CCM kutumia Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi, Inajua Ikishindwa Ndio Itakufa Jumla, Itakubali?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,558
113,751
Wanabodi,

Baada ya vyama vya upinzani kupata ushindi wa matumaini na CCM kuporwa mitaa na vijiji kadhaa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kumefufua matumaini ya uwezekano wa CCM kushindwa jumla katika uchaguzi mkuu ujao, hivyo kuweka possibility ya CCM kuwa ni chama cha upinzani Tanzania ama baada ya 2015 au 2020!.

Wengi tunajua kuwa CCM huwa inashinda chaguzi mbalimbali, sio tuu kwa sababu inapendwa, au imewatendea mema Watanzania, bali katika baadhi ya maeneo CCM inapendwa mpaka basi, huku baadhi ya maeneo imechokwa!, ila bado huwa inashinda kwa mbinu mbali, ambazo some ni hooks & crooks!, kunakopelekea wengi wa wapiga kura kujikuta, hata wafanye nini, CCM ni lazima tuu itashinda!, hali iliyopelekea watu kujikatia tamaa na any possibility ya CCM kushindwa, hivyo kuamua kuliko kupoteza muda wao kupiga kura, bora wajilalie tuu majumbani mwao, ndio maana tumeshuhudia watu milioni 22 wakijiandikisha, kisha ni watu milioni 8 tuu wakijitokeza!, hivyo msindi wa urais kushinda kwa kura milioni 5 tuu, ambayo ni asilimia 9% tuu ya watu milioni 45!.

Pia kuna maeneo CCM imechokwa ila bado inaendelea kushinda kwa mazoea tuu, watu hawana elimu ya uraia ya kutosha, hivyo kuamini kuwa chama kinachopaswa kuongoza Tanzania milele ni Chama cha Mapinduzi CCM!.

Kwa vile CCM imezoea kushinda kwa mbinu, kuna mwanajf alisema humu, kuwa hufikia wakati, hata "the greatest magicians runs out of tricks!" hivyo CCM waliishiwa mbinu, wakashindwa huko walikoshindwa!.

Wengi wanajipa matumaini kuwa kushindwa huko, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM!, lakini inawezakana pia isiwe hivyo, inawezekana sasa ni faru amejeruhiwa!, faru ni mnyama mpole sana, ila akijeruhiwa, atakuwa ni myama wa hatari sana, huisimamisha ile pembe yake na kukimbia hovyo chochote atakachokutana nacho mbele yake, anatoboa na pembe hiyo!.

Hivyyo kuna uwezekano sasa CCM ikaja na mbinu mpya za faru aliyejeruhiwa hivyo uchaguzi wa 2015 ikakomba kila kilicho mbele yake!, jee unajua ni kwa nini, CCM lazima ilazimishe kushinda ili kubakia madarakani?!.

Nimekuwa inspired kuandika uzi huu na thread ya mwana jf huyu

Baada ya kushinda vijiji vingi katika jimbo la Moshi vijijini changamoto mpya imezuka. Majengo mengi ambayo ofisi za vijiji zipo ni ofisi pia za CCM.

Katika vijiji vya Okaseni na Kimanganuni ofisi za vijiji zilijengwa wakati wa chama kimoja, na kwa kuwa CCM ndo walikuwa viongozi wa serikali za mtaa hii haiukuwa changamoo.

Sasa hatujui itakuwaje kwa kuwa CHADEMA nao wamepandisha bendera zao kwenye haya majengo, hivyo CCM sasa hawana tena ofisi katika vijiji hivi ambayo wameichagua CHADEMA 100%.

Sipati picha bendera za Chadema kwenye majengo ya CCM!.

