CCM inamilikiwa na nani?

CCM inamilikiwa na nani?

Uzuri wa CCM ambao vyama vingine vinatamani kuwa nao ni:
  • Haina mwenyewe unayeweza kum-point kuwa huyu ndie ccm. Chadema, CUF kuna watu_wao ndio chama_chama ndio wao. Mfano CUF ni ya wapemba na cdm ni ya wachaga. Inahitaji akili ndogo tu kukubaliana na hilo.
  • CCM haina mshiko wa udini. Chadema ina mshiko wa kidini unaotokana na mwanzilishi wake na imani ya watu wa Kilimanjaro ya uchaga(sio ya upare), majority ni wakristo. CCM haina hilo la udini na wala huwezi kufanikiwa kwa propaganda za udini ndani ya ccm.
  • CCM haina ukanda. cdm sio tu inaukanda bali pia ina sera za majimbo ambazo ni hatari sana kwa umoja wa kitaifa.
  • CCM inahubiri upendo kwa nchi (si kwa chama, maana vyama vitapita-nchi itabaki). CDM inahubiri watu waichukie nchi yao wakitukuze chama (rejea michango ya pro-cdm kwenye mgogoro wa mpaka wa malawi-walikuwa tayari kupigana upande wa malawi)
  • CCM inafanya juhudi za kuweka fursa za wananchi kutatua matatizo yao, CDM inajitahidi kutaja matatizo ya wananchi bila kueleza suluhu ya matatizo hayo.
 
Ni ukweli kuwa chimbuko la CCM ni chama kilichowaunganisha Wakulima na Wafanyakazi tena wale wa madaraja ya chini.Ikumbukwe kwamba katika harakati za kutafuta uhuru wa Tanganyika vingi ya vyama vilikua vinaanzishwa na kupata support kutoka kwa manamba, wakulima na baadhi ya wafanyakazi waliokuwa wakifanya kwa watu weupe. Harakati zake ziliratibiwa kwa umakini na walikuwa wakijiepusha na shughuli yoyote ambayo itatafsiriwa kisiasa.
Sasa nirudi kwenye hoja, kutokana na utangulizi huo utagundua kwamba mazingira ya wakati huo chama cha TANU na ASP vikianzishwa na hatimaye CCM yalikuwa yanatoa fursa kwa watu wa daraja la chini maana ndio iliyokuwa sera ya wakati huo.
Binafsi ninaamini dhana ya kuwa chama cha watu wa daraja la chini ilishabadilika tokea wakati huo. Zifuatazo huenda ndio zikawa sababu za mabadiliko hayo;
1. Kuondoka kwa ukoloni na mwanzo wa CCM kuwa chini ya wale waliofanikisha uhuru.
2. Mabadiliko ya kiuchumi yamekuwa kichocheo cha kubadilika mfumo mzima wa siasa.
3. Mabadiliko ya kitabaka kutoka lile la kikulima(kijamaa) kwenda lile la wenye nacho(kibepari).
4. Kuongezeka kwa elimu.

Hivyo basi kutokana na sababu hizo chache, unaweza ukang'amua kwamba sera ya uanzishwaji wa CCM wakati huo si sera ya uendeshaji iliyopo sasa, kwani mifumo mingi katika nchi inaendelea kubadilika.
 
