengine mengi tu UVCCM waliyotamka kwa faida ya wananchi....lakini eehe JF akisemwa vibaya Dr Slaa basi watu hawaoni tena.

May be in this post you will get time to console each other..lakini binafsi sitomuunga mkono Slaa wala Kikwete kama mtu anayeweza kuongoza taifa hili. Ushabiki wa vyama vya siasa sio mtazamo wangu

Naomba unifumbue macho; lipi lililotamkwa na hao vijana ambalo lina faida kwa wananchi? Naamini nimelisoma hilo tamko vizuri.
 
... it won't be pretty! Yatakapoanza kuporomoshwa matusi na mambo mengine dhidi ya viongozi wa CCM wa kitaifa isije kuoneekana "ni kuvunja heshima, kuchochea, matumizi mabaya ya vyombo vya habari" na upuuzi wa kawaida tuliouzoea.

Maana naamini walichofanya UVCCM kimewapa watu wengine haki ya kuwatukana na kuwasema viongozi wa taifa wa CCM katika masuala yao binafsi. That will be a tragedy.

Ukiniuliza mimi CCM (T) hawana zaidi ya masaa ishirini na nne ya kutoa kauli ya kinidhamu dhidi ya vijana wao.

Looks like the section on Dr. Slaa et al. was deliberately insirted to bring them on defencive against aginst different agenda.

Kama Chadema wasipouona huu mtego, ukawafyatukia basi itakuwa ligi ya matusi na kesi mahakamani na hizi agenda za kitaifa hazitapata kipaumbele tena.
 
I'm very serious; kuna msemo wa kiingereza kuwa "all is fair in love and war".. na UVCCM wamethibitisha hilo. Tatizo ni kuwa kikaango kitakapogeuzwa kwa upande mwingine patakuwa pachungu kweli.
ucjaribu kuzipotosha bongo za watanzania.... kikaango kipi ambacho bado hakijageuzwa. CDM imeshageuza kikaango chake pande zote na mara nyingi sana kiasi ambacho kikaango chenyewe kimepoteza ile rangi yake halisi.
kwetu sisi tunaotazama mambo bila kupofushwa na ushabiki maandazi, wala hatutilii maanani misemo na vitisho vyenu.
DR SLAA ni kansa ya taifa kama walivyo akina ROSTAM, LOWASA N.K.
TOFAUTI NI MOJA TU KWAMBA HATA CHAMA ALICHOTOKA SLAA NACHO NI KANSA YA TAIFA, ila CCM inaweza ikawachinja akina RA,na EL na chama kikabaki na sifa zile za tangu kipindi kileeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Inashangaza kuona hawa vijeba (UVCCM) kutoa matamko yanayofanana na mtu anayeharisha choo cha stendi kuomba kopo la maji. Fikiria
1. Wanadai baraza la mawaziri linagongana, chanzo Dowans. They move futher to suggest kuwa sitta na mwakyembe wapigwe chini (by implication.
2. Pili wanadai Dowans isilipwe vinginevyo watahitisha maandamano. My question, ni kitu gani wanatetea wakati hao hao wanaotetea Dowans isilipwe na Serikali ya kifisadi ya kikwete wanawapinga. Hivi hawa vijana wana akili kweli.
3. Wanashindwa kutoa tamko dhi ya EPA, IPTL, DEEP GREEN, Kiwira, RADA, Ndege ya rais, ATCL, mfumuko wa bei, uchakachuaji wa kura, mauaji ya raia yanayofanywa na kikwete under what he calls 'police' mauaji ya arusha, matamko ya kishetwani ya baadhi ya watu wachache wanojiita "Jopo la mashehe', nk, mazimwi yanayotishia ustawi wa jamii yetu.
My take
James Ole Millya, Beno Malisa, Kawawa; hawa ni CRAP who are synergized by Lowasa na rafiki Zake J.K na RA. Ukiangalia kwa undani utagundua hili kundi la wahuni limetumwa na hawa jamaa na kupewa hadidu za rejea. Refer maneno yao "Tunaitaka Serikali kuwataja rasmi wamiliki wa Richmond ili ijulikane kipi ni kipi na hoja hii irudi bungeni ili Watanzania wajue nani aliifikisha Serikali hapa ilipo, kama ni Tume ya Mwakyembe (Dk. Harrison-aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Bunge iliyoundwa kuchunguza sakata hilo wakati ule, sasa Naibu Waziri wa Miundombinu) ililidanganya taifa, iwajibike na kama ni serikali basi imtaje mmiliki, ili yeye alipe pesa hizo na si wananchi," alisema Millya. Millya alisema wanayotaarifa kuwa sakata hilo lilianzia bungeni na hatimaye Tume (ya Mwakyembe) ilitoa ripoti kuwa Richmond ni kampuni hewa na wamiliki wake halali hawajulikani" (Source; Habari leo, 21,Jan 2011). wanashindwa kufahamu kuw ahii kamati ilikuwa ya bunga na si si mwakyembe kama wanavyotaka ifike kwetu. Mimi nadhani hii hoja ikifika bungeni kikwete antangoka madarakani. Mwakyembe atatumia hii fusra kusema na kutaja yake waliyosema wametunza ili kuinusuru serikali isianguke; ambayo obviously ni kuhusika kwa jk kwenye sakata hili la kifisadi.