Wakati wa chama kimoja, CCM ilichangiwa kwa lazima na wafanyakazi wote!, ile siku tunaanza vyama vingi, kiuhaki na kiuhalali, ilibidi mali zote CCM iliyomiliki kwa michango ya lazima, zilipaswa kurudishwa serikali, zikiwemo zile mali CCM iliyozivuna kama chama dola, mfano uwanja wa CCM, Kirumba, ukumbi wa CCM, Kizota, Jengo la Makao Makuu ya CCM, Dodoma, Jengo la Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba, na mali zote za jumuiya za CCM, likiwemo jengo la Umoja wa Vijana, lile jengo la Airtel etc, yalipaswa kurudishwa serikalini, yaani kutaifishwa kuwa mali ya umma!.

Kitendo cha CCM kuendelea kuzishikilia hizo mali, ni wizi, ujambazi na uharamia kwa jasho la Watanzania!. Nilishauri, kama kweli itakuja kufika siku, CCM ikawa ni chama cha upinzani, huo ndio utakuwa mwisho wa CCM, milele, maana kazi ya kwanza ya chama kingine kikitawala, itakuwa ni kuipoka, na kuipurura CCM, malizo zote ilizojitwalia kwa uporaji (looting), na kuzigeuza ni mali ya umma!.

CCM ikiishaporwa kila kitu!, kamwe haiwezi kuamka tena!, that will be the end of it jumla, ndio maana kwenye chaguzi mbali mbali CCM does all it can to remain in power, maana naamini hili CCM hili wanalijua, hivyo nawaombeni sana msiendelee kuishangaa CCM inapotumia all the means, by hooks and crooks to remain in power, ni pamoja the fear of unknown!, on what will happen, if CCM looses, ndio maana mnaona hakuna any preparations kwa serikali na vyombo vya dola, kuitumikia serikali ya chama kingine!.

Kama ilivyo kanuni ya the law of the jungle ni "struggle for existence, survival for the fittest", bila kujali ni mbinu gani zitatumika kushinda uchaguzi, kwa sababu mwisho wa siku, uhalali wa mshindi, unapatikana kwa "the end, justify the means!", "The winner takes it all!, the looser standing small!.

Mnaondani kuwa baada ya kipigo hiki cha serikali za mitaa, CCM will just sit and watch!, they might be wrong!.

Tangu tuanze mfumo wa vyama vingi, kuna baadhi ya maeneo ambayo watu wake wanajitambua, yamekuwa yakiwachagua wapinzani, maeneo hayo ni pamoja na jimbo la Moshi mjini, Arusha Mjini na Jimbo la Kigoma Mjini, tangu kuasisiwa kwa mfumo wa vyama vingi, majimbo haya yamekuwa ni chachu ya upinzani, hivyo huku ndiko CCM itaweka concentration kubwa ya mbinu na crooks kwasababu kutumia hooks kwa watu wanaojitambua, hakuwezi kuzaa matunda. Hivyo majimbo stronghold za upinzani jiandaeni kivita kuzuia hizo crooks vinginevyo majimbo haya yatarejeshwa CCM.

Namalizia kwa swali, kama CCM imekuwa ikitumia mbinu za Hooks & Crooks kushinda chaguzi mbali mbali, ili kuhakikisha inabakia madarakani, kwa sababu inajua ikishindwa, ndio itakufa jumla, jee unadhani CCM itakubali kujikalia na kujiangalia tuu huku ikijifia kibudu, au itaendelea kutawala hadi milele na milele ?.

Jumapili Njema,

Pasco.
 
Asante Pasco kwa kuketa uzi. Nini kifanyike, tunaliomba jeshi la wananchi lijiandae kusimamia haki na sio kusuburi kupewa amri na ccm. Nasema hivyo kwani jeshi la polisi limepoteza uhalali wa kusimamia haki bali limejigeuza ni tawi ama jumuiya ya ccm. Na hili linatokea kwani jeshi la polisi kwa kushirikiana na ccm wamekuwa wala rushwa wakubwa hivyo wana kanuni ya nifae kwa jua nami nikufae kwa mvua. Niwatake na viongozi wa dini sasa ni wakati wa kuhakikisha wanalitendea haki taifa hili. Hao viongozi wa ccm wakiwataka waliombee taifa amani wawaulize nini sababu ya kutoweka amani? Najua hawana jibu zaidi ya propaganda za kizamani. Hivyo wawaambie waache demokrasia ya kura itawale vinginevyo umma utachukua hatua. Nadhani kila mmoja anajua nini kitatokea iwapo umma utaamua. Vijana sasa ni wakati wetu kusimama tayari kwa kulitetea taifa letu linaloporwa na kikundi cha wahuni.
 