CCM inamilikiwa na wajanja wajanja wasio na huruma na binadamu wenzao
 
Uzuri wa CCM ambao vyama vingine vinatamani kuwa nao ni:
  • Haina mwenyewe unayeweza kum-point kuwa huyu ndie ccm. Chadema, CUF kuna watu_wao ndio chama_chama ndio wao. Mfano CUF ni ya wapemba na cdm ni ya wachaga. Inahitaji akili ndogo tu kukubaliana na hilo.
  • CCM haina mshiko wa udini. Chadema ina mshiko wa kidini unaotokana na mwanzilishi wake na imani ya watu wa Kilimanjaro ya uchaga(sio ya upare), majority ni wakristo. CCM haina hilo la udini na wala huwezi kufanikiwa kwa propaganda za udini ndani ya ccm.
  • CCM haina ukanda. cdm sio tu inaukanda bali pia ina sera za majimbo ambazo ni hatari sana kwa umoja wa kitaifa.
  • CCM inahubiri upendo kwa nchi (si kwa chama, maana vyama vitapita-nchi itabaki). CDM inahubiri watu waichukie nchi yao wakitukuze chama (rejea michango ya pro-cdm kwenye mgogoro wa mpaka wa malawi-walikuwa tayari kupigana upande wa malawi)
  • CCM inafanya juhudi za kuweka fursa za wananchi kutatua matatizo yao, CDM inajitahidi kutaja matatizo ya wananchi bila kueleza suluhu ya matatizo hayo.
Jaribu kuelewa unachoongelea hapo kwenye nyekundu, Badala ya kulinganisha vyama unaingiza na serikali!.
 
Uzuri wa CCM ambao vyama vingine vinatamani kuwa nao ni:
  • Haina mwenyewe unayeweza kum-point kuwa huyu ndie ccm. Chadema, CUF kuna watu_wao ndio chama_chama ndio wao. Mfano CUF ni ya wapemba na cdm ni ya wachaga. Inahitaji akili ndogo tu kukubaliana na hilo.
  • CCM haina mshiko wa udini. Chadema ina mshiko wa kidini unaotokana na mwanzilishi wake na imani ya watu wa Kilimanjaro ya uchaga(sio ya upare), majority ni wakristo. CCM haina hilo la udini na wala huwezi kufanikiwa kwa propaganda za udini ndani ya ccm.
  • CCM haina ukanda. cdm sio tu inaukanda bali pia ina sera za majimbo ambazo ni hatari sana kwa umoja wa kitaifa.
  • CCM inahubiri upendo kwa nchi (si kwa chama, maana vyama vitapita-nchi itabaki). CDM inahubiri watu waichukie nchi yao wakitukuze chama (rejea michango ya pro-cdm kwenye mgogoro wa mpaka wa malawi-walikuwa tayari kupigana upande wa malawi)
  • CCM inafanya juhudi za kuweka fursa za wananchi kutatua matatizo yao, CDM inajitahidi kutaja matatizo ya wananchi bila kueleza suluhu ya matatizo hayo.

Well you really popped-up in this....big time
 
Kimbunga,

Nashukuru sana kwa kunileta kwenye uzi huu, kwani kwa sababu fulani fulani, uzi huu ulinipita. Iwapo sijachelewa sana, ningependa kuchangia mada iliyoletwa na mwenzetu 'Tubadilike Sasa' katika maeneo machache na kwa ufupi sana.

Kwanza nakubaliana na hoja yake kimsingi kwamba CCM haikistahili tena kuitwa chama cha wakulima na wafanyakazi kwani sote tunashuhudia jinsi gani makundi yote haya mawili hivi sasa yanavyozidi kuwa on a Collision Course na chama (CCM) ambacho kiliungwa mkono na wananchi wengi wakati wa harakati za uhuru wakiamini kwamba kitawatetea na kuwalinda, na wengi ya hawa walikuwa ni wakulima, na wachache wakiwa ni wafanyakazi. Napozungumzia CCM na serikali yake kuwa on a collision course na makundi haya mawili sidhani kama inahitaji mtu kuwa a rocket scientist kubaini hilo, kwahiyo sitalijadili zaidi.

Baada ya kusema hayo, ningependa kufafanua nijadili kidogo hoja kwamba huko nyuma, TANU/CCM kilikuwa ni chama cha wakulima na wafanyakazi. Kwa mtazamo wangu, Mwalimu Nyerere alipendelea iwe hivyo, hasa baada ya kufanya ziara yake vijijini (akimwachia Kawawa uongozi wa nchi) ili kujionea na kusikia njozi, matumaini na matamanio ya wengi. Tukumbuke kwamba at independence, atleast 90% ya watanzania walikuwa vijijini. Jibu alilolipata Mwalimu baada ya ziara yake ni kwamba ili kuwalipa fadhila wananchi waliojitolea kupigania uhuru, hasa waliounga mkono harakati za TANU, ilikuwa haina budi kwa Tanganyika kufuata sera ya Ujamaa, huku ikiwaweka wakulima na wafanyakazi at the centre (sio sasa ambapo wamewekwa at the periphery).

