logician mkuu
JF-Expert Member
- Jun 2, 2014
- 792
- 221
Msituchanganye bana. Mnyika alisema kuwa ataleta maji Ubungo. Wala hakusema kuwa ataishirikisha serikali ya CCM kutekeleza hilo. Kama kazi imewashinda rudisheni majimbo kwa CCM
Waulize hao Wabunge wako fedha wanazopewa za mfuko wa Jimbo wanazitumiaje
mwambieni mnyika tunataka maji ubungo alisema ndani ya mwezi mmoja akichaguliwa ataleta maji ubungo yako wapi sasa hayo maji aliyosema mnyika.
Pesa za maji zipo, tena zipo nyingi tu, zilizotolewa na wafadhili na za ndani. Uzembe na ufisadi wa serikali ya CCM ndio unakwamisha. Mnyika anafuatilia na anafanya lile analopaswa kufanya kama mbunge.kwani kwa mawazo yako pesa ya mfuko wa jimbo inafanya kazi gani.
Tutaanza kufichua mabilioni yaliyotengwa kwa ajili ya maji yanavyotumika vibaya.
Kwanza kuna pesa za MCA (Milennium Challenge AccounT) kama ambavyo mradi unajieleza kwenye website ya serikali.
Hizi ilipewa wizara ya fedha moja kwa moja. Je, Mnyika atafute nyingine na kuanza project mpya?
Alipopelekwa hoja yake binafsi ya kufuatilia mradi huu, Waziri alimzima, wote tunakumbuka.
Waziri mwenyewe alituambia kuwa kuna fedha hii kwenye bajeti ya 2012/13 Namnukuu hapa
Watanzania tumekuwa wajinga. Mahali ambapo uzembe uko wazi tu, tunaleta siasa eti kuadhibu upinzani.Serikali yatenga mabilioni kugharimia maji.
WIZARA ya Maji jana iliwasilisha makadirio yake ya matumizi kwa mwaka 20012/2013 bungeni ambayo yanaonyesha kuwa imetenga Sh465.756 bilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.Akiwasilisha bajeti hiyo, Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe alisema kati ya fedha hizo, Sh140.015 bilioni ni za ndani na Sh325.740 ni fedha kutoka nje.
Profesa Maghembe alisema kwa ujumla wake, wizara yake inakusudia kutumia Sh485.898 bilioni, kati ya hizo matumizi ya kawaida ni Sh20.142 bilioni.
Alisema miongoni mwa kazi ambazo wizara hiyo imepanga kuzitekeleza ni pamoja na maeneo yanayofaa kuchimba visima virefu na kusimamia uchimbaji kwa maeneo 630 katika sehemu mbalimbali nchini.
"Mwaka 2012/2013, kupitia Bajeti ya Serikali, Sh51.9 bilioni kutoka mfuko wa pamoja zimepangwa kugharimia ujenzi wa miundombinu ya maji, kujenga uwezo wa watekelezaji wa programu, uhamasishaji, kutoa elimu ya usafi na mazingira, ufuatiliaji na kulipa wataalamu washauri kwa ajili ya usimamizi wa makandarasi," alisema Profesa Maghembe na kuongeza:
"Kiwango hicho cha fedha kilichotengwa ni sehemu ya Sh81.8 bilioni ya mchango wa Serikali na ahadi ya Washirika wa Maendeleo."
Alisema Serikali inaendelea kutekeleza Mpango wa Dharura wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Jiji la Dar es Salaam na Miji ya Kibaha na Bagamoyo ambao unalenga kuongeza uwezo wa uzalishaji wa maji kutoka mita za ujazo 300,000 kwa siku hadi mita za ujazo 710,000 siku ifikapo 2014.
Profesa Maghembe alisema mpango huo unatekelezwa kwa ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Serikali ya Norway, Serikali ya India na washirika wengine wa maendeleo kupitia Mfuko wa Pamoja wa Maji.
"Utekelezaji wa Mpango huo ulianza rasmi Februari 2011 na umepangwa kukamilika Desemba 2014 na utagharimu Sh653.9 bilioni," alisema Profesa Maghembe.
Mimi ntaanza kulikuza hili, nahisi kuna uchafu kama wa EPA na ESCROW.
Kwa nini Maghembe alizima hoja binafsi ya Mnyika?
Kwa nini team Lumumba inaitumia hii kama propaganda ya kumchafua Mnyika?
Tatizo si kuwa pesa hakuna, tatizo zimetumikaje?
Baada ya Escrow mnaonaje tulikuze hili limtikise Maghembe?
Ukweli ni kwamba Mnyika anachukiwa na CCM kwa jinsi anavyohoji mambo bungeni!!