CCM na Mategemeo yao JKT

Mimi naomba waanze na wabunge hawa Vijana, vinginevyo CDM msikubali kwenda huko JKT
1. Dr. Hussein Mwinyi
2. Dr. Emmanuel Nchimbi
3. Dr. mathayo David Mathayo
4. Ummi Mwaalim
5. Angela Kairuki
6. January Makamba
7. Wliiam Ngereja
8. Steven Massele
9. George Simbachawene
10. Mwigulu Nchemba
11. Amos Makalla
12.

Waanze mawaziri na manaibu wote ambao hawakupitia JKT. Kama ni kisima CCM mlikuwa mnachimba mtatumbukiwa wenyewe!

Mbona Umemsahau Mbunge wa SINGIDA MJINI - DEWJI?

Lau Masha pia kama akitaka tena UBUNGE lazima aende
 
Wapendwa wanajamvi salaam kwenu,
Nimekuwa nikitatizwa sana na sera ambazo serikali imekuwa ikizitekeleza bila mpangilio maalumu. Kwa muda kidogo ilikuja na mpango wa kurejesha programu ya kupeleka wahitimu wa kidato cha sita kupata mafunzo ya JKT. Tatizo hasa linalonitatiza ni kile ambacho kimekuwa kikitolewa kama sababu ya kurudisha programu hiyo. Yamekuwepo masuala mbalimbali ambayo yamepelekea na kusababisha serikali ianzishe tena programu hii. Nadharia zipo nyingi sana lakini hizi mbili zimepata kuwa maarufu; kurejesha uzalendo kwa nchi na vijana wa sasa ni legelege hivyo tunahitaji kuwafanya kuwa wakakamavu.
Nitajadili nadharia mojamoja na wale ambao wana hoja madhubuti pamoja nao wale ambao ni wazamani kidogo enzi zile za program kama hii ilipokuwapo watasaidia kuniweka sahihi maana mi bado kijana mdogo ndo kwanza nimemaliza form six.
Nadharia ya uzalendo; Inashangaza kuona watu wenye akili timamu tunadhani uzalendo waweza kujengwa kwa mazoezi makali na ya mateso ya miezi sita kwa wahitimu wa kidato cha sita na wiki tatu kwa wabunge walio tayari na uzalendo kama Zitto Kabwe(Japo na yeye ni kati ya wafuasi wa mpango huu). Uzalendo ni hali ya kuwa na mapenzi ya dhati kwa taifa hasa katika kutetea rasilimali za taifa an maaslahi ya watu waliowengi katika taifa husika. Uzalendo hujengwa kwa misingi imara na mfumo wa kizalendo katika jamii ambamo mhusika amelelewa. Japokuwa mara nyingine uzalendo huweza kujengwa na matamanio ya mtu kuinasua jamii yake kutokana na uonevu wanaoupata kutoka kwa mtawala flani. Kwa misingi hiyo sidhani kama kuwapeleka raia ama vijana katika kambi za jeshi kwa mafunzo haya kupandikiza uzalendo litafanikiwa. Nalazimika kukumbuka nukuu hii wakati maamuzi kama haya yanapochukuliwa kwa minajili ya kurejesha uzalendo “No abounding of military training shall avail us if our spiritual senses atrophy. The foes of our own household will surely prevail against us unless there be in our people an inner life which finds its outer expression in a morality like unto that preached by the seers and the prophets of God”
Nadharia ya ukakamavu kwa vijana; Wakati naanza shule ya msingi tulikuwa na utaratibu wa kukimbia mchakamchaka asubuhi mwendo kama wa kilometa moja. Utaratibu huu wa kukimbia mchakamchaka ulikuwapo hata shuleni niliposoma o-level. Mi nadhani kuliko kupoteza rasilimali na pesa nyingi katika kuandaa camp za mafunzo na kuendesha hayo mafunzo yenyewe serikali ingefanya yafuatayo;

