Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
- Thread starter
- #41
Tangu lini Ngedere akamfukuza Nyani kwenye Shamba la mahindi?
Fupa kalishindwa Fisi ataliweza Mbwa kweli?
Nimeipenda hii. Inaeleza wazo zima kwa ufasaha. Nyani kwa umbile ni mkubwa kuliko ngedere. Wote ni wavamizi katika shamba la mahindi. Ngedere kwa umbile na nguvu zake ndogo, hawezi kumfukuza nyani kwenye shamba. Ngedere anakula mahindi shambani kwa ridhaa ya nyani. Nyani akicharuka, anaweza kumfukuzia ngedere mbali. Ngedere akitaka kushiba, itabidi ale mahindi kimya kimya, bila kumbughudhi nyani.