Lakini chama hiki kina historian ya kupita katika vipindi vigumu na vya misukosuko mikubwa mwisho wa siku kina kaa sawa na wanaendelea. Tokea enzi wanafukuzwa uongozi kina Aboud Jumbe watu wakadhani Afro Shirazi inarudi CCM inameguka lakini wapi, ikaja walipofukuzwa kabisa uwanachama kina Seif Sharif Hamad, Juma Dunia Haji, Hamad Rashid na wenzao pamoja na nguvu waliokua nayo lakini CCM ikakaa sawa. Kina Jenerali Ulimwengu, Njelu Kasaka na wenzao katika movement ya G55 napo pia wakapita salama!
Nyakati za uchaguzi mkuu kupata mgombea wa CCM nafasi ya uraisi nadhani pia hua ni kipindi kigumu sana kwao lakini meli yao inapita katika dhoruba hizo na kuibuka ufukweni salama! Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa lakini ukweli ki oganaizesheni CCM wapo vizuri kupita maelezo! Misukosuko inayokipata ingekua chama kingine chochote hapa nchini ingekua ni historia na tungesha kisahau