CCM na magari ya uchaguzi...

Makala kama kweli ni mkweli yeye alitakiwa kuwapa waandishi wa habari hizi risiti wazione na awape copy waweke hadharani maana si siri ila alitaka ukweli . Tutajuaje kama risiti hizo ni za magari yaliyo bandarini ? Why idadi inapungiua tena na wakati wakubwa wake walisema ni 200 ? Je baada ya kumwita Slaa muongo ndiyo hawaendi mahakamani kama walivyo tamka ? Bado kuna siri kubwa ukweli mwingi umefichwa.Ngojeeni Slaa akiibuka .

Lunyungu,

Mpeni Dr. Slaa data za ukweli. Akikosea mara mbili au tatu kama alivyofanya kweli hili la magari, tayari mnakuwa mmewapa CCM ngao ya kummaliza. Kumbuka ya Mrema, alikuwa analipua mabomu ya kweli lakini baada ya muda CCM wakaanza kumpelekea data fake ili aumbuke na kuonekana mwongo.

Ni mategemeo yangu hatutaenda huko na Dr. Slaa. Hii habari sio siri Dr. Slaa ameongea kitu ambacho sio ukweli.
 
SHUPAZA na Wana JF,

Kilichobakia ni kuhakikisha Dr. W. Slaa anakuwa Rais wa nchi yetu mwaka ujao. Kazi ifanyike. Hakuna mbadala.

HAwezi kuwa rais labda 2015, urais ni zaidi ya mtu mmoja!! Hiyo CHADEMA itaunda serikali kwa potential figures zipi? Tuwe realistic sometimes... na tuache kumuonea Slaa, wacha aendelee kuwa mbunge kwani kule mchango wake ni muhimu sana
 
Tatizo ni Registrar of Political Parties...lazima vyama vi-file in returns za mapato yao aidha toka kwenye michango,fadhila nk..hili sijalisikia Tanzania lakini kwingineko ipo..hata UK ilitoka zogo siku za nyuma juu ya finances za labour...15bn/- sio mzaha..wamwpata wapi?Ruzuku haifiki huko na sidhani wanachama wanalipa michango yao maana sijaona mkakati wa makamba.makalla & co(walaji not advocates) kufuatilia memebrs fees hata kwa speech
 
Tatizo ni Registrar of Political Parties...lazima vyama vi-file in returns za mapato yao aidha toka kwenye michango,fadhila nk..hili sijalisikia Tanzania lakini kwingineko ipo..hata UK ilitoka zogo siku za nyuma juu ya finances za labour...15bn/- sio mzaha..wamwpata wapi?Ruzuku haifiki huko na sidhani wanachama wanalipa michango yao maana sijaona mkakati wa makamba.makalla & co(walaji not advocates) kufuatilia memebrs fees hata kwa speech
Safari,

Naona hizo ni pesa chafu na CCM watakuwa tu wamepewa na mafisadi. Ilitakiwa huko ndio CHADEMA wang'ang'anie badala ya kujikita kwenye data ambazo sio sahihi.

Tatizo wakianza kuulizia kila senti imetoka wapi, watajikuta na wenyewe kwenye matatizo hayo hayo, wakiulizwa pesa za kununulia helikopta wamezitoa wapi?

Vyama TZ vyote vinatumia pesa za matajiri kujiendeshe kitu ambacho ni makosa. Inatakiwa watumie pesa kutoka wanachama na wapenzi wao wadogo wadog.
 
Mkulima,
Ndio maana ufisadi hauishi kwa kuwa anayejaribu kuupigia kelele naye anajikuta yumo pia....bahati mbaya huyu msajili,CAG/NAO na NEC ni Vya kuteuliwa na executive kwa hiyo hawana independence...laiti wangekuwa chini ya bunge...
 
