Maneno haya ameyasema jana, je ni ya kweli au.....? Kama hivi ndivyo asemavyo, kweli hapa kazi tunayo."Nashukuru Kigoma mlichagua sana CCM na wabunge wengi ni wa CCM, mimi ni Rais wa wote bila kujali vyama vyao, wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA (Mh Kasuku Bilago) katakuwemo tu, ila Buyungu siku nyingine mchague vizuri, huyu mbunge ananiomba maji kama ana uwezo si alete yeye? Miradi yote inaletwa na CCM"
JPM, Kakonko, 21/07/2017.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe kikuku hebu angalia umeandika nini na mtoa mada kasema nini???Yeriko unaongea kama unavuta bangi mimi nina ndugu yangu CCM tena kada wa umoja wa vijana kanyimwa mkopo kisa kasoma shule za private wakati mama yake mama nitile amekopa mikopo ya pride kibao .Weka data.Sasa hivi mzigo umetuangukia ndugu sababu yeye kasoma sayansi na vigezo vya bodi ya mikopo vilikuwa vinataka aliyesoma sayansi na anaenda kuchukua digrii ya sayansi apewe mkopo.Magufuli alivyoingia akabadilisha kwa hili kusema WanA CCM ndio wanapata mikopo elimu ya juu ni uongo
Yericko, haya si ya CCM pekee ni pamoja na mwenyekiti wao si kwamba hajui yeye ndiye mastermind wa yote haya yanayotokea...Kama serikali yetu sikivu ya Rais wetu kipenzi John Pombe Magufuli haitaingilia kati kuzuia "upuuzi" huu unaofanywa na chama cha Mapinduzi chini ya akina Hamfrey Polepole, tutarajie kesho kutatangaziwa kuwa wale wanachama wote wa CCM wanaoumwa na hawana hela ya kutibiwa Muhimbili waende Ofisi za CCM Lumumba dawa na vipimo vya CT Scan vinagawiwa pale bureee.
Tafsiri yake ni kuwa ccm inatengeneza sera zisizotekelezeka ili watu wakose mikopo na kisha itumie tatizo hili kwa vijana wetu kujinufaisha kisiasa, kwamba ili upate mkopo lazima uwe na kadi ya ccm tena uende Lumumba,
Kumbuka ccm hii ndio inayoongoza serikali, yaani ile bodi ya mikopo kwa wanafunzi ipo chini ya serikali ya ccm, iweje ccm hii badala ya kuishauri serikali wanafunzi wapateje mikopo, ati inasema vijana wakapange foleni Lumumba ili kupata mikopo???
Hivi tukisema ccm imekwenda kuchota pesa ya umma kule bodi ya mikopo na kuzihamishia vichochoro vya Lumumba na kisha kutoa mikopo hiyo kwa vijana kwa sharti uwe mwanaccm, Wanaweza kujiteteaje?
Nawahakikishia ccm mnaligawa taifa mchana kweupe, na laana hiii haitawaacha salama... Kama ccm inamsaada huo ipeleke mojakwamoja bodi ya mikopo ili vijana wetu Wakitanzania wote bila kujali itikadi za kisiasa wakapate mikopo hiyo...
Rais wangu Magufuli ingilia kati hili, ccm wanakuhujumu mchana kweupe!
Na Yericko Nyerere
View attachment 547617
Kama serikali yetu sikivu ya Rais wetu kipenzi John Pombe Magufuli haitaingilia kati kuzuia "upuuzi" huu unaofanywa na chama cha Mapinduzi chini ya akina Hamfrey Polepole, tutarajie kesho kutatangaziwa kuwa wale wanachama wote wa CCM wanaoumwa na hawana hela ya kutibiwa Muhimbili waende Ofisi za CCM Lumumba dawa na vipimo vya CT Scan vinagawiwa pale bureee.
Tumsubiri tuoneUnasema aingilie kati wakati yeye yuko mstari wa mbele kwa hilo!