Pasco, thread yako inafikirisha na kuogopesha.Nchi hii itaingia kwenye wakati mgumu sana pale ccm watakapoona wazi kabisa kwamba mwisho wao unakaribia.Na huo wakati ni sasa, uchaguzi wa serikali za mitaa.Tumeona jinsi ccm inavyotumia nguvu kubadili matokeo pale inaposhindwa uchaguzi na kuvuruga amani kwa kutumia jeshi la polisi.
Tuwaombe viongozi wote wa vyama vya upinzani UKAWA et al wakutane wajadili hali hii hatari ya ccm kutumia nguvu za jeshi kuzima/kuzuia ushindi wa vyama vya upinzani.

Baada ya majadiliano hayo, na kuweka wazi jinsi nchi hii itakavyoingia kwenye machafuko, viongozi hawa wawageukie viongozi wa dini kuwaomba walitazame swala la amani ya nchi kwa mkabala tofauti, kwamba amani ya nchi inachafuliwa na chama tawala -ccm.Kisha viongozi wa dini wawaombe viongozi wa ccm wawe na subira/uvumilivu kwenye chaguzi.
Ni jambo gumu kwa viongozi wa dini kulitekeleza lakini kama kweli wana nia ya kuliombea amani taifa hili watajikaza wafanye hivyo.
Scenario ninazoziwazia kwenye uchaguzi mkuu 2015 zinanipa wasiwasi mkubwa na hata wewe unayesoma post hii una picha ya kitakachotokea oktoba 2015 pale ccm itakapokosa mgombea ubunge kwenye jimbo fulani ambapo wamejitokeza wagombea kadhaa wa upinzani waliopitishwa na kukubalika na vyama vyao.

CCM kwa kukaa madarakani muda mrefu kimejijengea kiburi hatari kinachokigeuza chama kuwa cha kihuni na kufanana sana na kikundi cha Robin Hood.
 
Last edited by a moderator:
ccm kwa sasa ni genge la wahuni wanaotaka kuhakikishakuwa wanatawala bila kibali cha wananchi kwani wanajua kuwa bila kutawala genge lao litasambalatika kwani wote walimo humo wamo kwa ajili ya maslahi ndiyo maana wakaandika katiba itakayo wahakikishia ulaji na kuwanyima wananchi uwezo wa kuwadhibiti viongozi wahuni,
 
Umenena vyema, watakao sababisha vurugu ni ccm pale watakapoona matokea yamekuwa tofauti na matarajio yao 2015.Unajua sikio la kufa huwa halisikii dawa,mpaka sasa wana amini watatawala milele acha watupige kwa mabomu na wao pia muda utafika watapigwa tu.
 
I'm proud leo umekuja na uzi makini wenye maslahi mapana ya nchi yetu! Baada ya muda mrefu sana hatimae leo umeonekana ki-ILBORIAN zaidi!!! Products za Bino et al huwa zinavionjo vya Uzalendo!!! all in all uzi huu unamashiko kuanzia kwa UKAWA hadi wananchi wa Kawaida...Ukwli ndo huo kuwa CCM wanalinda maslahi yao Zaidi ya Kuwatumikia wananchi!!! Threat kubwa kwao ni kunyang'anywa mali za Watanzania, wanajua kuwa ndo itakuwa mwisho wao kutawala!! Hata hivyo CCM inakingiwa kifua na MNCs zinazokwapua Utajiri wetu!!! Mbowe aliwahi kuhojiwa kwenye Mkutano wa Mabeberu kuwa CDM ikichukua nchi watafuta Mikataba? Ilibidi wajieleze kwa umakini sana...