HAwezi kuwa rais labda 2015, urais ni zaidi ya mtu mmoja!! Hiyo CHADEMA itaunda serikali kwa potential figures zipi? Tuwe realistic sometimes... na tuache kumuonea Slaa, wacha aendelee kuwa mbunge kwani kule mchango wake ni muhimu sana

Potential figures? una maana ganai?? Hivi CCM zipi ni potential figures?? Je hizo potential figures zimetufikisha wapi?? Sasa kama akina Ghasia, Matayo, Nchimbi, Bendera, Mdhihiri, Mama Ntimizi, Mama Sitta, Megji n.k wameweza kuwa mawaziri iweje leo useme Chadema hawana watu. Hivi vichwa kama vyote vile Chadema unaona havifai. Tatizo mnaangalia Balaza la mawaziri 60. We do not need 60 ministers in a poor country like ours.A maximum of 20 Ministers can do the job.

Wala usifikiri eti selikali mpya ikiingia makatibu na wakurungenzi nao watabadilika.
 
Potential figures? una maana ganai?? Hivi CCM zipi ni potential figures?? Je hizo potential figures zimetufikisha wapi?? Sasa kama akina Ghasia, Matayo, Nchimbi, Bendera, Mdhihiri, Mama Ntimizi, Mama Sitta, Megji n.k wameweza kuwa mawaziri iweje leo useme Chadema hawana watu. Hivi vichwa kama vyote vile Chadema unaona havifai. Tatizo mnaangalia Balaza la mawaziri 60. We do not need 60 ministers in a poor country like ours.A maximum of 20 Ministers can do the job.

Wala usifikiri eti selikali mpya ikiingia makatibu na wakurungenzi nao watabadilika.

Mr. Ziro ulichokisema ni sahihi kabisa. Tukiamua tunaweza kuendesha nchi yetu kwa kuwa na wizara hata 15. Ni suala la kukaa chini na kupanga ipasavyo. Ni muhimu sana tukaheshimu uwezo wa Watanzania wenzetu ambao bahati mbaya hawajapata nafasi ya kulitumikia taifa letu katika ngazi ya kitaifa. Tuwape nafasi na tuwasaidie. Lazima tutafika.
 
Lunyungu,

Mpeni Dr. Slaa data za ukweli. Akikosea mara mbili au tatu kama alivyofanya kweli hili la magari, tayari mnakuwa mmewapa CCM ngao ya kummaliza. Kumbuka ya Mrema, alikuwa analipua mabomu ya kweli lakini baada ya muda CCM wakaanza kumpelekea data fake ili aumbuke na kuonekana mwongo.

Ni mategemeo yangu hatutaenda huko na Dr. Slaa. Hii habari sio siri Dr. Slaa ameongea kitu ambacho sio ukweli.
Mkulima,
Ukweli wa ukwepaji huu haujawekwa hadharani na ccm bado. Tutaendelea kuwakaba koo hadi ushuru wote utakapolipwa. Mbinu zote tumezikamata, hakika safari hii hawatapata mteremko kama ilivyokuwa wakati wa Meremeta, Deep Green. Sisi tunachotaka ni Ushuru na kodi zilipwe ili shule zijengwe, Zahanati zijengwe, Barabara zijengwe na wananchi wapate maji. Tumesema nchi hii imetafunwa ya kutosha na sasa inatosha. Ni vizuri wana JF muwe wachunguzi badala ya ushabiki hata kama ni mwana ccm damu damu. Ukosefu wa shule unawabana sawa sawa wajomba zako, wapwa zako walioko vijijini hata kama wewe unanufaika kwa kiwango chochote kile kile.

Mama na dada zako wanatembea kilomita na kilomita kusaka maji na maajabu yanatokea kwenye msako huo na hakuna anayeyazungumzia. Ni swala la dhamira tu. Ushabiki tu hauwezi kulikomboa Taifa hili. Tunataka Ushuru wote na kodi zote zilipwe. Full stop. Siku zimelipwa zote tutanyamaza lakini vinginevyo niliisha kuwapa ruksa waende mahakamani. Hapo ndio data zote zitamwagwa mpaka ushuru wa Mahindra uliokwepwa mwaka 2005, baiskeli nazo pikipiki.

