CCM inataka kumwekea Lowassa pingamizi

CCM inataka kumwekea Lowassa pingamizi

Makamu mwenyekiti wa ccm anasema mgombea urais wa Ukawa amekiuka makubaliano 12 yaliyowekwa sahihi na vyama vya siasa, tume ya uchaguzi na serikali. Aliyasema haya siku ya jpili kwenye mdahalo wa Nyerere Foundation uliofanyika jpili tarehe 16.08.2015
Ukawa hakikisheni lowasa hasemi chochote ambacho kitakwenda kinyume cha makubaliano hayo.
Hayo makubalino ni ya kisheria kwa maana ya kwamba yapo kwenye sheria za uchaguzi zinazotambulika na Tume ya Uchaguzi? Mbona JK kakiuka makubaliano mengi tu waliyofanya na vyama vya upinzani ikiwa ni pamoja na uundwaji wa tume huru ya uchaguzi na kusitishwa kwa bunge la katiba na hajafanywa chochote. Makubalino ya vyama sio sheria za uchaguzi. Ndio maana hata UKAWA ni makubaliano ya vyama lakini siyo sehemu ya sheria za uchaguzi kuweko kwa UKAWA
 
Mwaka huu ndio mwisho wa Viongozi mnaowalaza makaburini. Imeandikwa mchawi na asiishi, mwaka huu kule bagamoyo makaburini mlikokuwa mnamwagulia Jk tumemaliza kazi yake. Mlima kilimanjaro mlikokuwa mmezindika kiuchawi ili mzidi kutawala tumepanda na kupindua pindua maagano na vibuyu vyenu. Shekhe Yaaya mliyekuwa mnamtumia kujaza majini ikulu tulimpa miezi 5 kutubu vinginevyo atakufa akajidai yeye mtaalamu tukamkata mtama may 2011 hadi kuzimu!!!

Tukawaambia na watumishi wakawaonya ccm acheni ujambazi mnaowafanyia watanzania mkajibu kwa kejeli tena mkasema watumishi wa Mungu ni wapuuzi!!!

Tukawaambia wote mnaopata uongozi kwa kulala makaburini mwaka huu hamtapenya. Tunasema tena wachawi wote na wanowaagua viongozi mwaka huu mmeng'ata jiwe, tumevibomonda vibuyu vyenu, tumezitawanya tunguli zenu na kuvuruga mipango yenu.

Nakumbuka ktk safari hii akaja Mtumishi mmoja, Askofu Z. Kakobe mkamdhihaki na kumdharau mkasema hana hadhi kujibishana na nyie alipowaandikia ikulu barua ya upendo tena ya kinabii akiwataka mbadilike!! Tena akawa mkarimu kwenu kwa kuwafunulia siri za Mungu kuwa msipobadilika Mungu anawaangusha. Akawa muwazi kabisa kuwa msipotii mtavurugana na mtatofautiana ndimi ka wajenzi wa babeli. Tena hakuacha jambo akasema yote na jinsi mtakavyoanguka kwa kutofautiana kauli na lugha. Hamtakuwa tena wamoja ka mlivyozoea kwa miaka zaidi ya 50.

Tumeyaona hamtaki kuamini maana mmeshupaza shingo hivyo lazima ivunjike. Tumeona wajenzi wa babeli wakilingoa jiwe la pembeni la mnara huu mkuu na mawe sasa yanaporomoka kwenda bondeni penye utulivu na wajenzi wa nyumba wasiotaka mnara wa kwenda mbinguni maana ni chukizo kwa Mungu wao. Sasa jiwe kuu walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni.

Hapa ndio nampenda Mungu maana anauliza "ni jambo gani gumu nisiloliweza?" Hakika hakuna wewe ni mkuu sana.