Wanabodi,

Baada ya vyama vya upinzani kupata ushindi wa matumaini na CCM kuporwa mitaa na vijiji kadhaa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kumefufua matumaini ya uwezekano wa CCM kushindwa jumla katika uchaguzi mkuu ujao, hivyo kuweka possibility ya CCM kuwa ni chama cha upinzani Tanzania ama baada ya 2015 au 2020!.

Wengi tunajua kuwa CCM huwa inashinda chaguzi mbalimbali, sio tuu kwa sababu inapendwa, au imewatendea wema Watanzania, bali CCM kiukweli CCM imechokwa!, ila bado huwa inashinda kwa mbinu mbali, ambazo some ni hooks & crooks!, kunakopelekea wengi wa wapiga kura kujikuta, hata wafanye nini, CCM ni lazima tuu itashinda!, hali iliyopelekea watu kujikatia tamaa na any possibility ya CCM kushindwa, hivyo kuamua kuliko kupoteza muda wao kupiga kura, bora wajilalie tuu majumbani mwao, ndio maana tumeshuhudia watu milioni 22 wakijiandikisha, kisha ni watu milioni 8 tuu wakijitokeza!, hivyo msindi wa urais kushinda kwa kura milioni 5 tuu, ambayo ni asilimia 9% tuu ya watu milioni 45!.

Pia kuna maeneo CCM imechokwa ila bado inaendelea kushinda kwa mazoea tuu, watu hawana elimu ya uraia ya kutosha, hivyo kuamini kuwa chama kinachopaswa kuongoza Tanzania milele ni Chama cha Mapinduzi CCM!.

Kwa vile CCM imezoe kushinda kwa mbinu, kuna mwanajf alisema humu, kuwa hufikia wakati, hata "the greatest magicians runs out of tricks!" hivyo CCM waliishiwa mbinu, wakashindwa huko walikoshindwa!.

Wengi wanajipa matumaini kuwa kushindwa huko, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM!, lakini inawezakana pia isiwe hivyo, inawezekana sasa ni faru amejeruhiwa!, faru ni mnyama mpole sana, ila akijeruhiwa, atakuwa ni myama wa hatari sana, huisimamisha ile pembe yake na kukimbia hovyo chochote atakachokutana nachoto mbele yake, anatoboa na pembe hiyo!.

Hivyyo kuna uwezekano sasa CCM ikaja na mbinu mpya za faru aliyejeruhiwa hivyo uchaguzi wa 2015 ikakomba kila kilicho mbele yake!, jee unajua ni kwa nini, CCM lazima ilazimishe kubakia madarakani?!.

Nimekuwa inspired kuandika uzi huu na thread ya mwana jf huyu


Sipati picha bendera za Chadema kwenye majengo ya CCM!.

Wakati wa chama kimoja, CCM ilichangiwa kwa lazima na wafanyakazi wote!, ile siku tunaanza vyama vingi, kiuhaki na kiuhalali, ilibidi mali zote CCM iliyomiliki kwa michango ya lazima, zilipaswa kurudishwa serikali, zikiwemo zile mali CCM iliyozivuna kama chama dola, mfano uwanja wa CCM, Kirumba, ukumbi wa CCM, Kizota, Jengo la Makao Makuu ya CCM, Dodoma, Jengo la Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba, na mali zote za jumuiya za CCM, likiwemo jengo la Umoja wa Vijana, lile jengo la Airtel etc, yalipaswa kurudishwa serikalini, yaani kutaifishwa kuwa mali ya umma!.

Kitendo cha CCM kuendelea kuzishikilia hizo mali, ni wizi, ujambazi na uharamia kwa jasho la Watanzania!. Nilishauri, kama kweli itakuja kufika siku, CCM ikawa ni chama cha upinzani, huo ndio utakuwa mwisho wa CCM, milele, maana kazi ya kwanza ya chama kingine kikitawala, itakuwa ni kuipoka, na kuipurura CCM, malizo zote ilizojitwalia kwa uporaji (looting), na kuzigeuza ni mali ya umma!.