Ni muhimu sana tukaelewa kwamba kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi lilikuwa ni jaribio tu ambalo halikufanikiwa sana licha ya kulazimisha makundi haya kwa nguvu (sio kwa ihari) yajiunge kama wanachama. Pamoja na kulazimishwa huku (badala ya ihari), kwa mtazamo wangu, kulikuwa na faida na hasara zake, lakini faida outweighed hasara, kwa hiyo kwa mtazamo wangu, the end justified the means, ingawa huu ni mjadala mwingine tofauti kabisa. Kwa mfano, kwa mujibu wa ibara ya (8) ya Katiba ya TANU/CCM [WAKATI ULE], sehemu kubwa ya wananchi ikiwemo ile ya wafanyakazi, wakulima na wengine walitengwa kukosa haki ya kuwa wanachama. Ibara ya 8)7) ilitamka hivi:

Mtu yoyote hatakubaliwa kuwa mwanachama au kuendelea kuwa mwanachama isipokuwa awe ni mkulima au mfanyakazi na asiyejihusisha na mambo yoyote ya kibepari au kikabaila kama vile:

a) Kuwa na hisa katika kampuni;
b) Kuwa mkurugenzi katika kampuni ya kibepari;
c) Kupokea zaidi ya mshahara mmoja;
d) Kumiliki nyumba ambayo anaikodisha;

Hii ni tofauti sana kwa mfano na Chama Cha Kikomunisti cha China ambapo uanachama wa chama pekee cha kisiasa nchini humo yaani Chama Cha Kikomunisti cha China, uliwekwa wazi kwa raia wa aina nyingi, na kiliweza kujizolea wanachama wengi (wakulima na wafanyakazi) kwa ihari yao. Kwa mfano ibara ya (1) ya katiba ya chama hicho (1982) ilitamka hivi:

"Mfanyakazi yoyote wa Kichina, Mkulima, mwanajeshi, msomi au mwanamapinduzi yoyote ambae atakua amefikia umri wa miaka 18 na ambaye anakubaliana na programu za Katiba ya Chama na ambaye yuko tayari kujiunga na kufanya kazi katika moja ya jumuia za uanachama ipasavyo, anaweza kuomba uanachama wa Chama Cha Kikomunisti Cha China"


Pengine nisisitize tu kwamba dhumuni la kufananisha TANU na Chama Cha Kikomunisti Cha CHina ni kuonyesha tu kwamba sio kweli Mwalimu aliiga kila kitu kutoka China, lakini muhimu zaidi ni kwamba mazingira yetu yalitulazimu kufuta suala la IHARI juu ya kujiunga na CCM i.e. Wakulima na Wafanyakazi na badala yake kuwa suala la ULAZIMA, lakini kama nilivyokwisha tamka, faida outweighed hasara, na huu ni mjadala mwingine ambae nisingependa kuingia katika uzi huu.