Ndipo ninakumbuka maneno ya mtume Mwingira October 2014 akihubiri kibaa akasema "2015 mtamuelewa Mungu ninayemtumikia... mnaenda kupata raisi bora sana Mungu amesikia kilio chenu.... kama nilivyosema 2005 kuwa Tanzania inaenda kupata kiongozi mbovu kuwahi kutokea kwa miaka 10 na ikawa hivyo.... Sasa nasema tena mnaenda kupata raisi bora Afarika Mashariki. Msuniulize ni raisi gani mtayaona makanyagano ambayo hamkutegemea wengi mtashangaa yatakayotoke maana Mungu atapinduapindua siasa ya tanzania. Ila ombeni sana maana siyo kipindi raisi maana damu yaweza mwagika, ila mwisho wa siku ni ukombozi ni lazima"

Nikikaa nikitafakari na nikiona wanajimu wakija na nyota na utabiri wa kijinga nashangaa maana naona mkiumbuka. Tukutane october 25 siku ya kuhitimisha uchawi tanzania na kumuinua Mungu wa majeshi.
 
Umesema sahihi, Lowasa alishiriki ufisadi wa Richmond, akabumburushwa na ku resign. Baada ya kuresign ame reform ama ameendelea kufasidi? Ufisadi mungapi umefanyika baada ya Lowasa?



1. Richmond = Lowasa +ccm + JK etal.

2. EPA ?? + ccm + JK etal

3. Kagoda ?? + ccm + ??

4. Meremeta ?? + ccm + ??

5. REA ?? + ccm + ??

6. Escrow JK etal +ccm + ??

7. Ujenzi wa bomba la gas ?? + ?? + ccm

List inaongezeka.

Ufisadi wote huo amefanya Lowasa? Kama wewe ni mkweli, kwa nini huongelei hizi fasidi zingine ambazo ni nyingi tu na kubwa za kutisha na wahusika wake?

Ukiongelea suala la Richmond, ni kweli lowasa alihusika, lakini unamwachaje mwenyekiti wenu wa chama? Kama mwenyekiti wa chama ni fisadi kiasi hicho, bado huoni aibu kujibainisha utiifu na ufuasi wako kwake, huku ukijitahidi kushwaishi uko upande wa Watanzania?


Sasa Lowasa amebadilika, na yuko tayari kupambana na mafisadi ikiwemo kusimamia rasimu ya ktiba ya Warioba. Unawezaje kumsakama huyu aliyebadilika ukayaacha maharamia yaliyoko huko ccm ambayo yanaendelea na ufisadi huku yakiapa kufa kwa kulinda ufisadi huo?

Uwe na aibu!

Hakuna jiniaz ndani ya ccm atakaye kupatia majibu ya kweli ya maswali yako.

Maswali yako ni ya msingi sana. Sisi wananchi tusiokuwa na vyama tunaona jinsi ccm wanavyopagawa, hawalali usingizi, wanaweweseka kila linapotajwa jina EL.

Tangu 1995 sijawahi ona ccm wakichezeshwa ngoma na wapinzani namna hii. Ingekuwa mpira tungesema ccm wanatafuta mpira kwa tochi kwa vile ball possession ya ukawa ni 85% na ccm ni 15%!

Umati mkubwa wa watu wanaohudhuria kwenye mikutano ya ukawa inabezwa na ccm, wanasahau kwamba hawakubeza umati wa watu kwenye mikutano ya kampeni ya JK mwaka 2005!
 
Huyu fisadi nani amuogope mtu mwenyewe nguzo yake yote ni ufisadi tu.

Akiwa ccm sio fisadi mnamnadi na kumlinda, akihama ni mbaya ndio maana chaka cha kulea wezi? Kwa nini chenge,Tibaijuka na Ngereja mmewalea?
Hatuhitaji kichaka cha kutunzia wezi 0ctober watanzania wanakichoma,miaka 53 imetosha"!
 
