CCM na Mategemeo yao JKT

Ilikuwa zamani hata passport hupati kama sio mwana CCM, lakini kwa sasa ni ngumu sana
 
si kweli, sasa hivi demokrasia imetapakaa kila mahali.. hizo ni dhana potofu za kuwagawa watu kichama ref: uchaguzi wa 2010 cdm iliongoza mitaa ya masaki, makongo ambayo ni ngome ya jeshi tena kwa gap la mamia ya kura, kambi nyingine karibu zote tz cdm ilipeta tofauti na watu walivyofikiri mwanzo kuwa uko ndio uchakachuaji utatokea.

worry out,
 
Haitasaidia Mkuu vijana wa siku hizi ni ngumu sana kuwadanganya labda wawachomoe ubongo zao wawe kama mazombie

Ni kweli unachosema, mie naamini huko ndo vijana wanaenda kuunganisha nguvu na kubadilishana mawazo namna ya kuiondoa sisiem, kwani watakuwa pamoja kwa muda mrefu, watakuja na mbinu mpya nyingi, kwa miaka 3 iliobaki watakuwa wamepikwa vijana sio chini ya milioni 1.5, litakuwa ni ongezeko kubwa la kuleta chachu ya mabadiliko.
 
Ni kweli unachosema, mie naamini huko ndo vijana wanaenda kuunganisha nguvu na kubadilishana mawazo namna ya kuiondoa sisiem, kwani watakuwa pamoja kwa muda mrefu, watakuja na mbinu mpya nyingi, kwa miaka 3 iliobaki watakuwa wamepikwa vijana sio chini ya milioni 1.5, litakuwa ni ongezeko kubwa la kuleta chachu ya mabadiliko.

Duuh! JKT bado naitiliashaka!
 
Nadhani CCM wameona Umuhimu wa Kurudisha JKT kwani ndio tegemeo lao kutumia mwanya huo kuzoa wanachama. Vijana watakaojiunga ni dhahili watalazimishwa kujiunga na MAGAMBA wapende wasipende. My take: JKT IJAYO SI KAMA ILE ILIYOPITA, HII IPO KIMKAKATI WAKUIBEBA CCM ZAIDI.

Hapa CCM inaweza kuwa na mipango ya aina mbili.

Mpango wa kwanza ni kutengeneza EPA au meremeta nyingine.

Mpango wa pili ni kuwaweka vijana kambini na kuwajaza woga.

Nimekuwa na wasiwasi huo kwa sababu hakuna mpango wowote unaoonekana kuwa umeandaliwa kwa ajili ya hao vijana watakaojiunga kwa mujibu wa sheria. Sitegemei vijana hao wasomi wa kidato cha sita kwenda JKT kupalilia mahindi kama zamani na kupiga pasi miradi (walopita makutupora wanaujua mradi) wakati sasa tunahitaji mechanised Agriculture.
 
Nadhani CCM wameona Umuhimu wa Kurudisha JKT kwani ndio tegemeo lao kutumia mwanya huo kuzoa wanachama. Vijana watakaojiunga ni dhahili watalazimishwa kujiunga na MAGAMBA wapende wasipende. My take: JKT IJAYO SI KAMA ILE ILIYOPITA, HII IPO KIMKAKATI WAKUIBEBA CCM ZAIDI.
Wapumbavu wanaotegemea kulindwa kama wanawake majumbani mwao utwajua tu!
 
Haina maana hata kidogo. Enzi za Jkt ikuwa ukimaliza majority walikuwa wanapelekwa kwenye vyuo husika na baadae ajira. Leo hii ni nani utakaembana aende jeshini? kwanza hata huko jeshini huna uwezo wa kuwapeleka wote, pili huna uwezo wa kuwaajiri. itawezekanaje? ujamaa na ubepari ni mifumo tofauti kabisa. Hv hawa jamaa hawaelewi? mi naona ni kutengeneza mapinduzi ya kijeshi ambayo hatuyataki. Cloroquin iliweza kutibu malaria huko nyuma leo haitibu na imepigwa marufuku.
 