Mashabiki wanaweza kufikiri ni mchezo, lakini wako bado watanzania wenye dhamira!!! na Nchi hii itaendelea kutetewa kikamilifu ccm hawawezi kukaa tena kwa amani
 
Mkulima,
Ukweli wa ukwepaji huu haujawekwa hadharani na ccm bado. Tutaendelea kuwakaba koo hadi ushuru wote utakapolipwa. Mbinu zote tumezikamata, hakika safari hii hawatapata mteremko kama ilivyokuwa wakati wa Meremeta, Deep Green. Sisi tunachotaka ni Ushuru na kodi zilipwe ili shule zijengwe, Zahanati zijengwe, Barabara zijengwe na wananchi wapate maji. Tumesema nchi hii imetafunwa ya kutosha na sasa inatosha. Ni vizuri wana JF muwe wachunguzi badala ya ushabiki hata kama ni mwana ccm damu damu. Ukosefu wa shule unawabana sawa sawa wajomba zako, wapwa zako walioko vijijini hata kama wewe unanufaika kwa kiwango chochote kile kile.

Mama na dada zako wanatembea kilomita na kilomita kusaka maji na maajabu yanatokea kwenye msako huo na hakuna anayeyazungumzia. Ni swala la dhamira tu. Ushabiki tu hauwezi kulikomboa Taifa hili. Tunataka Ushuru wote na kodi zote zilipwe. Full stop. Siku zimelipwa zote tutanyamaza lakini vinginevyo niliisha kuwapa ruksa waende mahakamani. Hapo ndio data zote zitamwagwa mpaka ushuru wa Mahindra uliokwepwa mwaka 2005, baiskeli nazo pikipiki.

Mashabiki wanaweza kufikiri ni mchezo, lakini wako bado watanzania wenye dhamira!!! na Nchi hii itaendelea kutetewa kikamilifu ccm hawawezi kukaa tena kwa amani

MUNGU azidi kuwalinda. Naamini mtafanikiwa katika azma yenu njema na kwa faida ya Wana-CCM pia.
 
yako wapi hayo maelezo?

CCM NA MAGARI YA UCHAGUZI


"""" Mkulima,
Ukweli wa ukwepaji huu haujawekwa hadharani na ccm bado. Tutaendelea kuwakaba koo hadi ushuru wote utakapolipwa. Mbinu zote tumezikamata, hakika safari hii hawatapata mteremko kama ilivyokuwa wakati wa Meremeta, Deep Green. Sisi tunachotaka ni Ushuru na kodi zilipwe ili shule zijengwe, Zahanati zijengwe, Barabara zijengwe na wananchi wapate maji. Tumesema nchi hii imetafunwa ya kutosha na sasa inatosha. Ni vizuri wana JF muwe wachunguzi badala ya ushabiki hata kama ni mwana ccm damu damu. Ukosefu wa shule unawabana sawa sawa wajomba zako, wapwa zako walioko vijijini hata kama wewe unanufaika kwa kiwango chochote kile kile. Mama na dada zako wanatembea kilomita na kilomita kusaka maji na maajabu yanatokea kwenye msako huo na hakuna anayeyazungumzia. Ni swala la dhamira tu. Ushabiki tu hauwezi kulikomboa Taifa hili. Tunataka Ushuru wote na kodi zote zilipwe. Full stop. Siku zimelipwa zote tutanyamaza lakini vinginevyo niliisha kuwapa ruksa waende mahakamani. Hapo ndio data zote zitamwagwa mpaka ushuru wa Mahindra uliokwepwa mwaka 2005, baiskeli nazo pikipiki. Mashabiki wanaweza kufikiri ni mchezo, lakini wako bado watanzania wenye dhamira!!! na Nchi hii itaendelea kutetewa kikamilifu ccm hawawezi kukaa tena kwa amani.""""

