Ole
JF-Expert Member
- Dec 16, 2006
- 2,157
- 975
Chama Cha Mapinduzi kwa mara nyingine kinawahadaa walipa kodi kwa kusema kwamba viongozi Mafisadi waliojikita ndani ya chama hicho na kukifadhili wataachia ngazi walizonazo na kukiacha chama hicho kuwa safi. Je, huu ndio utawala wa sheria ambao chama hiki kinahubiri?
Ikumbukwe kwamba kashfa ambazo RA, Chenge pamoja na EL zinawakabili ni kubwa sana za kuhujumu uchumi wa nchi. Sheria za kuwaadhibu zipo, Je ni kwa nini hazichukuliwi ili tufahamu zipi ni mbivu? Je, JK anaogopa kwamba na yeye ataingia kwenye huo mtego? Inawezekana vipi watu wakwapue pesa za walipa kodi na wasiwe na adhabu yoyote? Je tumefika mahali ambapo sheria za nchi zinatembezwa mfukoni kama pesa? Inawezekana vipi JK akatembea kifua mbele wakati anashindwa kulinda katiba ambayo aliapa kwamba atailinda?
RA, EL, Chenge na wafuasi wao lazima wachukuliwe hatua zinazostahili bila kuwaonea aibu kwa sababu tukiwaonea aibu hawa itabidi tuwaonee aibu wanaoiba kuku pamoja na heleni.
Ikumbukwe kwamba kashfa ambazo RA, Chenge pamoja na EL zinawakabili ni kubwa sana za kuhujumu uchumi wa nchi. Sheria za kuwaadhibu zipo, Je ni kwa nini hazichukuliwi ili tufahamu zipi ni mbivu? Je, JK anaogopa kwamba na yeye ataingia kwenye huo mtego? Inawezekana vipi watu wakwapue pesa za walipa kodi na wasiwe na adhabu yoyote? Je tumefika mahali ambapo sheria za nchi zinatembezwa mfukoni kama pesa? Inawezekana vipi JK akatembea kifua mbele wakati anashindwa kulinda katiba ambayo aliapa kwamba atailinda?
RA, EL, Chenge na wafuasi wao lazima wachukuliwe hatua zinazostahili bila kuwaonea aibu kwa sababu tukiwaonea aibu hawa itabidi tuwaonee aibu wanaoiba kuku pamoja na heleni.