CCM ikiishaporwa kila kitu!, kamwe haiwezi kuamka tena!, that will be the end of it jumla, ndio maana kwenye chaguzi mbali mbali CCM does all it can to remain in power, maana naming CCM hili wanalijua, hivyo nawaombeni sana msiendelee kuishangaa CCM inapotumia all the means, by hooks and crooks to remain in power, ni pamoja the fear of unknown!, on what will happen, if CCM looses, ndio maana mnaona hakuna any preparations kwa serikali na vyombo vya dola, kuitumikia serikali ya chama kingine!.

Kama ilivyo kanuni ya the law of the jungle ni "struggle for existence, survival for the fittest", bila kujali ni mbinu gani zitatumika kushinda uchaguzi, kwa sababu mwisho wa siku, uhalali wa mshindi, unapatikana kwa "the end, justify the means!", "The winner takes it all!, the looser standing small!.

Mnaondani kuwa baada ya kipigo hiki cha serikali za mitaa, CCM will just sit and watch!, they might be wrong!.

Namalizia kwa swali, kama CCM imekuwa ikitumia mbinu za Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi mbali mbali, ili kuhakikisha inabakia madarakani, kwa sababu inajua ikishindwa, ndio itakufa jumla, jee unadhani CCM itakubali kujikalia na kujiangalia tuu huku ikijifia kibudu, au itaendelea kufurukuta mpaka itakapo kata roho?!.

Jumapili Njema,

Pasco.
 
Kikubwa kifanyike kilichofanyika temeke 1995 uchaguzi wa marudio temeke Mrema vs Sisco mtiti ulikua mkali sijawahi ona kampeni kama zile na kujitokeza upinzani kama ule hapa dsm na tanzania kwa ujumla . Nchi yote ilihamia temeke serekali ilikua temeke kila waziri alifika temeke .Mrema alikuwa na nccr ya kina marando lamwai selasini na mbatia, Makongoro nyerere, ndimara bob makani we acha bhana. Ukitaka kuidhibit ccm ni lazima uwashinde kwa mbaaaaali kama ilivokuwa temeke. watu walikesha kituo cha kuhesabia kura uwanja wa taifa kulikuwa na wakeshaji zaidi ya 9000 utafikiri kuna mechi usiku huo chama kinachoweza kudili nao ni CUF ingawa nao wamelainika kipindi hiki.
 
Pasco umeandika vyema, nionavyo mimi CCM hawana namna ya kubaki madarakani kwani mbinu zao zote zimekwishafahamika. Mbaya zaidi elimu ya uraia inazidi kukua kwa watanzania na hivyo kudanganyika kama zamani hicho kitu hakipo / kinapungua kila kukicha.
Ni mbinu 2 tu ambazo CCM imebaki nazo. Moja ilitumiwa 2005 na ikazaa matunda lakini sasa chini ya UKAWA mbinu hiyo inakosa target. Pia mbinu ya pili ni ile iliyotumika kibaha 2010, nayo pia inazidi kukosa mashiko jinsi elimu ya uraia inavyoongezeka. (Sijaziweka wazi kwa makusudi maalumu).
Kupitia uzoefu nilioupata uchaguzi wa serikali za mitaa nikiwa Vingunguti (ambapo CUF ilikomba kila kitu pamoja na kuahirishwa uchaguzi huo), pia kupitia uchaguzi 2010 nikiwa wilaya moja ambapo CCM walifakikiwa kupora ushindi wa CDM siku ya 4 toka kura kupigwa lakini baada ya DED kuzimia mara kadhaa kwa kulazimishwa apindue matokeo.
Hivyo mbinu zote ziko wazi na nitakapopata wasaghaa nitawapakulia UKAWA ili wajue namna ya kudhibiti mbinu hizo. Nitawapakulia kwa kuwa napenda maendeleo kuliko vyama, kwani vyama ni madaraja tu ya kuelekea tanzania tuitakayo.
 
