CCM inaligawa taifa, Rais Magufuli ingilia kati

Mkuu usikwepeshe mada anayeligawa Taifa ni Magufuli ambaye pia ni kiongozi mkuu wa MACCM. Tusipindishe ukweli na huu unaosema ni upuuzi wa akina Pole pole muumbaji wake si mwingine bali ni huyo huyo anayeligawa Taifa. Unadhani Pole pole anaweza kufanya lolote ndani ya MACCM ambalo halina baraka za malaika?

Huyo uliyemwandikia ndo kinara wa kuligawa taifa huyo polepole unamwonea bure anapata maagizo kutoka juu.

Magufuli ndio mwalimu wa ujinga wote huu unaofanywa na akina Polepole, hivyo ni ngumu sana kuingilia kati kwa mambo anayoyatengeneza mwenyewe
Hofu yangu msije kuitwa wachochezi kwa kumtaja miunguwatu!!

Cairo's
 
  • Thanks
Reactions: BAK
bro huyo mtu unaye,uomba aingilie kati ndoto zake siku moja vyama vingine vipotee ibaki ccm so kuomba aingilie kati mkuu naona kama unapotoka kidogo hakuna wa kuingilia kati Cc kankoko leo ulisikia mkuu alivomuita mbunge aliyechagulia kua kambunge kenu kaliahidi maji halafu serikali yake itekeleze thubutu labda 2020 wasirudie kosa km hilo
Alisema hivyo kweli?! Ahh basi nchi iliingia chaka mbaya!!!. Nyerere anahitajika leo kuliko wakati wowote ule.

Cairo's
 
"Nashukuru Kigoma mlichagua sana CCM na wabunge wengi ni wa CCM, mimi ni Rais wa wote bila kujali vyama vyao, wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA (Mh Kasuku Bilago) katakuwemo tu, ila Buyungu siku nyingine mchague vizuri, huyu mbunge ananiomba maji kama ana uwezo si alete yeye? Miradi yote inaletwa na CCM"

JPM, Kakonko, 21/07/2017.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yeriko unaongea kama unavuta bangi mimi nina ndugu yangu CCM tena kada wa umoja wa vijana kanyimwa mkopo kisa kasoma shule za private wakati mama yake mama nitile amekopa mikopo ya pride kibao .Weka data.Sasa hivi mzigo umetuangukia ndugu sababu yeye kasoma sayansi na vigezo vya bodi ya mikopo vilikuwa vinataka aliyesoma sayansi na anaenda kuchukua digrii ya sayansi apewe mkopo.Magufuli alivyoingia akabadilisha kwa hili kusema WanA CCM ndio wanapata mikopo elimu ya juu ni uongo
Bahati mbaya hujamuelewa Yericko.Ikiwa bodi ya mikopo iko chini ya serikali ya CCM inakuwaje washindwe kuishauri serikali yao mpaka ifikie hatua ya kuitana Chmani?
 
"Nashukuru Kigoma mlichagua sana CCM na wabunge wengi ni wa CCM, mimi ni Rais wa wote bila kujali vyama vyao, wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA (Mh Kasuku Bilago) katakuwemo tu, ila Buyungu siku nyingine mchague vizuri, huyu mbunge ananiomba maji kama ana uwezo si alete yeye? Miradi yote inaletwa na CCM"

JPM, Kakonko, 21/07/2017.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kumbe alisema hivi!! Huyu ni Rais Mbaguzi kuwahi kutokea Tz..Hatari sana
 
Yeriko unaongea kama unavuta bangi mimi nina ndugu yangu CCM tena kada wa umoja wa vijana kanyimwa mkopo kisa kasoma shule za private wakati mama yake mama nitile amekopa mikopo ya pride kibao .Weka data.Sasa hivi mzigo umetuangukia ndugu sababu yeye kasoma sayansi na vigezo vya bodi ya mikopo vilikuwa vinataka aliyesoma sayansi na anaenda kuchukua digrii ya sayansi apewe mkopo.Magufuli alivyoingia akabadilisha kwa hili kusema WanA CCM ndio wanapata mikopo elimu ya juu ni uongo
Hoja ya yeriko ni hiyo tweet ya polepole inavyoleta ubaguzi. Ukweli unaousema wewe ni uthibitisho kuwa ubaguzi hauwezi kuiacha Tanzania na watu wake, bila kujali itikadi zao, salama!
 
Kama serikali yetu sikivu ya Rais wetu kipenzi John Pombe Magufuli haitaingilia kati kuzuia "upuuzi" huu unaofanywa na chama cha Mapinduzi chini ya akina Hamfrey Polepole, tutarajie kesho kutatangaziwa kuwa wale wanachama wote wa CCM wanaoumwa na hawana hela ya kutibiwa Muhimbili waende Ofisi za CCM Lumumba dawa na vipimo vya CT Scan vinagawiwa pale bureee.

Tafsiri yake ni kuwa ccm inatengeneza sera zisizotekelezeka ili watu wakose mikopo na kisha itumie tatizo hili kwa vijana wetu kujinufaisha kisiasa, kwamba ili upate mkopo lazima uwe na kadi ya ccm tena uende Lumumba,

Kumbuka ccm hii ndio inayoongoza serikali, yaani ile bodi ya mikopo kwa wanafunzi ipo chini ya serikali ya ccm, iweje ccm hii badala ya kuishauri serikali wanafunzi wapateje mikopo, ati inasema vijana wakapange foleni Lumumba ili kupata mikopo???

Hivi tukisema ccm imekwenda kuchota pesa ya umma kule bodi ya mikopo na kuzihamishia vichochoro vya Lumumba na kisha kutoa mikopo hiyo kwa vijana kwa sharti uwe mwanaccm, Wanaweza kujiteteaje?

Nawahakikishia ccm mnaligawa taifa mchana kweupe, na laana hiii haitawaacha salama... Kama ccm inamsaada huo ipeleke mojakwamoja bodi ya mikopo ili vijana wetu Wakitanzania wote bila kujali itikadi za kisiasa wakapate mikopo hiyo...

Rais wangu Magufuli ingilia kati hili, ccm wanakuhujumu mchana kweupe!

Na Yericko Nyerere

View attachment 547617
Yeriko kuwa shujaa, sema Magufuli, Polepole hana kauli, ukiona ametoa kauli imetoka kwa aliyemchagua.
 
Kama mikopo ya uni imehamia lumumba ni hayari kubwa. Hapo viongozi na wasomi wote waende wapinge hili.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom