KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Huko kwenye ma-group ndiko iliko CCM?Niko katika group nyingi za chama za WatsApp na mitandao miingine, yaani ni kimya hata kama kuna tukio litatokea hatutaarifiani. Hii ni kwamba hawakubaliani na Mamlaka iliyopo au wanataka nini? Mzee keshaondoka na mema yake kaacha tumalizie alikoachia acheni chuki tutakigawa chama.
Ma'group" ya walaji ndiyo unaiita CCM?
CCM chini ya Magufuli ilikuwa ni hiyo aliyokuwa ameishikilia Magufuli mwenyewe kama silaha yake ya kuwapigia anaowaona kama wanampinga.
Wewe hukuona alivyowapiga na kuwapondaponda kabisa wale wazee "Makatibu wastaafu", na wengine wote alioona kuwa nitishio kwake?
Nyinyi wa kwenye hayo ma'group' yenu mlikuwa mnakula toka mikononi mwake. Sasa hayupo, unataka muwe na furaha huku njaa imewajaa tumboni?
CCM kwa sasa hivi inaeleaelea tu, haijulikani mwenyewe ni nani.
Huyu mama bado wanamsoma na kumhesabia sabini zake. Akizubaa tu, "Analiwa".
CCM ni mzoga, roho yake inayumbayumba haijui iingie kiwiliwili gani kati ya vilivyopo sasa.