  1. Kwa shule za msingi na sekondari iwe ni lazima wanafunzi kukimbia mchakamchaka na kujihusisha moja kwa moja na kazi za nje kama kupalilia, kufyeka na kujihusisha na mazoezi ya viungo kwenye pindi za P.E( Physical education) hii itasaidia sana watoto kuanza kuondokana na uvivu na uzembe taratibu .
  2. Majeshi yetu kutuma vijana wake kama walivyofanya enzi za miaka ya themanini pale Tabora Boys kuwapa vijana angalau Short term training wakiwa bado wapo skuli. Ni vizuri pia kama wanaweza kupatiwa mafunzo ya mgambo kwani yanaweza kutolewa shuleni kama ambavyo wanawapa mazoezi na mafunzo watoto wa halaiki.
  3. Shule zenye mashamba (hizi ni nyingi mikoani) kuwashirikisha wanafunzi kwa kiasi fulani katika uzalishaji kwa muda ambao hautaathiri masomo yao.
  4. Wanafunzi washiriki shughuli kama kuwa scouts na uwekwe utaratibu wajaichanganye na jamii katika usafi wa miji na kazi nyingine za kujitolea.
Ni matumaini yangu kuwa njia hizo zinaweza kuwafanya vijana wawe wakakamavu na kujenga mazoea ya kufanya kazi hasa kama watazoezwa tangu wakiwa wadogo. Kwa mtazamo wangu hakuna sababu ya msingi kutenga pesa ambazo nchi ingeweza kutenga kunzisha miradi ambayo ingeweza kutoa ajira kwa vijana hao hao pindi watapomaliza vyuo.Katika mazingira ambayo taifa lina unemployment rate of about 10.7% nilitegemea mabilioni hayo ya pesa yangetumika hata kuanzisha viwanda vya kati ambavyo ni labour-intensive ili kuondoa bomu ambalo Mr. Lowassa humkumbusha Jakaya kila anapopata wasaa.
Nadharia ya kuongeza nguvu kazi JKT ; Hii ni nadharia ambayo imekuwa inaongelewa kwa chini kwamba wanafunzi hawa watapelekwa JKT kusaidia na kuongeza rasilimali watu katika programu zinazotekelezwa na JKT. Japo hii haisemwi sana lakini inaweza kuwa ni mkakati wenyewe hasa ikizingatia kwamba KILIMO KWANZA inaonekana imekuwa ni sera inayotekelezwa na JKT kwa bidii.
Kwa wale ndugu zangu wakubwa wa zamani ningependa mtujuze nini kilipelekea programu hii ya JKT kufutwa mwanzoni mwa miaka ya tisini? Na pili serikali wakati ilipoanzisha programu hii ilipata makusudio iliyoyatarijia hadi ilipofutwa? Lakini la mwisho utekelezaji wake kwa formula ya miaka hiyo utaweza kufanikiwa kwa kizazi hiki cha watoto mdebwedo, wazembe na wasiojua kilimo maana wengi wa mjini siku hizi.( Hapa namaaanisha mtoto wa Kariakoo au Masaki ashinde kwenye kazi ngumu kila siku miezi sita ) pamoja na masharobabies kama wajiitavyo wenyewe bila kuzimiazimia sana?

Naomba kuwasilisha.
 
Kama ni kuleta uzalendo ao viongoz mafisadi nao enz zao c walipita jkt? Nakumbuka kingunge aliwah kusema tusikurupuke!
 
Wangeanzisha mgambo tu. unatosha, Tupate vijana kama wale waliomnanihii gadafi.
 
Kumbukeni kwenye majeshi yetu hakuna 'no' zaidi ya ndio afande, yes sir huku chain in command ikizingatiwa kwa hali ya juu. Jeshi linanizamu yake katika ufanyaji wa shughuri zake kila siku na kikubwa zaidi 'no matter what kind of order you're given, kwao ni obedience ndio msingi wa nizamu. Taifa letu linakabiliwa na tatizo kubwa la ajira kwa vijana sina uhakika ni wastani wa % ngapi but nisawa na alivyosema Lowasa. Kwahiyo maswari unayopaswa kujiuliza wanajeshi wetu kuanzia mgambo, polisi hadi JWTZ wanapiga kura kipindi cha chaguzi au vipi? Na wadhani kama wako tayari kwenda kupiga watu virungu na mabomu wanapoandamana kudai haki je wakati wa kupiga kura wanachagua chama gani zaidi ya chama kilichowapa ulaji? Kwahiyo hili swala la JKT kikwete aliliongelea tangia ule uchaguzi wa kwanza 2005, swali la kujiuliza kwanini miaka yote hiyo program hii haikuanzishwa hadi ianzishwe sasa!? Ukifikiria hapo utapata jibu.
Kiukweli CCM imepoteza mvuto kwa vijana,kuanzisha JKT nia nikuwakama na kuhakikisha uchaguzi ujao wanapata kura za wote watakaokua wamejiunga na JKT. Hili jambo wamelipeleka kisiasa na sio kwamba serikali yetu inania ya kuwakomboa vijana waliomtaani wakihangaika na maisha magumu. Graduates wengi wapo mtaani, ajira wanatoa kwa kujuana baada ya mtoto wa aunt. Uncle sijui wa fulani wameshapata ndipo wanaangalia wengine.
Cha msingi ni kubadilisha mfumo mzima wa kiutawala na kuwaweka watu walio serious kweli na wenye nia ya kweli kuiona nchi yetu inasonga mbele kimaendeleo na sio kuburatana kama inavyofanya serikali hii.
 