Leo hii waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa akisoma bajeti ya wizara yake bungeni ametangaza kwamba kuanzia mwezi march mwakani wabunge vijana wanaotaka kupata mafunzo ya JKT wataanza kushiriki mafunzo hayo.

Hata hivyo spika akachomekea wakati waziri anasoma bajeti na kusema labda kwa mafunzo hayo wabunge hao vijana watabadilika
 
wapo wangapi! wawape hao magamba, wajifunze uzalendo! japo mm sioni mantiki ya kurudisha hayo mafunzo, ni njia nyingine ya ufisadi hiyo
 
Nimesikia msemaji wa kambi ya upinzania nimesikia akitoa salamu kwa magamba kwa ushindi wa uchaguzi halamashauri fulani please mwenye habari kamili atupe sijaipata vema.
 
Wabunge vijana wameomba kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na wamekubaliwa kufanya hivyo. Ila tofauti na vijana wengine watakaojiunga na jeshi hilo kwa mujibu wa sheria baada ya kuhitimu kidato cha sita mwezi Machi, 2013, wao watapata mafunzo hayo kwa majuma matatu tu ilhali wenzao watapata mafunzo hayo kwa miezi sita.

Hongereni wabunge wetu mkajifunze UZALENDO na MAADILI huko jeshini.

Source: Bungeni leo.
 
Wabunge vijana wameomba kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na wamekubaliwa kufanya hivyo. Ila tofauti na vijana wengine watakaojiunga na jeshi hilo kwa mujibu wa sheria baada ya kuhitimu kidato cha sita mwezi Machi, 2013, wao watapata mafunzo hayo kwa majuma matatu tu ilhali wenzao watapata mafunzo hayo kwa miezi sita.

Hongereni wabunge wetu mkajifunze UZALENDO na MAADILI huko jeshini.

Source: Bungeni leo.

This is another silly reasoning from CCM! Hivi kuna watu wanaopanga strategies katika serikali ya CCM na Bunge Lao.

What was the objective of JKT which was started 48 years ago and was the objective attained over the thirty years before it was dissolved ?

Nadhani wakati inaanzishwa Idadi ya vijana waliojiunga kwa mujibu aw sheria wale waliomaliza kidato cha Sita na walio kuwa wanataka katika vyuo vya Ualimu na
Ufundi na Medical assistants walikuwa wachache if you compare with today. Kilichopelekea kufutwa kwa JKT ni yale Makambi ya JKT kushindwa kuwa chukua vijana wengi walikuwa wanamaliza vyuo kwa sababu kambi hazikuongezeka kwa uwiano sawa.

Bila kumumunya
 
Wabunge vijana wameomba kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na wamekubaliwa kufanya hivyo. Ila tofauti na vijana wengine watakaojiunga na jeshi hilo kwa mujibu wa sheria baada ya kuhitimu kidato cha sita mwezi Machi, 2013, wao watapata mafunzo hayo kwa majuma matatu tu ilhali wenzao watapata mafunzo hayo kwa miezi sita.

Hongereni wabunge wetu mkajifunze UZALENDO na MAADILI huko jeshini.

Source: Bungeni leo.

This is another silly reasoning from CCM! Hivi kuna watu wanaopanga strategies katika serikali ya CCM na Bunge Lao.

What was the objective of JKT which was started 48 years ago and was the objective attained over the thirty years before it was dissolved ?

Nadhani wakati inaanzishwa Idadi ya vijana waliojiunga kwa mujibu aw sheria wale waliomaliza kidato cha Sita na walio kuwa wanataka katika vyuo vya Ualimu na
Ufundi na Medical assistants walikuwa wachache if you compare with today. Kilichopelekea kufutwa kwa JKT ni yale Makambi ya JKT kushindwa kuwa chukua vijana wengi walikuwa wanamaliza vyuo kwa sababu kambi hazikuongezeka kwa uwiano sawa.

Bila kumumunya maneno CCM hawajajiandaa kuweza kurudisha JKT kwa vile ideology au falsafa yenyewe haikuwa endelevu.