Pasco!Ninakuhakikishia CCM ina kila dalili za ku expire!Ukiona chama chenye dola kama CCM kinaanza kutumia mahakama kusigina haki za raia unapata tafsri moja tu!Nayo ni kwamba,Mahakama ikishindwa maana yake CCM itakuwa imebakiza silaha moja tu!,KUUA WATU!Tukifika hapo ndio itakuwa mwisho wa CCM maana nchi itageuka Egypt.Mimi si Yahya Husein lakini haya mambo yatatokea ndani ya miaka 10 ijayo.
 
wasiwasi huu wa Tawala kuchukua sheria mkononi ili iendelee kuwepo...hauwezi tena kutisha raia wa Tanzania kuchukua uamuzi wa kurudisha madaraka mikononi mwao. They are ready for it, after all, they have nothing to loose.
 
Wazee fulani pale moshi waliwahi kisema uchaguzi wa 2010 kama mzee slaa akishindwa watajiua sijui ilikuwaje wakashindwa kujitia visu shingoni baada ya mzee slaa kushindwa,hali kama hii inaweza kuwakuta wanachadema wachache ambao wanadhani uchaguzi mkuu ujao watashinda lakini ukweli ni kwamba watagongwa sana tu tena kwa mbali sana.
 
wasiwasi huu wa Tawala kuchukua sheria mkononi ili iendelee kuwepo...hauwezi tena kutisha raia wa Tanzania kuchukua uamuzi wa kurudisha madaraka mikononi mwao. They are ready for it, after all, they have nothing to loose.
Hakuna nchi ambayo inaongozwa kwa bangi kama unavyodhani watanzania wako makini sana na uamuzi wanaofanya kwahiyo usidhani kuwa wanaweza kuchagua hata nyanya mbovu kuziweka madarakani mtu kama slaa aliyekuwa mwizi mpaka kanisani atachaguliwa na nani.
 
Leo umeongea point mkuu Pasco hakika you deserved to be ILBORIAN MSULIATA.
 
Last edited by a moderator:
CCM wakubali kushindwa na wanaweza kurudi tena kwa roho safi tu.

Ila CCM waling'ang'ania madaraka, watapotea kama KANU.

Mbona DEMOCRATS na REPUBLICAN wanaweza kubadilishana utawala, UK pia, France/Ufaransa - Niko Sarkous anaweza kushinda urais tena mwakani...

Hatari ya CCM itakuwa kusababisha vurugu na itakula kwao

CCM wameanza kutapatapa, dalili hizo hapo chini-- Wamekosa Dira. Mbaya zaidi CCM imekosa umoja miongoni mwao.

--- Huoni wanavuruga uchaguzi?


---- Huoni hata uandikishaji daftari la wapiga kura una sua sua (sabotage)

-- Huoni wanataka kuingiza wanajeshi katika NEC?

-- Huoni miradi ya maendeleo imesimama... MCC na flyovers

- Budget ya serikali imekwama -- wafadhili wamekata misaada..

-- Ilani ya CCM haitatekelezeka....

- Madawa hospitali hakuna

-- Vijana hawana ajira... Kuna wasomi zaidi ya Million moja mitaani wamemaliza Varsity

Sasa piga hesabu wazazi wa hawa vijana, ndugu zao wa karibu wataikataa CCM..

Yaani CCM ikijaribu kutumia TISS, Polisi, na Wanajeshi... Haitasaidia.... Kimbunga kitaezua Nyumba tuu... No way
Na ikiwa Hivi ndo mbaya zaidi... Maana ikitokea Vita halafu Mafisadi wakakimbilia nje walikoficha pesa... imekula kwao, Wazungu watawageuka.... Watakuta akaunti nyeupe... Labda waweke pesa Cash kwenye sandarusi, salfate, mabox na rambo waende nazo South Africa (trillion ya Shimbo) na labda Saudi Arabia....

Yuko Wapi Mobuto Seseseko na mapesa yake, gadafi.....
 
