Wale wote wachafu wamekuwa wakitimiliwa ndani ya chama tangia kuanzishwa kwake.
Hebu taja wachache tu kati ya hao waliotimuliwa na nyadhifa zao katika chama.
CCM sio chama cha mtu mmoja ama genge la watu fulani najua unalijua hilo, na imekuwa ikiwaondoa wale wote ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa wakienda kinyume na katiba ya chama, kupitia vikao vyake vya kawaida na dharura katika ngazi zinazohusika.
Je unayo habari kwamba usemi, "CCM ina wenyewe" ilianzishwa lini, na nani na kwa malengo gani ?
CCM ina "untouchables" ambao serikali yenyewe ya CCM imesema wazi kuwa wakiguswa nchi itayumba. Je, wewe Kibunango umo miongoni mwa hao - sidhani kwa sababu you are so misinformed.
Na wengine kwa kushindwa kufuata katiba ya chama hicho wamekuwa wakijiengua wenyewe kabla ya kutimuliwa.
Watiifu wa CCM kamwe hawawezi kujiengua wala kutimuliwa - huo ubavu utapatikana wapi. Adui mkubwa wa CCM kwa wakati huu ni yule anayejaribu kukisafisha na huyu wana CCM hawasiti kumwona dui kwa kutaka kutia mkate wao mchanga - wakale wapi ?
Kauli ya usafi ama uchafu ni kauli ambayo tupo nayo katika miaka hii, CCM kama chama inaenda sambamba na kauli hiyo kwa kuendelea kuwaondoa wale wote wanabainika kuwa ni wachafu. Taratibu za kuwaondoa wachafu hao ni zilezile ambazo zimekuwa zikitumika tokea kuanzishwa kwa chama hicho.
Ama wewe hujui kinachotokea ndani ya CCM au unaamua kwa sababu zako kusema uwongo. Tabia na taratibu iliyojengeka ndani ya CCM siku zote ni ya kulindana na hili hata mtoto mdogo analifahamu. Kwa hivi sasa KAGODA ni mfano hai wa kulindana ndani ya CCM kunavyozidi kukomazwa - je, ni kweli hata hili hulioni ?
Uzuri wa miaka hii ni kuwa wale wachafu ambao hutimuliwa CCM hupata sehemu za kwenda na mazagazaga yao ya uchafu.
Wataje hao. Ninavyojua wachafu wanaoondoka CCM hukosa pa kutua na mwishowe hulazimika kurudi huko huko na kupokelewa kwa vifijo na nderemo. Huko nje baada ya muda hugundua kuwa hakuna mabwawa ya Richmond, Kiwira, Kagoda, n.k - sasa wataogelea wapi ?
Na huko hukutana na wachafu wenzao na kuendeleza tabia zao za uchafu uchafu, huku wakiota siku moja wataongoza nchi na mauchafu yao.
Huko nje hukutana na wazalendo wenye nia ya kweli ya kukomboa nchi na inabidi ama wajioshe wawe wasafi au warudi CCM. Mifano iko mingi tu lakini ukweli unabaki pale pale kuwa CCM wanaongoza nchi kwa kuwa wako madarakani kwa uchafu wao nambari wani - rushwa.
Nyumba safi inaweza kukaliwa na wachafu vilevile, hata hivyo kutokana na sifa ya uchafu kuwa unuka ni rahisi kwa wachafu kujulikana katika nyumba safi. Na pua za wasafi wengi wa CCM siku zote zimekuwa zikinusa wale wote ambao awali walikuwa wasafi, lakini wakaanza kuwa wachafu. Uzuri utimuliwa mapema kabla ya kueneza tabia zao mbaya za uchafu.
Kweli kabisa ni rahisi kwa wachafu kujulikana kwenye nyumba safi kuliko msafi kujulikana ndani ya nyumba chafu. Pua za wasafi ndani ya CCM kama wapo zimeshindwa kunusa wachafu kwa sababu wote tayari wanaogelea kwenye uchafu na kupakana uchafu. Sasa hapa wa kunyosha kidole atapatikana wapi !!
Kimsingi Wachafu bado kwisha ndani ya CCM, lakini hii haina maana kama CCM ni chafu.
Ahaa, sasa unaanza kupata ka mwanga ila uchafu wenyewe umeshaligharimu taifa matrilioni ya shilingi na CCM haina tena nia wala uwezo wa kujisafisha. Kati ya uchafu na usafi wamechagua uchafu na kansa sasa imeenea mwili mzima na hakuna tena tiba.
Baba wa nyumba ya CCM ameshasema bayana kuwa mchafu yoyote atakayebainika ndani ya nyumba ataondolewa na kupelekwa kunako husika na usafishaji wa wachafu.
Baba mwenyewe alikubali kutawazwa kwenye nyumba yenye uchafu na hivyo kuogelea humo humo - sasa hiyo jeuri ataitoa wapi ? Sana sana atabaki anawashangaa wanaopigia kelele uchafu wa nyumba anamoishi yeye.
Kauli za Baba huyu zimeshaanza kuonekana licha ya maneno ya kejeli toka katika katika nyumba za Wachafu wengi ambao kutwa wamekuwa wakitamani Nyumba safi ya CCM iwe chafu kama zao.
Kwa nini kelele zitoke nje ya hilo jumba tu na zisitoke humo ndani kama kweli nyumba bado ina wasafi. Unasema nyumba ya CCM ni safi halafu unakubali kuwa bado kuna wachafu humo ndani yake - kweli hii inaingia akilini.
Kibunango which makes more sense -
wachafu kutoka kwenye usafi au wasafi kutoka kwenye uchafu ?