Therefore nawshauri wasikurupuke kutenga 7Bilion shilings za kurejesha JKT without redefining the philosophy and get popular mandate from the people. Kutumia Imla and dictating approach is doomed to total failure for the failed CCM policies.

Hao vijana Wabunge wanajiunga kufanya nini?
 
Ni baada tu ya kuhitimu kidato cha sita, wanafunzi wote baada ya paper ya mwisho tunaanza kupitia list nani kachaguliwa kwenda kambi ipi. Mimi nasoma nakuta natakiwa kureport MAKUTUPORA –Dom.

Naangalia list zaidi nakuta na rafiki yangu naye kapangwa makutupora – Tunapanga tukutane Dom ili tupange safari wote, tunaagana kwa likizo fupi majumbani kuaga wazazi wetu maana tuendako ni pagumu.

Wakati ule hakuna simu za mkononi, ila tunaitikia ahadi tunakutana Dodoma stend ile tarehe husika ilipofika, mimi namshauri rafiki yangu (ambaye kwa sasa ni Meja wa Jeshi) tuende Jpili na si leo ijumaa, Jumapili ni siku ya mapumziko kwa hiyo tutapata muda wa kuzoea kambi kabla ya kuanza mafunzo Jtatu asubuhi – tunakubaliana tunaondoka wote kwa mjomba wangu for two days rest.

Jumapili saa nane tunapanda gari tayari safari ya kuanza maisha ya JESHI. Mimi na yeye na mabegi yetu madogo mwili ukiwa tayari kwa lolote lile, ndani yamoyo wangu ni wasiwasi tu hivi kukuje huko? Mara konda anapita oyaa mnaenda wapi? Natamka tunaenda Makutupora JKT, watu kwenye basi wanageuka kutuagalia moyo unazidi kudunda mmhh kulikoni watu kuhamaki.

Nyie wa JKT haya mmeshafika, nauli tafadhali!! Tunalipa nauli tunachukua mabegi yetu gari inaondoka natamani irudi tuondoke nayo; Mbele naona Nembo ya jeshi,
JESHI LA KUJENGA TAIFA
MAKUTUPORA JKT.
UTII NA UKAKAMAVU ( Sikumbuki maandishi yote)

Tunatembea kwa tahadhali kubwa, hakuna anayeongea na mwenzake – ndani ya kambi naona kwa mbali watu wanakimbia kimbia nikahisi basi wale ni wenzetu ila wamepewa vibukta na Tshet za kijani, Mara tunasikia sauti ya juu ---
Kruta chuchumaa Chini-(hapo najua mziki sasa umeanza, huku najiuliza mbona leo ni jumapili hawa hawana weekend?)
Weka begi mgongoni – haya ruka kichura mpaka hapa tulipo (huyo alikuwa askari wa zamu lango kuu la kuingilia kambini)
Tulitii amri ile tukaruka kichura hadi main gate ---
Simama juu --- chuchumaa – amri hii ilidumu kama dakika tano aisee nikahisi ugali niliokula home unaanza kurudi kwenye koromeo taratibuu)

Baada ya hapo ni kupewa sheria za kambi ---1. Kila kitu unachoambiwa lazima ujibu – NDIYO AFANDE 2. Marufuku kutembea sababu Kruta hujafundiswa 3. Kila uendako hakikisha una Mestin (bakuli la msosi). Kanuni zingine mtazipata kombania – wewe (mimi) umepangiwa D copy na wewe A coy. Hapo ndiyo ukawa mwisho wetu maana tayari tumetenganishwa na rafiki yangu – kweli maisha mapya nitaweza kuumaliza mwaka mzima humu. Najiuliza nikiwa nimepoteza matumaini.

Naondoka na begi langu mwendo ni wa mbwa, yaani kukimbia hadi Kombania namkuta Sajenti pamoja na Kopro – haya Kruta chukua vifaa – hapo napewa Bukta, Fulana, zote za kijani Buti na mestini. Hawa jamaa mbona hawaangali size? Najiuliza kwa mshangao, kweli nimepewa bukta na fulana kubwa mno lakini nimeambiwa hakuna kuuliza swali hapa.