Wapendwa wanajamvi salaam kwenu,
Nimekuwa nikitatizwa sana na sera ambazo serikali imekuwa ikizitekeleza bila mpangilio maalumu. Kwa muda kidogo ilikuja na mpango wa kurejesha programu ya kupeleka wahitimu wa kidato cha sita kupata mafunzo ya JKT. Tatizo hasa linalonitatiza ni kile ambacho kimekuwa kikitolewa kama sababu ya kurudisha programu hiyo. Yamekuwepo masuala mbalimbali ambayo yamepelekea na kusababisha serikali ianzishe tena programu hii. Nadharia zipo nyingi sana lakini hizi mbili zimepata kuwa maarufu; kurejesha uzalendo kwa nchi na vijana wa sasa ni legelege hivyo tunahitaji kuwafanya kuwa wakakamavu.
Nitajadili nadharia mojamoja na wale ambao wana hoja madhubuti pamoja nao wale ambao ni wazamani kidogo enzi zile za program kama hii ilipokuwapo watasaidia kuniweka sahihi maana mi bado kijana mdogo ndo kwanza nimemaliza form six.
Nadharia ya uzalendo; Inashangaza kuona watu wenye akili timamu tunadhani uzalendo waweza kujengwa kwa mazoezi makali na ya mateso ya miezi sita kwa wahitimu wa kidato cha sita na wiki tatu kwa wabunge walio tayari na uzalendo kama Zitto Kabwe(Japo na yeye ni kati ya wafuasi wa mpango huu). Uzalendo ni hali ya kuwa na mapenzi ya dhati kwa taifa hasa katika kutetea rasilimali za taifa an maaslahi ya watu waliowengi katika taifa husika. Uzalendo hujengwa kwa misingi imara na mfumo wa kizalendo katika jamii ambamo mhusika amelelewa. Japokuwa mara nyingine uzalendo huweza kujengwa na matamanio ya mtu kuinasua jamii yake kutokana na uonevu wanaoupata kutoka kwa mtawala flani. Kwa misingi hiyo sidhani kama kuwapeleka raia ama vijana katika kambi za jeshi kwa mafunzo haya kupandikiza uzalendo litafanikiwa. Nalazimika kukumbuka nukuu hii wakati maamuzi kama haya yanapochukuliwa kwa minajili ya kurejesha uzalendo “No abounding of military training shall avail us if our spiritual senses atrophy. The foes of our own household will surely prevail against us unless there be in our people an inner life which finds its outer expression in a morality like unto that preached by the seers and the prophets of God”
Nadharia ya ukakamavu kwa vijana; Wakati naanza shule ya msingi tulikuwa na utaratibu wa kukimbia mchakamchaka asubuhi mwendo kama wa kilometa moja. Utaratibu huu wa kukimbia mchakamchaka ulikuwapo hata shuleni niliposoma o-level. Mi nadhani kuliko kupoteza rasilimali na pesa nyingi katika kuandaa camp za mafunzo na kuendesha hayo mafunzo yenyewe serikali ingefanya yafuatayo;

  1. Kwa shule za msingi na sekondari iwe ni lazima wanafunzi kukimbia mchakamchaka na kujihusisha moja kwa moja na kazi za nje kama kupalilia, kufyeka na kujihusisha na mazoezi ya viungo kwenye pindi za P.E( Physical education) hii itasaidia sana watoto kuanza kuondokana na uvivu na uzembe taratibu .
  2. Majeshi yetu kutuma vijana wake kama walivyofanya enzi za miaka ya themanini pale Tabora Boys kuwapa vijana angalau Short term training wakiwa bado wapo skuli. Ni vizuri pia kama wanaweza kupatiwa mafunzo ya mgambo kwani yanaweza kutolewa shuleni kama ambavyo wanawapa mazoezi na mafunzo watoto wa halaiki.
  3. Shule zenye mashamba (hizi ni nyingi mikoani) kuwashirikisha wanafunzi kwa kiasi fulani katika uzalishaji kwa muda ambao hautaathiri masomo yao.
  4. Wanafunzi washiriki shughuli kama kuwa scouts na uwekwe utaratibu wajaichanganye na jamii katika usafi wa miji na kazi nyingine za kujitolea.
Ni matumaini yangu kuwa njia hizo zinaweza kuwafanya vijana wawe wakakamavu na kujenga mazoea ya kufanya kazi hasa kama watazoezwa tangu wakiwa wadogo. Kwa mtazamo wangu hakuna sababu ya msingi kutenga pesa ambazo nchi ingeweza kutenga kunzisha miradi ambayo ingeweza kutoa ajira kwa vijana hao hao pindi watapomaliza vyuo.Katika mazingira ambayo taifa lina unemployment rate of about 10.7% nilitegemea mabilioni hayo ya pesa yangetumika hata kuanzisha viwanda vya kati ambavyo ni labour-intensive ili kuondoa bomu ambalo Mr. Lowassa humkumbusha Jakaya kila anapopata wasaa.
Nadharia ya kuongeza nguvu kazi JKT ; Hii ni nadharia ambayo imekuwa inaongelewa kwa chini kwamba wanafunzi hawa watapelekwa JKT kusaidia na kuongeza rasilimali watu katika programu zinazotekelezwa na JKT. Japo hii haisemwi sana lakini inaweza kuwa ni mkakati wenyewe hasa ikizingatia kwamba KILIMO KWANZA inaonekana imekuwa ni sera inayotekelezwa na JKT kwa bidii.
Kwa wale ndugu zangu wakubwa wa zamani ningependa mtujuze nini kilipelekea programu hii ya JKT kufutwa mwanzoni mwa miaka ya tisini? Na pili serikali wakati ilipoanzisha programu hii ilipata makusudio iliyoyatarijia hadi ilipofutwa? Lakini la mwisho utekelezaji wake kwa formula ya miaka hiyo utaweza kufanikiwa kwa kizazi hiki cha watoto mdebwedo, wazembe na wasiojua kilimo maana wengi wa mjini siku hizi.( Hapa namaaanisha mtoto wa Kariakoo au Masaki ashinde kwenye kazi ngumu kila siku miezi sita ) pamoja na masharobabies kama wajiitavyo wenyewe bila kuzimiazimia sana?