Vijana hawa hawana cha kufanya. Hoja ilikuwa ni kumtukana Dr Slaa na siyo hayo mengine maana wanaijua serikali yao fika. Wametumia page moja na robo kumzungumzia Slaa pekee. hwa ni kina bora liende.
 
Kama mtu ambaye nimemuunga mkono Dr. Slaa na kuamini kuwa ni mtu aliyepaswa na anayestahili kupewa nafasi ya kuliongoza taifa nimeshtushwa na kusikitisha na tamko la UVCCM hususan mashambulizi yao ya mtu - ad hominem thidi ya Dr. Slaa. Ninawasihi viongozi wa CCM Taifa kukemea na kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya kundi hilo la viongozi wa vijana.

Kutokuchukua hatua mara moja na kukaa kimya binafsi naamini iwakuwa ni halali kuamini kuwa uongozi wa taifa wa CCM umetoa baraka zake. Which brings me to my observation: it won't be pretty! Yatakapoanza kuporomoshwa matusi na mambo mengine dhidi ya viongozi wa CCM wa kitaifa isije kuoneekana "ni kuvunja heshima, kuchochea, matumizi mabaya ya vyombo vya habari" na upuuzi wa kawaida tuliouzoea.

Maana naamini walichofanya UVCCM kimewapa watu wengine haki ya kuwatukana na kuwasema viongozi wa taifa wa CCM katika masuala yao binafsi. That will be a tragedy.

Ukiniuliza mimi CCM (T) hawana zaidi ya masaa ishirini na nne ya kutoa kauli ya kinidhamu dhidi ya vijana wao.

MM, Hata mimi nimesikitishwa sana. Lugha ya hawa UVCCM sawa na ya yule mzushi anayeitwa Salve Rweyemam. Mambo binafsi ya Dr Slaa yameingiaje katika tamko lao linaloonekana kuwa zuri, ukiliangalia haraka haraka. Kesi za Dr Slaa (ya kuwa na mchumba aliyewahi kuolewa na ile ya yaliyojiri Arusha) ziko mahakamani. Na hivyo tamko hili na katika kipengele hicho halikuwa la lazima.
 
ucjaribu kuzipotosha bongo za watanzania.... kikaango kipi ambacho bado hakijageuzwa. CDM imeshageuza kikaango chake pande zote na mara nyingi sana kiasi ambacho kikaango chenyewe kimepoteza ile rangi yake halisi.
kwetu sisi tunaotazama mambo bila kupofushwa na ushabiki maandazi, wala hatutilii maanani misemo na vitisho vyenu.
DR SLAA ni kansa ya taifa kama walivyo akina ROSTAM, LOWASA N.K.
TOFAUTI NI MOJA TU KWAMBA HATA CHAMA ALICHOTOKA SLAA NACHO NI KANSA YA TAIFA, ila CCM inaweza ikawachinja akina RA,na EL na chama kikabaki na sifa zile za tangu kipindi kileeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Eti CCM inaweza ikafanya nini? Wana-ubavu. Makamba pekee amewashinda itakuwa RA na EL.
 
UVCCM hawajakemea mafisadi bali wamekemea Mwakyembe na Sita kwa nini walisababisha mkataba kuvunjwa kwa ripoti ya uongo bungeni. Subiri utaona kitakachotokea.
 
UVCCM wako sahihi kabisa! Kwani hawaja msingizia jambo lolote Dr wa Phd ya ukweli nashangaa mapovu yanvyo watoka midomoni humu JF! Imewauma sana! Hongera UVCCM kwa Tamko lenu! Alta Continuaaa!
Katika matamko yao kuna kitu ambacho watu hawakifahamu? mambo ya miaka mitatu, miwili iliyopita ndio wanatoa tamko leo? Akili zao ni nzito, kufikiri kitu kwa miaka mitatu? Kitu ambacho watu wengine waliisha kifikiri na kukifanyia kazi, tamko la richmond walitakiwa walitoe pale Lowasa alipojiuzuru. Eti hawa akina Beno Malisa ndio viongozi wa taifa hili baada ya akina JK, What a disaster!!
 