Nafika Hangani ( bweni ) nakutana na kuruta wenzengu, najitahidi kuwazoea kwa haraka hasa wale waliotoka kidato cha sita – nakutana na baadhi tuliosoma nao o'level Napata moyo wa maisha mapya, kabla hata sijaweka vitu vyangu nasikia filimbi – jamaa wananiambia kimbia twenda kombania afande kaja, aisee maisha naona magumu mno. Kombania nakutana na wasichana wengi tu, duh aisee moyo unaanza kuwa na imani, wote wamevaa vibukta na Tshit za kijani, kasoro mimi kwani sikupata muda wa kuvaa. Mara nasikia KRUTA WA DANGER –Jamaa wote wanajibu AFANDEEEEE!!!; Nawapa dakika 20 nikirudi nikute vyura wanalia kwenye hayo maua --- Wanajibu na mimi najitahidi kuzoea -- NDIYO AFANDEEE!!! Cha kushangaza hakuna ndoo, bomba ni moja maji yanatoka kidogo sana, sasa tumwagilie bustani hadi vyura walie --- naona mambo ya ajabu haya ila wenzangu waliofika mapema wameshazoea, wanachukua mestini zao foleni kukinga maji. hilo ndilo Jeshi -- Hakuna kuhoji hakuna Kutafakari ni Kutii amri.

Inafika saa tatu naambiwa jiandae tunaenda DISCO, duh kuna disko huku? nakumbuka aaahh leo ni Jpili kumbe ni Disco day -- kabla hata sijamaliza kufikiri zaidi naambiwa si DISCO la kucheza ni DISCO la kuimba kwa hiyo kumbuka wimbo wowote ule maana wewe lazima utachaguliwa na afande uimbishe - aisee maisha mapya kabisa.
Kweli zilikuwa Nyimbo za kupeana matumaini, nyimbo za ujasiri na hata nyimbo za kushekesha kama mabata madogo madogo yanaogelea......nk.


Wakuu hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kwanza JKT – kwa hiyo wabunge vijana mnaotaka kuandika majina yenu kwenda kulitumia Taifa (JKT) hakuna mwongozo wa spika kule, kule kila kitu unachoambiwa jibu ni NDIYO AFANDE – hakuna kuhoji wala kutafakari na hiyo ndiyo amri ya JESHI. Kwa hiyo kina Mnyika, Nasari, Zitto, Mchemba, Kafulila, Mdee, Makamba, Sugu na wengineo mkiandika majina basi msisahau kwenda kuaga makwenu maana lazima mrudi na alama unless muwe treated kama waheshimiwa kitu ambacho hakitakuwa na maana yoyote.

Otherwise ni sehemu ya kufurahia na uzuri wa jeshi Siku ikiisha basi imeisha, Hakuna mambo ya Jana ulitoroka NO; na kazi kubwa ya kutumia ubongo kule ni jinsi ya kumtoroka Afande wakati anapanga kazi ila uhakikishe unakula bila kukushika, akikushika utakula chakula vizuri ila utaanza doso kafie kwenu ambapo lazima msosi wote uliokula utokee mdomoni bila mpangilio.

Ni maisha mapya ya kufurahisha ingawa kuna siku utalia na kukumbuka wazazi wako.

Baadhi ya misemo kuje JESHINI
Kalinyekalinye - adhabu
Songombigo – adhabu kali
Doso kafie kwenu – hii lazima upimwe afya kwanza kabla hujaanza kuitumikia
Usawa wa Gudulia – Kwenye sufuria la msosi
Kujongomea –kutoroka
,Kichele – Kipindi hicho tulikuwa tunapata mshahara kwa mwezi – sikumbuki bei gani ila ilikuwa kidogo sana

OPERATION VYAMA VINGI – MAKUTUPORA JKT.
Kwa wale mnaokumbuka tulicheza gwalide la kufuzu kwa niamba ya kambi zote nchini – Mgeni rasmi alikuwa Mzee J. Malecela – wakati huo waziri mkuu. something to remember in life time. Go and Enjoy!!!
 
Back
Top Bottom