Naomba kuwasilisha.

Mdogo wangu nalazimika kukuita hivyo kwa sababu umesema wewe ni form six naomba nikuambie kwanza kabisa kuwa wewe ni mwoga tu hakuna raha kama kupata military knowledge katika maisha yako hilo fahamu hivyo kwanza.
Sasa ngoja niendelee faida iliyotokana na watu kupitia JKT ni kama ifutavyo:
  1. Watu walifahamiana kwa kwakuwa kwenye JKT watu wote walikutana huku bila kujali imani zao na hali zao kiuchumi wote walikuwa sawa tofauti na sasa mgawanyiko ni mkubwa aliyesoma shule ya Kata na aliyesoma St. some one hilo gap kwa sasa litarekebishwa na JKT watu wachangia kambi chakula na malazi kwa ubora ule ule bila kujali wewe ni nani na una nguvu gani kiuchumi.
  2. Faida nyingine iliyopatikana na itakayopatikana kutokana na mafunzo hayo ni ukakamavu na nidhamu ambayo kwa sasa imeshuka sana kwa vijana kama wewe unakuta mtu amemaliza chuo kikuu lakini anavaa nguo chupi yake inaonekana hata mbele ya mama yake mzazi na dada zake!!! Jambo ambalo huwezi kulikuta jeshini na zaidi ya yote pia unakuwa mbunifu kukabili mazingira yoyote yale magumu na pia ni rahisi kwa aliyepitia jeshi kujilinda binafsi kwa usahihi tofauti na asiye na mafunzo ya kijeshi.
  3. Magonjwa mengi yamekuwa tishio kwa vijana wa sasa kutokana na matumizi ya vyakula bila mazoezi kwa hiyo ukienda JKT hutapata magonjwa kama kisukari na mengineyo ikiwa utazingatia mafunzo hayo na wengi waliopitia JKT na wakazingatia mafunzo hayo hutawakuta wanamatizo ya magonjwa yatokanayo na uzembe.
  4. Pale kwenye red na bold JKT ni zaidi ya hapo kipindi kile tulikuwa tunakimbia mchakamchaka na ilikuwepo elimu ya kujitegemea, chipukizi na Scout sasa hivi hivyo vyote havifanyiki kabisa shuleni na ilikuwa mwanafunzi akifanya kosa anachapwa na akienda nyumbani kusema kama kaonewa na mwalimu mzazi alikuwa anamtandika na kumrudisha shuleni kwa sasa mambo hakuna mwalimu akimchapa mwanafunzi anapelekwa polisi na matokeo yake walimu nao wamekata tamaa na matokeo yake wanatumia mbinu chafu kuwafaulisha wanafunzi bila kusoma kwa ushahidi angalia wanafunzi wanaokwenda kuanza form one hawajua hata kuandika majina yao,Walimu hawa wangepitia JKT wasingefanya madudu haya na pia Mwalimu huyohuyo utamkuta amevaa mdebwedo unadhani mwanafunzi wake ataacha kucopy na kupaste akiamini huo ndiyo uvaaji sahihi JKT hakuna ujinga huo,Israel watu wote wanapata mafunzo ya kijeshi toka shule ya msingi na hiyo imewafanya kuwa mahiri siyo katika jeshi tu bali katika kila fani kuanzia kilimo na sayansi na technologia duniani wameweza kubadili jangwa na kufanya eneo la kilimo bora na kamwe haina njaa hata siku. Tanzania ni zidi ya Israel, JKT inaweza kuikomboa kiuchumi kama itatumika vizuri kama alivyowahi kusema Dr. Juliani Bujugo mmiliki wa shule za Green acres. Shule zilizokuwa na mchepuo wa kijeshi kama Tabora Boys/Girls umeondolewa kwa sababu tu baadhi ya viongozi hawakutaka watoto wao wapate elimu ya kijeshi kwa kisingizio wanateseka, shule za scout nazo kwa sasa hakuna kabisa ila moja tu kwa Col Kipingu na ukipata product ya pale wale vijana wako smart kama waliosoma seminary huwezi ukamkuta kijana goigoi na siye mbunifu wengi wana majibu na future zao tofauti na wengine wanasoma shule za kitajiri wanaishi kwa kutumia akili za wazazi wao au walezi wao kwani muda wote hawana cha kufikiri zaidi ya kufanya starehe kwa kujua kila kitu yupo atakayewafanyia na hii ni hatari kwa maisha yao. lakini ukipita JKT utatengenezewa mazingira ya kufikiri zaidi na kutatua matizo yako kwa kutumia akili yako mwenyewe tofauti na hivyo utaumia jambo ambalo hutakuwa tayari kuruhusu uumie na hivyo kusudio litakuwa limekamilika.
  5. JKT kama taasisi zingine zote kwa wakati ule ilikuwa na mapungufu kidogo kwa hasa suala la haki za binadamu lakini hayo yote yamerekebishwa kwenda na wakati tulio nao sasa kwani jeshi la sasa ni tofauti na jeshi la miaka ya themanini mpaka tisini mambo mengi yameboreshwa.
KWA NINI JKT ILIFUFUTWA MIAKA YA TISINI
Kwa uelewa wangu hakuna sababu za msingi zilizosababisha JKT kufutwa kwa wakati ule kwa sababu kama ni sababu za kiuchumi sikubaliani nazo mpaka sasa kwani mtu anapokuwa JKT anazalisha zaidi ya anavyotumia sasa hapo tatizo liko wapi? kama ilivyo kwa Azimio la arusha kufutwa kwa kutumia azmio la zanzibar watu wenye nguvu serikalini walitunga kitu na wakafanikiwa kuwashawishi wenye mamlaka kupunguza muda toka mwaka mmoja na kuwa miezi sita na hatimaye kuondolewa kabisa.