Hakuna nchi ambayo inaongozwa kwa bangi kama unavyodhani, watanzania wako makini sana na uamuzi wanaofanya. kwahiyo usidhani kuwa wanaweza kuchagua hata nyanya mbovu kuziweka madarakani. ......

Ebu sema/andika vizuri unachowaza na ambacho ulikusudia kusema/andika.
 
Asante Pasco kwa kuketa uzi. Nini kifanyike, tunaliomba jeshi la wananchi lijiandae kusimamia haki na sio kusuburi kupewa amri na ccm. Nasema hivyo kwani jeshi la polisi limepoteza uhalali wa kusimamia haki bali limejigeuza ni tawi ama jumuiya ya ccm. Na hili linatokea kwani jeshi la polisi kwa kushirikiana na ccm wamekuwa wala rushwa wakubwa hivyo wana kanuni ya nifae kwa jua nami nikufae kwa mvua. Niwatake na viongozi wa dini sasa ni wakati wa kuhakikisha wanalitendea haki taifa hili. Hao viongozi wa ccm wakiwataka waliombee taifa amani wawaulize nini sababu ya kutoweka amani? Najua hawana jibu zaidi ya propaganda za kizamani. Hivyo wawaambie waache demokrasia ya kura itawale vinginevyo umma utachukua hatua. Nadhani kila mmoja anajua nini kitatokea iwapo umma utaamua. Vijana sasa ni wakati wetu kusimama tayari kwa kulitetea taifa letu linaloporwa na kikundi cha wahuni.

Asante mkuu...
 
Wanabodi,

Baada ya vyama vya upinzani kupata ushindi wa matumaini na CCM kuporwa mitaa na vijiji kadhaa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kumefufua matumaini ya uwezekano wa CCM kushindwa jumla katika uchaguzi mkuu ujao, hivyo kuweka possibility ya CCM kuwa ni chama cha upinzani Tanzania ama baada ya 2015 au 2020!.

Wengi tunajua kuwa CCM huwa inashinda chaguzi mbalimbali, sio tuu kwa sababu inapendwa, au imewatendea wema Watanzania, bali CCM kiukweli CCM imechokwa!, ila bado huwa inashinda kwa mbinu mbali, ambazo some ni hooks & crooks!, kunakopelekea wengi wa wapiga kura kujikuta, hata wafanye nini, CCM ni lazima tuu itashinda!, hali iliyopelekea watu kujikatia tamaa na any possibility ya CCM kushindwa, hivyo kuamua kuliko kupoteza muda wao kupiga kura, bora wajilalie tuu majumbani mwao, ndio maana tumeshuhudia watu milioni 22 wakijiandikisha, kisha ni watu milioni 8 tuu wakijitokeza!, hivyo msindi wa urais kushinda kwa kura milioni 5 tuu, ambayo ni asilimia 9% tuu ya watu milioni 45!.

Pia kuna maeneo CCM imechokwa ila bado inaendelea kushinda kwa mazoea tuu, watu hawana elimu ya uraia ya kutosha, hivyo kuamini kuwa chama kinachopaswa kuongoza Tanzania milele ni Chama cha Mapinduzi CCM!.

Kwa vile CCM imezoe kushinda kwa mbinu, kuna mwanajf alisema humu, kuwa hufikia wakati, hata "the greatest magicians runs out of tricks!" hivyo CCM waliishiwa mbinu, wakashindwa huko walikoshindwa!.

Wengi wanajipa matumaini kuwa kushindwa huko, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM!, lakini inawezakana pia isiwe hivyo, inawezekana sasa ni faru amejeruhiwa!, faru ni mnyama mpole sana, ila akijeruhiwa, atakuwa ni myama wa hatari sana, huisimamisha ile pembe yake na kukimbia hovyo chochote atakachokutana nachoto mbele yake, anatoboa na pembe hiyo!.