Mi naona yote waliyoyaongea ni upuuzi mtupu.......wametumwa.
1) wanaposema Dowans wasilipwe, the wanasema wanakemea mawaziri kutoa conflicting statements, wakiwaongelea specifically Mwakembe na Sitta (wote tunajua hawa wawili ni mwiba kwa RA na EL) wanataka kusema wao wana uhuru zaidi wa kusema Dowans isilipwe kuliko hawa wawili?

2) Wanaposema CCM ivunje board ya mikopo wakati waziri wa elimu ameshasema mfumo unaotumika kwenye board ya mikopo haufai na wataubadilisha.......wanmaanisha nini? wanapotoa mifano petty kama wa Mkwawa, kwamba wanafunzi wamegoma siku moja the following day wakapata fedha zao, wanafikiri hilo ni tatizo la kimfumo?.....uwajibikaji sifuri wa watendaji wa serikali na kupenda kujinufaisha na fedha za umma.

3) Matusi ya nguoni kwa Dr. Slaa ni wendawazimu tu wasiojua wasemalo wala wakitakacho. Hatuhitaji kujadili makelele ya watoto wakishabikia kombolela.
 
kweli ile bangi waliyovuta UWT sasa UVCCM wameanza kuivuta....

ni bangi ya mwakaleli milimani imechanganywa na kinyesi cha kitimoto!!! lazima ulipuke!

je si ni bora anayepigania haki ya msingi ya kuwa na mwenzi wake kuliko mwizi? je tuanze kuzungumzia maghorofa ya kina rz1 yanayoinuka kama uyoga mikoani? je tuzungumzie malori 60 ya huyo huyo yaliyo iringa kwa kiingizio cha asas dairies? je tyuzungumzie kupewa binti na kila familia ya mafisadi? je tuzungumzie jinsi KIKWETE anatambulika kama ni mwekezaji mkubwa COMORO?
 
ucjaribu kuzipotosha bongo za watanzania.... kikaango kipi ambacho bado hakijageuzwa. CDM imeshageuza kikaango chake pande zote na mara nyingi sana kiasi ambacho kikaango chenyewe kimepoteza ile rangi yake halisi.
kwetu sisi tunaotazama mambo bila kupofushwa na ushabiki maandazi, wala hatutilii maanani misemo na vitisho vyenu.
DR SLAA ni kansa ya taifa kama walivyo akina ROSTAM, LOWASA N.K.
TOFAUTI NI MOJA TU KWAMBA HATA CHAMA ALICHOTOKA SLAA NACHO NI KANSA YA TAIFA, ila CCM inaweza ikawachinja akina RA,na EL na chama kikabaki na sifa zile za tangu kipindi kileeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Na wewe ni Kansa ya JF... Dr Slaa ni Rais wa waTanzania mioyoni mwetu, rais wa ukweli tuliyemchagua kwa kura milioni 6 mkachakachua while Jk mkwere ni rais wa Tanzania kupitia majeshi na sio mioyoni mwetu na hata yeye anajua kuwa hatumtaki. Ndio maana anaishi kama digidigi kuchimbia magogoni halafu anaibuka kufungua shule ya msingi, kazi ya katibu tarafa anaifanya rais wa nchi???
 
Sio Bure hawa vijana wametumwa walikua wapi siku zote,ama kweli siku zote mbwa huanza kumfokea mmiliki wake, na ukiona mbwa juu ya mti ujue hajapanda mwenywewe kawekwa
 
Mzee mwanakijiji hivi hujui kuwa kabla ya tamko ni lazima viongozi wa ccm taifa kupitia hilo tamko? pia ujue kuwa ktk kamati ya utekelezaji uvccm taifa makamba na raisi ni wajumbe pia,hivyo ktk lile tamko kunabaraka zote za uongozi wa juu wa ccm,hii ni kutokana na kanuni ya uvccm inavyosema

so kila jambo lifanywalo na uvccm ni lazima kuwe na mkono wa ccm kwani ndiye mlazi wa jumuia zote
mapinduziiiiiii daimaaaaa:frusty:
 
Sio Bure hawa vijana wametumwa walikua wapi siku zote,ama kweli siku zote mbwa huanza kumfokea mmiliki wake, na ukiona mbwa juu ya mti ujue hajapanda mwenywewe kawekwa


ha ha ha nasikitika ma thinker wa jf kutumia muda mwingi kuwajadili UVCCM , uliona mtu anakufa bila kutapatapa, usisumbuke kuzuia kivuli cha mti wewe kata mti wenyewe awa vijana sidhani kama wana jipya la kuweza kuwajadili
 