Hao wavaa mdebwedo na masharobaro ndiyo wanatakiwa wapelekwe JKT wakawe shaped kule, kwani kule hakuna wa Masaki wala wa manzese na tandale. Umetoa maelezo haya yote kutaka kutuaminisha kuwa jambo hili haliwezekani kwa hoja zako dhaifu za kutaka kuhalalisha uzembe, Tanzania ni moja hayo matabaka unayoyasema wa Masaki hawawezi mikikimikiki ya JKT unajidanganya wataweza tu kama huamini waulize wenzio na ningependa wewe uniambie umeomba kwenda kambi gani naamini utang'angania uwe mwanajeshi baada ya kuvuliwa tabia za uraiani dogo jeshini kuna raha utapapenda tu ila ngoma iko kwenye miezi miwili ya kwanza baada ya hapo utasema hivi kuna mahali penye raha kama jeshini?

Baada ya maelezo hayo hapo juu utakuwa umeelewa mambo ambayo hukuyajua na wenzangu watakuongezea watakayoona nimepunguza.
 
badala ya kuboresha elimu na kutengeneza ajira kwa vijana wanawapeleka kushika bunduki uh! Nafikiri it is a matter of time kabla ya kuanza kuibuka kwa magenge ya uhalifu na ugaidi mbali mbali nchini
 
Nadhani CCM wameona Umuhimu wa Kurudisha JKT kwani ndio tegemeo lao kutumia mwanya huo kuzoa wanachama. Vijana watakaojiunga ni dhahili watalazimishwa kujiunga na MAGAMBA wapende wasipende. My take: JKT IJAYO SI KAMA ILE ILIYOPITA, HII IPO KIMKAKATI WAKUIBEBA CCM ZAIDI.

Hii ninaweza kukubaliana na wewe kiasi fulani. Nakumbuka wakati ule kulikuwa na wanajeshi makada waliokuwa wanafundisha siasa. Hawa ndio wakina Kikwete, Kinana, Makamba, Chiligati, etc ambao mara nyingi huwa wanazawadiwa ukuu wa mikoa, wilaya, nk. Huwa bado wanaendelea na vyeo vyao hata wanapokuwa uraiani.

Wale wapiganaji ambao pia ni makada wa chama wanaofikia vyeo vya juu (Brigedia, majenerali) wanazawadiwa sehemu nono kama ukurugenzi wa vitengo muhimu na ubalozi nchi za nje (Hashim Mbita - Katibu wa Nchi zilizokuwa mstari wa Mbele, Lupogo - TACAIDS, etc).

Hii JKT inayokuja kabla hatujajiuliza kama jeshi letu limejitenga na siasa (Wameondolewa wote walio na ukoko wa CHAMA) itatuletea dhahma katika mustakabali wa demokrasia ya ukweli.

JKT mpya ianzishwe na Askari wapya walioandaliwa kitaalamu zaidi kwa kuangalia uzalendo na maslahi ya taifa. Wakubwa wote walioko sasa jeshini wasihusike kwa namna yoyote kwenye mafunzo haya. Then tutakuwa na imani kuwa JKT sio kitengo cha kuwafunza Janjaweed wa CCM.
 