Baada ya kusema hayo, nadhani sasa nitaeleweka iwapo nitasema kwamba TANU/CCM haikuwahi kumilikiwa na wakulima na wafanyakazi, bali TANU/CCM kilitumiwa na wakulima na wafanyakazi kuikomboa Tanganyika, na hivyo ndivyo TANU/CCM hatimaye ikaja kushika hatamu. Kuna misconception nyingi sana hata kwenye vijiwe vya CCM vya wakubwa kuhusu chama kushika hatamu. Maana halisi ya Hatamu ni kwamba - Hatamu za TANU zilikuwa ziko katika nguvu za wananchi jambo ambalo lilifanya serikali ya kikoloni, kabla ya uhuru kutambua na kuheshimu NGUVU YA UMMA; hii ndio ilifanya TANU iwe na mizizi mirefu kwenye jamii kwani UMMA ulikitegemea sana chama cha TANU kupigania uhurum hivyo kukiunga mkono katika harakati hizo; baada ya uhuru, juhudi za Mwalimu kukifanya TANU kumilikiwa na wakulima na wafanyakazi iliingia dosari kwani halikuwa jambo rahisi; kwa mfano, kikiwa ni chama pekee cha siasa enzi hizo, kilikuwa (hadi sasa) na vyombo vikuu vitatu: (1) MKUTANO MKUU; (2) HALMASHAURI KUU (NEC); (3) KAMATI KUU; Kati ya vyombo hivi vitatu, NEC ndio ilikuwa na nguvu kichama, kiserikali, kimahakama, YOU NAME IT...; Ni CCM-NEC ndio ilipitisha sheria ya muungano; ni CCM-NEC ndio ilipitisha Katiba ya 1977...na sijawahi kusoma katika historia sehemu yoyote wakulima na wafanyakazi kushirikishwa katika haya;

Vile vile sijawahi kusikia katika historia ya CCM kwamba NEC ilikuwa na idadi tosha ya Wakulima; navyoelewa mimi, wengi ya Wakulima walikuwa ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa na kama tunavyofahamu, chombo hiki kwa kawaida huwa ni Rubber Stamp tu ya NEC; Lakini again, kwa mazingira yale, the end justified the means, na faida outweighed the costs kasoro kwenye suala moja tu kubwa - MUUNGANO, na hapa nasema wazi kwamba kati ya makosa aliyofanya Mwalimu, ni muundo wa muungano, but again huu ni mjadala tofauti.

Nikirudi kwenye hoja ya 'tubadilike sasa' kuhusu CCM kutokuwa chama cha kutetea wanyonge kimsingi nakubaliana nae, kwani hata mtu ukitizama kinyang'anyiro cha sasa cha nafasi za CCM-NEC, pia nafasi za ubunge na udiwani 2010, kipimo cha kiongozi bora ni Fedha au Ukaribu/upambe kwa wakubwa, na kuwa mkulima is synonymous na didqualification kwani kwa miaka 50 CCM imeshindwa kumwezesha mkulima kuwa na uwezo kifedha, na vilevile mkulima hana uwezo wa kuwa na ukaribu na wakubwa ili na yeye ajikusanyie 'point' ili zikijumlishwa, awe na sifa za kuwa kiongozi bora.

Ningependa kumalizia kwa kuelezea jinsi gani Chama Changu Cha CCM kimeacha kusimamia mambo ambayo chenyewe iliyaweka ndani ya Muongozo (1982), na mengi ya haya, wenzetu wa Chadema wanajaribu kuyatumia kikamilifu and it pays. Chadema ina practice mambo yetu (CCM) according to Mwongozo, kwa mfano mwongozo wetu ulipotamka katika ibara ya 53 kwamba:

"Chama Cha Kijamaa kama vile CCM ni chombo cha uongozi. Hakifanyi kazi kwa amri zisizo msingi wala kufanya kazi zao kwa nguvu au vitisho vya nguvu. Kinaongoza kwa kuelimisha, kwa kuwashirikisha watu na kuonesha njia na kwa hivyo basi msingi wa nguvu zake na kuaminika kwake unatokana na kukubalika kwake kihalali miongoni mwa umma, mchanganyiko wa wanachama wake na msingi mzuri wa kisiasa ambayo inakwenda sawa na matakwa ya umma. Ili kuweza kutimiza lengo hilo Chama kinahitaji kuwa na Nguvu ya Hoja na SIO Hoja ya Nguvu."

Ni vigumu kuelewa nini kimekisibu CCM kufikia hatua ya kuwaona Chadema wanatenda sivyo huku udhaifu wetu ukizidi kukijengea Chadema HATAMU. Rejea mjadala juu ya hatamu ambapo hili ni suala la nguvu ya UMMA, sio NGUVU YA DOLA.