TAMKO LAO LILILENGA:
(1) Kumtukana mwana mapinduzi Dr. Slar binafsi na kuhadaa wa tz kuwa apuuzwe kwa mipango ya maandamano ya amani ya ukombozi popote tz
(2) Kusisitiza mawazo ya makamba, chitanda na polisi juu ya yaliyojiri arusha ili kuonesha umma kuwa CDM na DR. Slar ndio chanzo cha mauaji-katika lengo la kujionesha mbele ya watu kuwa CCM ni watakatifu
(3) Kuendeleza propoganda za udini ambazo zimekuwa zikitumika kama mtaji wao wa kutugawa watanzania ili waweze kutawala vema na kuwanyonya watanzania
(4) Kuhusu DIMONi, tamko linalenga KUZIBA midomo wapambanaji 6 na mwakyembe katika kusisitiza yale yale ya CHIKAWE ili wasiendelee kuiumbua serikali maana wanajua ndo wenye facts za jambo husika. Kimsingi wanakubaliana na kuilipwa DOWANS (swala la kwamba watafutwe Richmond ili walipe kwa niaba ya serikali/tanesco ni danganya toto-katika kujifanya nao wanauchungu na nchi kulipa. Maana kama wangekuwa ni wapambanaji wa kweli kwa nini kuwazodoa watu km 6 na mwakyembe ambao wanaujua ukweli wa uhewa wa DOWANS na RICHMOND?

*MATUSI YA NGUONI KWA DR. SLAR YATAWARUDIA SI MUDA MREFU NA WAO WATAKUWA WA KWANZA KULALAMA

VIJANA SI WA CCM WALIOWENGI KWA SASA, BALI VIJANA WANAUKOMBOZI NDO WENGI, HIVYO TAMKO LAO NI KUJILIWAZA WENYEWE.
 
Hao ndio vijana wa ccm ambao wameelimika tayari kushika hatamu za uongozi wa taifa,
Inatisha sana, Kama hawatakemewa basi mlango wa matusi kwa viongozi wa ccm utakuwa umefunguliwa.

Hawa vijana hata wakikemewa hawawezi badilika. Washa lewa madaraka ya wazee wao. Napes and Riz1 design. Kwa jinsi CCM inavyoiendesha nchi hii na jinsi vijana wa CCM walivyoweza kutuonyesha ngozi yao waziwazi kuwa wao si kondoo badi ni mbweha, wametusaidia kutuhakikishia waTZ kuwa nchi yetu ina serious leadership crisis CCM, now and later. Now, I mean the current government and later the UVCCM, the so called future leaders.
 
MM
I wish hao CCM taifa wangekuwa na huo muono wa kujua kama vijana wao wamemkosea adabu Dr Slaa. Ukweli ni kwamba hajui na wala hawatajua kama yale ni matusi. Ukikumbuka ile barua ya Salva haina tofauti kubwa na hili tamko la UVCCM. Kwangu mimi UVCCM wameendeleza pale Ikulu ilipoishia. Ulishasikia mkuu wa ikulu kamuomba radhi Dr Slaa kwa kile Salva alivyoandika??? Kwa hili tusitegemee kama kutakuwa na tofauti.
Bahati nzuri asilimia kubwa ya hao UVCCM nawafahamu vizuri ki matendo na tabia, hakuna viongozi/watu wenye japo chembe ya busara pale, ni ubabaishaji tu.
Ki maadili tu wala hawakupaswa kumrukia mzee Slaa kwa matusi/kejeli/mipasho ya namna ile. Pale UVCCM nani ambaye anaweza sema Dr Slaa si kama mzazi wake?? Ni utovu wa nidhamu na upunguwani ndo ulichofanya waingilie hata mambo yasiyowahusu. UVCCM na Dr Slaa wapi na wapi??
Lakini hii ndio CCM ya sasa na Ijayo...... Mwenye akili anaweza jua nini la kufanya.
 
UVCCM hawajakemea mafisadi bali wamekemea Mwakyembe na Sita kwa nini walisababisha mkataba kuvunjwa kwa ripoti ya uongo bungeni. Subiri utaona kitakachotokea.

Tuko katika mstari mmoja wa fikra. Kuna kitu fishy mahali...
 
Na je mtafanya nini yule mpumbavu kibaraka wa Wizara ya Nishati na Madini aliyetoa taarifa finyu potofu ya udanganyifu wa wamiliki wa Dowans siku chache zilopita? Ngeleja alipaswa ajiuzulu kwani hata chama chake hakiamini ripoti alotoa....na wamesema watajiwe wamiliki wa Richmond (na Dowans).

Ni uozo unaondelea katika utawala....mwenye akili na maadili kidogo angechepuka akimbie toka kundi la wezi na wahalifu liitwalo baraza la mawaziri (sic)
 
Back
Top Bottom