Mdogo wangu nalazimika kukuita hivyo kwa sababu umesema wewe ni form six naomba nikuambie kwanza kabisa kuwa wewe ni mwoga tu hakuna raha kama kupata military knowledge katika maisha yako hilo fahamu hivyo kwanza.
Sasa ngoja niendelee faida iliyotokana na watu kupitia JKT ni kama ifutavyo:
  1. Watu walifahamiana kwa kwakuwa kwenye JKT watu wote walikutana huku bila kujali imani zao na hali zao kiuchumi wote walikuwa sawa tofauti na sasa mgawanyiko ni mkubwa aliyesoma shule ya Kata na aliyesoma St. some one hilo gap kwa sasa litarekebishwa na JKT watu wachangia kambi chakula na malazi kwa ubora ule ule bila kujali wewe ni nani na una nguvu gani kiuchumi.
  2. Faida nyingine iliyopatikana na itakayopatikana kutokana na mafunzo hayo ni ukakamavu na nidhamu ambayo kwa sasa imeshuka sana kwa vijana kama wewe unakuta mtu amemaliza chuo kikuu lakini anavaa nguo chupi yake inaonekana hata mbele ya mama yake mzazi na dada zake!!! Jambo ambalo huwezi kulikuta jeshini na zaidi ya yote pia unakuwa mbunifu kukabili mazingira yoyote yale magumu na pia ni rahisi kwa aliyepitia jeshi kujilinda binafsi kwa usahihi tofauti na asiye na mafunzo ya kijeshi.
  3. Magonjwa mengi yamekuwa tishio kwa vijana wa sasa kutokana na matumizi ya vyakula bila mazoezi kwa hiyo ukienda JKT hutapata magonjwa kama kisukari na mengineyo ikiwa utazingatia mafunzo hayo na wengi waliopitia JKT na wakazingatia mafunzo hayo hutawakuta wanamatizo ya magonjwa yatokanayo na uzembe.
  4. Pale kwenye red na bold JKT ni zaidi ya hapo kipindi kile tulikuwa tunakimbia mchakamchaka na ilikuwepo elimu ya kujitegemea, chipukizi na Scout sasa hivi hivyo vyote havifanyiki kabisa shuleni na ilikuwa mwanafunzi akifanya kosa anachapwa na akienda nyumbani kusema kama kaonewa na mwalimu mzazi alikuwa anamtandika na kumrudisha shuleni kwa sasa mambo hakuna mwalimu akimchapa mwanafunzi anapelekwa polisi na matokeo yake walimu nao wamekata tamaa na matokeo yake wanatumia mbinu chafu kuwafaulisha wanafunzi bila kusoma kwa ushahidi angalia wanafunzi wanaokwenda kuanza form one hawajua hata kuandika majina yao,Walimu hawa wangepitia JKT wasingefanya madudu haya na pia Mwalimu huyohuyo utamkuta amevaa mdebwedo unadhani mwanafunzi wake ataacha kucopy na kupaste akiamini huo ndiyo uvaaji sahihi JKT hakuna ujinga huo,Israel watu wote wanapata mafunzo ya kijeshi toka shule ya msingi na hiyo imewafanya kuwa mahiri siyo katika jeshi tu bali katika kila fani kuanzia kilimo na sayansi na technologia duniani wameweza kubadili jangwa na kufanya eneo la kilimo bora na kamwe haina njaa hata siku. Tanzania ni zidi ya Israel, JKT inaweza kuikomboa kiuchumi kama itatumika vizuri kama alivyowahi kusema Dr. Juliani Bujugo mmiliki wa shule za Green acres. Shule zilizokuwa na mchepuo wa kijeshi kama Tabora Boys/Girls umeondolewa kwa sababu tu baadhi ya viongozi hawakutaka watoto wao wapate elimu ya kijeshi kwa kisingizio wanateseka, shule za scout nazo kwa sasa hakuna kabisa ila moja tu kwa Col Kipingu na ukipata product ya pale wale vijana wako smart kama waliosoma seminary huwezi ukamkuta kijana goigoi na siye mbunifu wengi wana majibu na future zao tofauti na wengine wanasoma shule za kitajiri wanaishi kwa kutumia akili za wazazi wao au walezi wao kwani muda wote hawana cha kufikiri zaidi ya kufanya starehe kwa kujua kila kitu yupo atakayewafanyia na hii ni hatari kwa maisha yao. lakini ukipita JKT utatengenezewa mazingira ya kufikiri zaidi na kutatua matizo yako kwa kutumia akili yako mwenyewe tofauti na hivyo utaumia jambo ambalo hutakuwa tayari kuruhusu uumie na hivyo kusudio litakuwa limekamilika.
  5. JKT kama taasisi zingine zote kwa wakati ule ilikuwa na mapungufu kidogo kwa hasa suala la haki za binadamu lakini hayo yote yamerekebishwa kwenda na wakati tulio nao sasa kwani jeshi la sasa ni tofauti na jeshi la miaka ya themanini mpaka tisini mambo mengi yameboreshwa.
KWA NINI JKT ILIFUFUTWA MIAKA YA TISINI
Kwa uelewa wangu hakuna sababu za msingi zilizosababisha JKT kufutwa kwa wakati ule kwa sababu kama ni sababu za kiuchumi sikubaliani nazo mpaka sasa kwani mtu anapokuwa JKT anazalisha zaidi ya anavyotumia sasa hapo tatizo liko wapi? kama ilivyo kwa Azimio la arusha kufutwa kwa kutumia azmio la zanzibar watu wenye nguvu serikalini walitunga kitu na wakafanikiwa kuwashawishi wenye mamlaka kupunguza muda toka mwaka mmoja na kuwa miezi sita na hatimaye kuondolewa kabisa.