NI Muhimu CCM Tujisahihishe, Vinginevyo Tugawane Chama.

 
Ni siri ilio wazi, ni kundi la wafanyabiashara ambao sio Wamakonde wa Ntwara, au Wafipa wa Katavi, au Wazarao wa Pwani bali wageni ambao wote tunawajua, wengine waliwahi kutukamata utumwa, wengine waliwahi kupigana na Kinjekitile na wengine walikuwa vibarua wa kujenga reli ya kati iliokuwa ya kupeleka rasilimali zetu ulaya
 
Uzuri wa CCM ambao vyama vingine vinatamani kuwa nao ni:
  • Haina mwenyewe unayeweza kum-point kuwa huyu ndie ccm. Chadema, CUF kuna watu_wao ndio chama_chama ndio wao. Mfano CUF ni ya wapemba na cdm ni ya wachaga. Inahitaji akili ndogo tu kukubaliana na hilo.
  • CCM haina mshiko wa udini. Chadema ina mshiko wa kidini unaotokana na mwanzilishi wake na imani ya watu wa Kilimanjaro ya uchaga(sio ya upare), majority ni wakristo. CCM haina hilo la udini na wala huwezi kufanikiwa kwa propaganda za udini ndani ya ccm.
  • CCM haina ukanda. cdm sio tu inaukanda bali pia ina sera za majimbo ambazo ni hatari sana kwa umoja wa kitaifa.
  • CCM inahubiri upendo kwa nchi (si kwa chama, maana vyama vitapita-nchi itabaki). CDM inahubiri watu waichukie nchi yao wakitukuze chama (rejea michango ya pro-cdm kwenye mgogoro wa mpaka wa malawi-walikuwa tayari kupigana upande wa malawi)
  • CCM inafanya juhudi za kuweka fursa za wananchi kutatua matatizo yao, CDM inajitahidi kutaja matatizo ya wananchi bila kueleza suluhu ya matatizo hayo.
mkuu kamati kuu ya chama chetu uwiano wa dini ukoje
 
Mkuu Mchambuzi ndio maana nikakukaribisha katika hoja hii kwani nilitegemea uchambuzi makini wa hoja toka kwako. Najua unaifahamu vyema CCM nadhani kuliko hata baadhi ya viongozi wakubwa wa CCM (huenda ukawa ni miongoni mwao!). Nimefurahi sana uliposema CCM haikuwahi kuwa ya wakulima kwa kuwa chombo cha maamuzi cha CCM/TANU ilikuwa/ni NEC-CCM ambayo haikuwa na wakulima. Pia kumbuk kwamba CC-CCM wakati huo ilikuwa na nguvu nyingi pia lakini wajumbe wake walikuwa ni vigogo wa Serikali. Nakumbuka mtu mmoja ambaye hakuwa serikalini ambaye alikuwa kwenye CC ya watu 14 (enzi hizo) alikuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Ndugu Sebastian Chale peke yake; wengine wote walikuwa ni mawaziri. Wakulima na wakwezi walikuwa wajumbe wa mkutano mkuu ambao kwa kweli haukuwa na kauli bali kudumisha fikra sahihi za Mwenyekiti na kubariki maamuzi ya CC na NEC. Wakulima hawajawahi kukimiliki Chama Cha Mapinduzi. Wafanyakazi walikuwemo ila sasa nao wengi ni wa serikali enzi hizo kukiwa na matawi ya Chama sehemu za kazi. Sasa wamiliki wa Chama inaonekana ni wafanyabiashara hasa ikizingatiwa matumizi makubwa ya fedha katika kusimikana madarakani.
 
Last edited by a moderator:
Mingoi hana fikra pevu. Sisi sio wafanyabiashara mafisadi wanaoimiliki.
 