HII TABIA YA KUTOKUWA MAKINI KATIKA MIKUTANO NDO INAWAPA SHIDA VIJANA WA KITANZANIA, mimi nilikuwepo kwenye mdahahlo huo Mzee Mangula aliongelea vitu viwili kimoja ni kanuni za maadili ndani ya ccm na akasema jinsi yalivyowaafect baadhi ya wagombea wengine ni wagombea wa Ukawa, La pili aliongea makubaliano waliokubaliana kwa vyama vya siasa, na kusema mtu anayekwenda kinyume na hayo anaadhibiwa kwa hilo. hakusema kwa namna yoyote kuwa mgombea wa Ukawa kakiuka hayo. wewe umetunga story ili kuwachonganisha watu, wacheni tabia hizo bwana
Makamu mwenyekiti wa ccm anasema mgombea urais wa Ukawa amekiuka makubaliano 12 yaliyowekwa sahihi na vyama vya siasa, tume ya uchaguzi na serikali. Aliyasema haya siku ya jpili kwenye mdahalo wa Nyerere Foundation uliofanyika jpili tarehe 16.08.2015
Ukawa hakikisheni lowasa hasemi chochote ambacho kitakwenda kinyume cha makubaliano hayo.
 
Moto wa mabua umeanza kuwachoma na bado kiwango cha mabua ni kikubwa ka Bomu la nyukriaa
 
magufuli anatumia raslimali za serikali kujipigia kampeni.pingamizi ni lazima
 
e bwana! ccm ccm ccm katika mtu nilikuwa nikimwona ni mstaarabu na anaezingatia nidham ni huyu mh. man'gula lkn kwa sababu ya kosa moja tu lakuto kusoma wakati linamkost utu wake '' basi achana nao chama hiyo imechoka imekwisha!!!!!!! la! ukingojea ikuangukie thats your choice.
 
Lowassa ndio mgombea pekee anaeweza kumkemea mtu na akaskia maana hana njaa useme atapelekeshwa na wenye ela kiukweli lowassa anauwezo wakumwajibisha yeyote alie mbele yake kama kweli unafwatilia siasa lowassa alijiuzulu kutokana na position alio kuwa nayo so huwezi mpeka hovyo kama unavyo dhani lowassa anafaa kabisa kuisimamia hii Tanzania yetu
 
young generation usually perment changes and changes always is inevitable.
 
Alipojiunga na vhama chenye msimamo huo ndio unapaswa kuwa msimamo wake pia. Je mlitarajia aende huko awabadilishe msimamo uliowaleta pamoja?


Ninachokiona hapa kuna haja kubwa sana ya kutoa elimu juu ya mabadiliko. Watu wenye uelewa mdogo hawawezi kutoa hoja za kuboresha zaidi sana wanaonyesha hofu ya mabadiliko. Wanaogopa kupoteza ama kutokea kwa wasiyoyojua.

Lakini jambo la ajabu, kuna kundi moja ama kwa makusudi au kwa ujinga, linajaribu kuwaaminisha watu kwamba mtu akihama kutoka chama kimoja na kwenda kingine, basi anahama na sera, mila na mazoea ya kule alikokuwa anayapelekea kule anakoenda. Na hili ndilo linawafanya wengine waone kama Lowasa kaenda kuharibu ukawa, na ccm wanaona kama ni kete ya kuwafitinisha wapenda mabadiliko kwamba Lowasa anahamisha ushetani wa ccm na kuuambukiza kwenye UkaWa.

Watu wanapaswa kujua wahamiaji wote wanakwenda CHaDEMA kwa kuwa wameona ni chama makini chenye misingi imara na uwezo wa kuongoza mabadiliko katika nchi. Na baada ya kuona hawaridhiki na mifumo iliyopo ikiwa ni pamoja na kunyimwa fursa za kuwaza mabadiliko ndani ya vyama vyao, wanatafuta uwezekano huo nje ya ccm.