Hao wavaa mdebwedo na masharobaro ndiyo wanatakiwa wapelekwe JKT wakawe shaped kule, kwani kule hakuna wa Masaki wala wa manzese na tandale. Umetoa maelezo haya yote kutaka kutuaminisha kuwa jambo hili haliwezekani kwa hoja zako dhaifu za kutaka kuhalalisha uzembe, Tanzania ni moja hayo matabaka unayoyasema wa Masaki hawawezi mikikimikiki ya JKT unajidanganya wataweza tu kama huamini waulize wenzio na ningependa wewe uniambie umeomba kwenda kambi gani naamini utang'angania uwe mwanajeshi baada ya kuvuliwa tabia za uraiani dogo jeshini kuna raha utapapenda tu ila ngoma iko kwenye miezi miwili ya kwanza baada ya hapo utasema hivi kuna mahali penye raha kama jeshini?

Baada ya maelezo hayo hapo juu utakuwa umeelewa mambo ambayo hukuyajua na wenzangu watakuongezea watakayoona nimepunguza.


Tatizo la baadhi ya watu ni kuwa hamkubali ukweli kwamba dunia ya sasa ni tofauti na zamani. Kama wewe unategemea kupanda mlima kwa kutumia kamba karne hii au kwenda vitani kwa kutumia kikosi cha askari wa infantry utakuwa unakosea. Angalia wamarekani walivyoendesha mission ya kumkamata Osama, ni akili, teknolojia na ubunifu hayo ya uzalendo unataka kufanya turudi kwenye karne ya ukombozi wa Afrika kitu ambacho sikubaliani nacho.

Fahamu kuwa wengi tulienda JKT na sio ishu sana ni jambo la kawaida tu na ukimaliza kule ukirudi kitaa baada ya mwaka tu huo ukakamavu unaisha maana huwezi kung'ang'ania ukakamavu wakati wenzio wanatengeneza hela mjini hapa.

JKT ni tatizo kubwa sana, watu watamaliza mafunzo then warudi mtaani, usalama wa raia watapata kazi kubwa mno nawaambieni, hata ujambazi utakaofanyika utakuwa very classified! Tusiangalie kwa upande wa sifa eti utakakamaa, wote tulienda huko na hakuna cha maana sio lazima wote tuwe wanajeshi wakati tunahitaji mathematicians, computer gurus etc! Nadhani JKT ibakie kama voluntary upon someone's volition. Kama wataweka lazima inamaana mtu akiumia kwenye mafunzo wakati hakutoa idhini yake wakati wa kujiunga serikali imejiandaa vipi kuja kulipa fidia wahanga wa ubabe huo? Kuna wakati mambo mengi ya kitaalamu yanatakiwa yafikiriwe sio tu kukurupuka na kufanya vitu kipuuzi eti kisa Israel wanafanya hivyo, wao wanamaana yao, kwao ni ugomvi na Palestina miaka yote they need such policy, leo TZ ina haja gani ya kuwa na vijana wakakamavu bila kuwatengenezea ajira?

Watarudi mtaani, watakosa kazi, wanajua silaha na mbinu zote za kijeshi, sijui kama kuna askari atakaewagusa nawaambieni kwa hakika.
 
Nadhani CCM wameona Umuhimu wa Kurudisha JKT kwani ndio tegemeo lao kutumia mwanya huo kuzoa wanachama. Vijana watakaojiunga ni dhahili watalazimishwa kujiunga na MAGAMBA wapende wasipende. My take: JKT IJAYO SI KAMA ILE ILIYOPITA, HII IPO KIMKAKATI WAKUIBEBA CCM ZAIDI.
Nikutokuwa na upeo leo hii nimsomeshe mtoto wangu kwenye Academy then uniambie akaende kutumika kwenye JKT??Nonsense...for CCM....Kwakipindi hicho kulikuwa na shule za serikali na vyuo vya serikali!
 
Tatizo la baadhi ya watu ni kuwa hamkubali ukweli kwamba dunia ya sasa ni tofauti na zamani. Kama wewe unategemea kupanda mlima kwa kutumia kamba karne hii au kwenda vitani kwa kutumia kikosi cha askari wa infantry utakuwa unakosea. Angalia wamarekani walivyoendesha mission ya kumkamata Osama, ni akili, teknolojia na ubunifu hayo ya uzalendo unataka kufanya turudi kwenye karne ya ukombozi wa Afrika kitu ambacho sikubaliani nacho.

Fahamu kuwa wengi tulienda JKT na sio ishu sana ni jambo la kawaida tu na ukimaliza kule ukirudi kitaa baada ya mwaka tu huo ukakamavu unaisha maana huwezi kung'ang'ania ukakamavu wakati wenzio wanatengeneza hela mjini hapa.