Hivyyo kuna uwezekano sasa CCM ikaja na mbinu mpya za faru aliyejeruhiwa hivyo uchaguzi wa 2015 ikakomba kila kilicho mbele yake!, jee unajua ni kwa nini, CCM lazima ilazimishe kubakia madarakani?!.

Nimekuwa inspired kuandika uzi huu na thread ya mwana jf huyu


Sipati picha bendera za Chadema kwenye majengo ya CCM!.

Wakati wa chama kimoja, CCM ilichangiwa kwa lazima na wafanyakazi wote!, ile siku tunaanza vyama vingi, kiuhaki na kiuhalali, ilibidi mali zote CCM iliyomiliki kwa michango ya lazima, zilipaswa kurudishwa serikali, zikiwemo zile mali CCM iliyozivuna kama chama dola, mfano uwanja wa CCM, Kirumba, ukumbi wa CCM, Kizota, Jengo la Makao Makuu ya CCM, Dodoma, Jengo la Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba, na mali zote za jumuiya za CCM, likiwemo jengo la Umoja wa Vijana, lile jengo la Airtel etc, yalipaswa kurudishwa serikalini, yaani kutaifishwa kuwa mali ya umma!.

Kitendo cha CCM kuendelea kuzishikilia hizo mali, ni wizi, ujambazi na uharamia kwa jasho la Watanzania!. Nilishauri, kama kweli itakuja kufika siku, CCM ikawa ni chama cha upinzani, huo ndio utakuwa mwisho wa CCM, milele, maana kazi ya kwanza ya chama kingine kikitawala, itakuwa ni kuipoka, na kuipurura CCM, malizo zote ilizojitwalia kwa uporaji (looting), na kuzigeuza ni mali ya umma!.

CCM ikiishaporwa kila kitu!, kamwe haiwezi kuamka tena!, that will be the end of it jumla, ndio maana kwenye chaguzi mbali mbali CCM does all it can to remain in power, maana naming CCM hili wanalijua, hivyo nawaombeni sana msiendelee kuishangaa CCM inapotumia all the means, by hooks and crooks to remain in power, ni pamoja the fear of unknown!, on what will happen, if CCM looses, ndio maana mnaona hakuna any preparations kwa serikali na vyombo vya dola, kuitumikia serikali ya chama kingine!.

Kama ilivyo kanuni ya the law of the jungle ni "struggle for existence, survival for the fittest", bila kujali ni mbinu gani zitatumika kushinda uchaguzi, kwa sababu mwisho wa siku, uhalali wa mshindi, unapatikana kwa "the end, justify the means!", "The winner takes it all!, the looser standing small!.

Mnaondani kuwa baada ya kipigo hiki cha serikali za mitaa, CCM will just sit and watch!, they might be wrong!.

Namalizia kwa swali, kama CCM imekuwa ikitumia mbinu za Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi mbali mbali, ili kuhakikisha inabakia madarakani, kwa sababu inajua ikishindwa, ndio itakufa jumla, jee unadhani CCM itakubali kujikalia na kujiangalia tuu huku ikijifia kibudu, au itaendelea kufurukuta mpaka itakapo kata roho?!.

Jumapili Njema,

Pasco.

Maajabu
CC:- Mungi, Filipo, Yericko Nyerere, Ben Saanane
 
Endapo CCM wakishindwa nawakiamua kulazimisha ushindi ndo utakua mwanzo wafujo kwani wananchi hawata kubali wao wanajua wamemchagua nani hivyo nivizuri ustarabu kutumika

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Nionavyo mimi chama kilichopo madarakani hakuihubiri kitafanya nini bali kimefanya nini. Kwa sasa utekelezaji wa mambo mengi umekwama sana kutokana na uhaba wa fedha jambo ambalo limaweza kuzua balaa kwao maana watu wanataka kuona nini kinafanyika

Lakini pia hata kama hawafanyi hayo mambo mfumo mzima umekaaje? Kama mfumo unatetea wezi hadharani kabisa ni jambo la ajabu na kutia hasira kabisa.
 
Back
Top Bottom