MTM,

Hayo ndiyo maelezo ya Dr. Slaa kama yanavyojieleza hapo juu. Yanapatikana kwa sasa kwenye ukurasa wa mwisho wa THREAD ya "CCM NA MAGARI YA UCHAGUZI" katika jukwaa hili la siasa.
 
Sabi,

nashukuru umetuma huu ujumbe na kwa kweli Dr. Slaa anaonyesha tena dhamira ya kweli!! Namuombea tu wasimuue
 
Twendeni taratibu lakini kwa makini kabisa kama vile paka amendeapo kumkamata panya! Mwisho wa siku tutakuwa tumepunguza myanya ya fedha za walipa kodi kutumiwa hovyo hovyo na wasio wazalendo. Kama Dr. Slaa asingelisema hili, bila shaka kodi ya magari yaliyonunuliwa na ccm isingelipwa kabisa. Pale tunapoona matumizi au ubadhilifu wowote wa fedha za walipa kodi ama kufanywa na ccm au chama chochote cha siasa tuwe tayari kuuambia umma haraka iwezekanavyo kabla ya kuchelewa ili kuwakamata shingoni na kuweza kujirekebisha.

Nafikiri tuko pamoja katika vita hii ya kuwapigania watanzania wote! Tunahitaji akina Dr. Slaa wengi tu hata kutoka ccm kwenyewe!
 
CCM yatumia Sh10b kununua magari


  • YASEMA MECHI BILA MAZOEZI HAKUNA USHINDI, YASISITIZA KULIPA KODI
Mwandishi Wetu
Date:12/29/2009

IMEBAINIKA kwamba CCM imetumia takriban Sh70 milioni kununua gari moja kati ya magari 150 aina ya Land Cruiser Hardbody yaliyoagizwa kwa ajili ya kufanikisha mradi wa kuimarisha chama" hicho, lakini bei halisi ya magari hayo ni zaidi ya Sh107 milioni.

Uchunguzi wa Mwananchi unaonyesha kuwa CCM itatumia zaidi ya Sh10 bilioni kununua magari yote 150 ambayo yatasambazwa kwenye wilaya zote nchini kufanikisha shughuli za kisiasa za chama hicho tawala.

Taarifa za kuingizwa kwa magari hayo zilifichuliwa na katibu mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa wakati alipoituhumu CCM kuwa imeingiza magari 200 na kukwepa ushuru wa takribani Sh600 milioni.

Dk Slaa alitoa tuhuma hizo wakati akihutubia kwenye moja ya mikutano ya Operesheni Sangara mkoani Tanga, lakini CCM ikamkosoa kuwa idadi ya magari iliyoagiza ni 150 na kwamba kiwango cha ushuru ni kikubwa zaidi ya alichokitaja.

Lakini tofauti hiyo ya bei halisi ya magari hayo na kiasi cha fedha kilichotajwa na CCM kuwa kimetumika kugharamia ununuzi wa magari na ushuru, kinaweka maswali kuhusu ukweli wa sakata hilo.

CCM imeeleza kuwa imeshaingiza magari 74 kutoka Japan wakati mengine 76 yapo bandarini yakisubiri kukamilika kwa taratibu za kulipia ushuru ili yatolewe wakati wowote kuanzia leo.

Uchunguzi wa Mwananchi unaonyesha kuwa CCM pamoja na kulipa ushuru imenunua gari moja kwa Sh70,451,619.7. Lakini taarifa kutoka kampuni inayouza magari hayo hapa nchini (Toyota Tanzania Limited) zinaonyesha kuwa gari moja la aina hiyo pamoja na kulipia ushuru linauzwa kwa Sh107,813,905, ikiwa ni tofauti ya Sh37,362,285.3.

Katibu wa masuala ya uchumi na fedha wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), Amos Makalla alibainisha wakati akiongea na waandishi wa habari kuwa chama hicho kimetumia Sh3,493,354,830 kununua magari hayo na imetumia Sh1,720,065,031 kulipia ushuru.