JKT ni tatizo kubwa sana, watu watamaliza mafunzo then warudi mtaani, usalama wa raia watapata kazi kubwa mno nawaambieni, hata ujambazi utakaofanyika utakuwa very classified! Tusiangalie kwa upande wa sifa eti utakakamaa, wote tulienda huko na hakuna cha maana sio lazima wote tuwe wanajeshi wakati tunahitaji mathematicians, computer gurus etc! Nadhani JKT ibakie kama voluntary upon someone's volition. Kama wataweka lazima inamaana mtu akiumia kwenye mafunzo wakati hakutoa idhini yake wakati wa kujiunga serikali imejiandaa vipi kuja kulipa fidia wahanga wa ubabe huo? Kuna wakati mambo mengi ya kitaalamu yanatakiwa yafikiriwe sio tu kukurupuka na kufanya vitu kipuuzi eti kisa Israel wanafanya hivyo, wao wanamaana yao, kwao ni ugomvi na Palestina miaka yote they need such policy, leo TZ ina haja gani ya kuwa na vijana wakakamavu bila kuwatengenezea ajira?

Watarudi mtaani, watakosa kazi, wanajua silaha na mbinu zote za kijeshi, sijui kama kuna askari atakaewagusa nawaambieni kwa hakika.

Nilisema ikiwa utayatumia mafunzo vizuri yana faida kuliko, hasara technologia kama uliyotolea mfano wa kumkamata Osama usije ukafikiri wale jamaa ni goigoi kwa sababu ya technologia wale jamaa wako fit hata kukuvujna shingo bila silaha na kumbuka kile kilikuwa ni kikosi maalumu cha makomandoo hivyo kama ulipita kweli JKT unajua nini maana ya Commandos, Huwezi kutengeneza ajira kwenye kundi la watu goigoi na wagonjwa hivo ukakamavu ni hatua ya kwanza ya pili ajira na huko JKT ajira zitapatikana kutokana na miradi itakayoanzishwa. Najua ni woga tu unakusumbua ndiyo maana unapinga JKT, Sera za Israel ni zaidi ya vita kama unavyofikiri wewe kilimo na uchumi wamefanikiwa kwa sera hiyo unayoiita wewe ya vita kumbuka mtu mkakamavu anafanya kazi nyingi na kwa muda mfupi kuliko asiye fanya mazoezi hasa katika kipindi hiki cha technologia uvivu umeongezeka sana. Kama kweli ulipita JKT na hukutoroka huwezi kulalamika kwamba ajira hakuna ni mzembe wewe JKT unafundishwa kujitegemea na siyo kuwa tegemezi. Hakuna atakayekuwa Jambazi kwani ujambazi ni tabia ya mtu mbona sasa hivi mafunzo ya JKT hakuna kwa mujibu wa sheria na watu ni majambazi wakiwemo asikari ambao wana ajira? Kama ajira ni shuluhisho la ujambazi inakuwaje huyu askari mwenye ajira akaibe tena il hali kazi anayo? Tamaa za mtu binafsi ni chanzo cha uhali na siyo kozi aliyo nayo. Nidhamu wanayofundishwa ndiyo itakayo wafanya watii mamlaka zilizopo mbona wanajeshi tunao na hawana ugomvi na idara zingine za usalama wa raia? Wewe kama ni mhalifu hata usipopewa kozi ya kijeshi utaiba tu kwani ni tabia zako, mambo haya siyo mapya hapa tz usiwatie hofu wasiojua kitu.
 
Hata shule za kata walidhani ni mbinu mojawapo ya kuiimasha ccm lakini sasa wanajuta! Huko kwenye Jkt ndio vijana watazidi kuichukia ccm vizuri..
 
Haija kaa vizuri,

ingekaa vizuri kama ingesema,
wabunge wote ambao hawajawahi kupita JKT,
ni lazima waende kwenye mafunzo hayo,
irrespective of their age.
Ikumbukwe kwamba,
hii si mara ya kwanza,
kwa waheshimiwa kwenda JKT,
kwa mafunzo maalumu.

Mzee Aboud Jumbe na Mrehemu Kawawa,
waliwahi kuhudhuria,
Crush program ya JKT miaka ya 70.
I believe kuna picha ya hawa waheshimiwa,
somewhere wakiwa wamevaa gear zao,
tayari kwa uchaka.
 
Wataikubali hata kwa kuchapwa viboko. Huo ndio mkakati uliopo!

Hii ni strategy ingawa wengi hawajaiona bado. Wakati wa uchaguzi mkuu kambi zitaongezeka zaidi na vijana wengi watapelekwa jeshini. Kura zitapigiwa jeshini na ndipo watakapochakachua BIG TIME. Wanajua jeshini hata kura zikiibiwa hakuna atakaefanya chochote, hakuingiliki kule.

CCM huwa hawafanyi kitu kwa nia njema ya taifa bali ya CCM.
 
si kweli, sasa hivi demokrasia imetapakaa kila mahali.. hizo ni dhana potofu za kuwagawa watu kichama ref: uchaguzi wa 2010 cdm iliongoza mitaa ya masaki, makongo ambayo ni ngome ya jeshi tena kwa gap la mamia ya kura, kambi nyingine karibu zote tz cdm ilipeta tofauti na watu walivyofikiri mwanzo kuwa uko ndio uchakachuaji utatokea.

worry out,

Hilo wameliona usitegemee watarudia hilo kosa tena. Sasa CDM walale usingizi wakijua watapa kura jeshini. Watch out CCM wapo kimaslahi zaidi.
 
Back
Top Bottom