Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Kuna uwezekano mkubwa kuwa CCM hawatasimamisha mgombea Arusha Mjini.
Wanajua kutakuwa na kura za hasira kwa jinsi kesi ilivyoendeshwa na namna hukumu ilivyotolewa.
Pili wanajua kuwa chama hakina tena mvuto kwa wananchi hasa hasa mijini na kama uchaguzi utarudiwa yatatokea yale yale ya Arumeru Mashariki.
Tatu, katika CCM ya sasa hakuna tena kada anayeamika kwa wananchi, Nkapa kachemsha na sidhani yuko tayari kudhalilishwa mara ya pili ndani ya miezi mitatu, Six amejaribu Kirumba kachemsha, Mama Kilango kachemsha Kiwira(vijijini), sijui sasa watamtuma nani akamsaidie mgombea wao. Kwa upande mwingine CHADEMA hata wakinituma mimi, ambaya hata sina cheo, nitawaongoza kushinda.
Kama wakifanya kosa wakasimamisha mgombea, na kulingana na upepo wa kisiasa wa sasa watapoteza tena uchaguzi, watakuwa wameamua rasimi kurudisha serikali mikononi mwa Wananchi kwani 2015 itakuwa ni kujumlisha kura tu!
Naona kuna uwezekano mkubwa kimada wa sisiyemu anaweza kuombwa asimamishe mgombea ambaye magamba watamuunga mkono nyuma ya pazia na kujiepusha na aibu ya kushindwa mara mbili ndani ya miezi mitatu.
Naomba kuwasilisha
Wanajua kutakuwa na kura za hasira kwa jinsi kesi ilivyoendeshwa na namna hukumu ilivyotolewa.
Pili wanajua kuwa chama hakina tena mvuto kwa wananchi hasa hasa mijini na kama uchaguzi utarudiwa yatatokea yale yale ya Arumeru Mashariki.
Tatu, katika CCM ya sasa hakuna tena kada anayeamika kwa wananchi, Nkapa kachemsha na sidhani yuko tayari kudhalilishwa mara ya pili ndani ya miezi mitatu, Six amejaribu Kirumba kachemsha, Mama Kilango kachemsha Kiwira(vijijini), sijui sasa watamtuma nani akamsaidie mgombea wao. Kwa upande mwingine CHADEMA hata wakinituma mimi, ambaya hata sina cheo, nitawaongoza kushinda.
Kama wakifanya kosa wakasimamisha mgombea, na kulingana na upepo wa kisiasa wa sasa watapoteza tena uchaguzi, watakuwa wameamua rasimi kurudisha serikali mikononi mwa Wananchi kwani 2015 itakuwa ni kujumlisha kura tu!
Naona kuna uwezekano mkubwa kimada wa sisiyemu anaweza kuombwa asimamishe mgombea ambaye magamba watamuunga mkono nyuma ya pazia na kujiepusha na aibu ya kushindwa mara mbili ndani ya miezi mitatu.
Naomba kuwasilisha