"Kwa magari hayo 74, tumelipa Sh3,493,354,830, sasa kama wewe ni mwanamahesabu mzuri jumlisha na ushuru tuliolipa wa Sh1,720,065,031 utajua gharama zote," alisema Makalla, ambaye alikuwa kiongozi wa tatu kutoa ufafanuzi wa tuhuma za Dk Slaa baada ya kutanguliwa na katibu wake mkuu, Yusuf Makamba na katibu wa itifaki wa Nec, John Chiligati.

"Ukitaka kujua bei ya gari moja aina ya Toyota Landcruiser Hardbody tuliyonunua, chukua kiasi hicho gawanya kwa 74."

Kwa maana hiyo, jumla ya fedha zilizotumika kununua na kuingiza magari hayo ni Sh5,213,419,861, ambayo ukiigawanya kwa 74 unapata Sh107,813,905, ambazo zilitumika kununulia gari moja kati ya hayo 150.

Kwa maana nyingine, gharama za magari 76 yaliyo bandarini zinakadiriwa kufikia Sh5,354,323,100.5 bilioni zikujumuishwa na ushuru wa Sh1,766,553,275.1 bilioni unaotarajiwa kulipwa kwa ajili hiyo.

Lakini utafiti uliofanywa Toyota Tanzania Limited, ambayo ni wakala wa magari hayo nchini unaonyesha kuwa bei ya sasa ya gari aina ya Toyota Landcruiser Hardbody ni Sh107 milioni baada ya kulipiwa ushuru na kukamilisha taratibu nyingine.

Kiwango hicho kinafanya tofauti ya bei iliyotumiwa na CCM na ile ya kampuni ya Toyota ni takribani Sh33 milioni. Makalla hakupatikana baadaye jana kutoa ufafanuzi kama magari waliyoagiza ni mtumba au ni mapya. Pia wakala aliyeagizia magari CCM hakuweza kupatikana jana.

Mwaka 2005, CCM pia iliagiza shehena ya magari aina ya Mahindra ambayo pia yaliamsha tuhuma kuwa chama hicho tawala kilikwepa kodi wakati wa kuyaingiza.

Makala alithibitisha kuwa magari mengine 76 yataanza kutolewa bandarini muda wowote kuanzia leo, pindi TRA itakapokamilisha taratibu na nyaraka husika zitakazoiwezesha CCM kulipia ushuru.

"Tumeyaleta (haya magari) kwa ajili ya mradi wa kuimarisha chama, lakini zitasaidia pia uchaguzi wa 2010. Tunalenga kuwafikia wananchi wote hata vijijini, tunafanya siasa ambayo bila usafiri haiwezekani, lakini kwa kuwa uchaguzi ni mwakani, tunafanya mazoezi kwani mechi bila mazoezi huwezi kushinda. Sasa tunapiga jalamba," alisema Makalla.

Tangu Dk Slaa amwage hadharani mpango huo, viongozi tofauti wa CCM wamejaribu kutoa ufafanuzi, akiwemo Chiligati ambaye alisema kwa kifupi tu kuwa chama hicho ni kikubwa hivyo suala la kununua magari hayo si la ajabu.

Makamba alifafanua makombora ya Dk Slaa kwa kueleza kuwa alikosea katika idadi ya magari yaliyoagizwa na CCM na kutaja kuwa ni 150 na ndipo Makalla alipoanza kutoa ufafanuzi kwa kuonyesha waandishi nakala za nyaraka za kuagizia magari hayo na risiti za benki za kulipia ushuru. Kuhusu mkakati wa wanaCCM kukichangia chama hicho fedha ili kijitegemee, Makalla alisema wanachama wameitikia wito huo na wengi wameonyesha nia ya kuchangia, lakini akasema baada ya vikao vikuu vya CCM Januari na Februari mwaka 2010 watazindua kampeni hizo za kuchangisha fedha.
 
Back
Top Bottom