Mkuu Mchambuzi ndio maana nikakukaribisha katika hoja hii kwani nilitegemea uchambuzi makini wa hoja toka kwako. Najua unaifahamu vyema CCM nadhani kuliko hata baadhi ya viongozi wakubwa wa CCM (huenda ukawa ni miongoni mwao!). Nimefurahi sana uliposema CCM haikuwahi kuwa ya wakulima kwa kuwa chombo cha maamuzi cha CCM/TANU ilikuwa/ni NEC-CCM ambayo haikuwa na wakulima. Pia kumbuk kwamba CC-CCM wakati huo ilikuwa na nguvu nyingi pia lakini wajumbe wake walikuwa ni vigogo wa Serikali. Nakumbuka mtu mmoja ambaye hakuwa serikalini ambaye alikuwa kwenye CC ya watu 14 (enzi hizo) alikuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Ndugu Sebastian Chale peke yake; wengine wote walikuwa ni mawaziri. Wakulima na wakwezi walikuwa wajumbe wa mkutano mkuu ambao kwa kweli haukuwa na kauli bali kudumisha fikra sahihi za Mwenyekiti na kubariki maamuzi ya CC na NEC. Wakulima hawajawahi kukimiliki Chama Cha Mapinduzi. Wafanyakazi walikuwemo ila sasa nao wengi ni wa serikali enzi hizo kukiwa na matawi ya Chama sehemu za kazi. Sasa wamiliki wa Chama inaonekana ni wafanyabiashara hasa ikizingatiwa matumizi makubwa ya fedha katika kusimikana madarakani.

Nashukuru sana kwa kuthamini michango yangu Kimbunga. Vinginevyo suala hili umeliweka vyema sana mkuu, na kwa mifano mizuri sana kama ya Sebastian Chale n.k; Nashukuru kwamba hata wewe unaliona hilo - kwamba CCM kilikuwa chama cha wakulima na wafanyakazi wakati ukweli ni kwamba hii ilikuwa ni kiini macho tu; Baada ya kusema hayo, nadhani pia utakubaliana na mimi kwamba katika zama hizi za vyama vingi, tyconization of CCM [chama kuendeshwa na wafanyabiashara lakini pia na matapeli), ni suala ambalo hata Chadema nao watakumbana nalo; hakuna chama cha siasa ambacho kipo immune na tyconization of politics, hata kwa wenzetu waliosonga mbele zaidi kiuchumi na kidemokrasia, tofauti kubwa baina yetu na wao ni kwamba wana utaratibu ambao upo transparent (ingawa sio 100%) juu ya jinsi gani wafanyabiashara wanajihusisha na siasa;

Vinginevyo ikitokea Chadema wakaanza kujenga hoja huko vijijini kwamba CCM kimekuwa chama cha wafanyabiashara, hii itakuwa a grave mistake on their part kwani hata wao (Chadema) wataenda huko huko; changamoto muhimu kwa Chadema ni kujaribu kuja na taratibu nzuri kama za nchi za wenzetu za kuhusisha siasa na biashara, kitu ambacho CCM kimewashinda;

Mwisho niseme tu kwamba mimi sio kiongozi wa CCM katika ngazi yoyote - hata uongozi wa shina au tawi sipo huko; why? kwa sababu ndani ya CCM uongozi ni Gharama na mimi ni mtu maskini kwa hilo, lakini muhimu zaidi, siamini katika kununua uongozi eti ili kwenda kuwatumikia maskini au kuwa mpambe ili kupewa madaraka; Kwa sasa mimi ni mwanachama hai wa CCM lakini iwapo Nyerere ambae ni muasisi wa chama hiki alipata tamka kwamba CCM sio Mama Yake, anaweza kuachana nacho, nitakuwa najidanganya kusema kwamba CCM ni mama yangu; hadi pale nitakapotumia haki yangu ya kikatiba kushiriki shughuli za kisiasa kupitia chama nitachoona kinanifaa, nitaendelea kuwa mwanachama wa CCM lakini siku nikija humu na kuzungumza kama mwanachama wa CUF, TADEA, CCK, NCCR, Chadema etc, au chama kitacho split from CCM, naomba usishangae kwani kutakuwa na sababu ya msingi ya kufanya hivyo, na uwezekano huo upo;
 
Back
Top Bottom