DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Alliance for Africa Farmers Party (AAFP), Said Soud Said amesema hawawezi kuungana kukiondoa Chama cha Mapinduzi (CCM) madarakani kwa sababu maendeleo yaliyofanya na CCM ni makubwa.
🗣"ni kwamba niliandaa mimi mwenye binafsi utaratibu wa kuhakikisha vyama vinaungana ili kuelekeza namna ya kuweza kuindoa CCM madarakani lakini jambo hilo limeshindikana kwa sababu vyama vimeamini kwamba yaliyofanywa ni maendeleo makubwa na kwa maana hiyo wamekataa kuungana kwa kuthamini maendeleo yaliyopo"
🗣"sasa na mimi sina budi nielekee hapo kwamba maendeleo yaliyopo ni makubwa na aliyefanya bado ana uwezo wa kufanya sasa hakuna haja tena ya kuendelea kuwa na mivutano ya kisiasa na hatimaye kufikisha nchi hii pabaya kwa mazingira tu ya kutafuta madaraka" Amesema Said Soud
🗣"ni kwamba niliandaa mimi mwenye binafsi utaratibu wa kuhakikisha vyama vinaungana ili kuelekeza namna ya kuweza kuindoa CCM madarakani lakini jambo hilo limeshindikana kwa sababu vyama vimeamini kwamba yaliyofanywa ni maendeleo makubwa na kwa maana hiyo wamekataa kuungana kwa kuthamini maendeleo yaliyopo"
🗣"sasa na mimi sina budi nielekee hapo kwamba maendeleo yaliyopo ni makubwa na aliyefanya bado ana uwezo wa kufanya sasa hakuna haja tena ya kuendelea kuwa na mivutano ya kisiasa na hatimaye kufikisha nchi hii pabaya kwa mazingira tu ya kutafuta madaraka" Amesema Said Soud