Lowasa anayetumiwa kwa mema na mabaya, amesema alitafuta fursa za kufanya mabadiliko ndani ya ccm lakini alinyimwa na akaona mahala sahihi pa kufanay hayo ni CHADEMA. Sasa kwa nini watu wasiamini kwamba anakohamia anakwenda kuungana na manguli aliowakuta kuongeza nguvu ya mabadiliko?

Kwa nini waamini kwamba Lowasa ataharibu kundi lote la waadilifu wa UKAWA, pamoja na nia yake njema na wasione kama kundi la waadilifu wa UKaWA ndiyo misngi wa mabadiliko ya kuwabadilisha wtu mmoja mmoja na chi nzime kutoka kwenye u ccm kwenda kwenye Utanzania?

Lowasa should not be an agenda now. Tumwone yeye na wageni wenzake, pamoja na wenyeji wao kwamba wanafanya kazi moja ya kulikomboa taifa kwa misingi ya UKaWA na si uozo unaonuka kule ccm.


Ccm haipaswi kupewa nafasi ya kuendelea ku create confusions na hofu eti Lowasa amehamishia ufirauni CHADEMA kwa kuwa hata yeye anasema anasimamia katiba ya Warioba? What else? Ukawa siyo ccm kila mtu aamue kufanya atakacho. Kla mmoja anafanya vile UKaWA unataka.

Pengine kwa kuwasaidia ccm, ni vizuri wakashughulika na mafisadi wao walioota magamba sugu huko ccm ambao wameapa kuendeleza ufisadi at any cost.

UKaWA, waachie wapigania ukombozi waliopo na wanaoungana na hili jeshi ili kuongeza nguvu na kasi ya ukombozi.
 
Siku hizi hakuna sasa kumekucha Dodoma
heri fisadi kuliko mpambavu na mjinga...mmetugeuza wauza chupa za uhai...vijana wote kazi yetu ni kuokota chupa...loll...laana iawapate nyie na watoto wenu...kizazi cha dot com kidumu na bahari ya mabadiliko ikawaangamize nyie ma ccm na familia zenu pamoja na mkuu ya kaya ya washirikina
 
Hata ukiipaka asali habari yako ni ya kulazimisha sana, ni kana kwamba sisi wengine hatukuwepo na wala hatukukisikia alichokisema Mangura ..acha kutunga stori kama una video irushe hapa siyo kukalia kuzusha ..Lowassa haitaji kuwekewa pingamizi lolote kwasababu hata kampeni yenyewe bado inamtoa nje na kamwe hawezi kumudu mchakamchaka wake
 
Unajua ukiona mtu anamdanganya mtu mwenye akiri timamu na yy akakubali basi hilo ni tatizo kubwa sana, kama Lowasa alitaka kuleta mabadiliko nani alimzuia? na swala Richmond kama alistuka mbona hakujiuzuru kama Mrema? chadema walitaka apitishwe na ccm ili wamchafue zaidi na zaidi, na ushahidi chadema wanao, kwani ndo walifany uwaziri wake mkuu kwisha, na pia hawa wapuuzi ndo walikataa Lowasa kuitwa waziri mkuu msitafu, leo ushahidi unefichwa na wao ss ndo wanamwita waziri mkuu msitafu, ujinga huu ni kwa ajili ya mburula tu na si kwa watu makini na wanaoipenda nchi yao. Pesa ya Lowasa imefanya Dr. Slaa kuonekana mjinga na hafai kwa watanzania, Prof. Lipumba kaonekana hafahi kabisa, ni ujinga kukbaliana na mawazo ya ujinga, ss Mbowe na wenzake wameanza tena kuwa wamepata tetesi, hizo tetesi na kama ushahidi wanao, basi waende mahakani, kwani sisi wanachi si mahakama ya vigeugeu. kwa kweli hatupendi ujinga huo ujirudie, kwani hata kama hatukusoma lakini picha twaweza kuiona.
 
Back
Top Bottom