CCM haitaiacha ikulu kwa kura

CCM haitaiacha ikulu kwa kura

Mtoto CCM kufia Rais Kikwete mapajani rasmi mnamo 2015.

Na hapo mbeleni kidogo, kutatokea POLITICAL RE-ALLIGNMENTS kwa namna ambayo hata viongozi wa sasa huko CCM hawatokaa waamini macho yao. Wapo watu wengi sana tu ndani ya CCM ambao tunawafahamu fika kuwa ni wasafi na waadilifu sana ila tu wamefata tu kupakwa shombo ya UFISADI kwa kuwa tu wamo ndani ya chungu kimoja na wale wazandiki.

Ujumbe wetu kwa masalio ya wasafi na waadilifu ndani ya CCM hadi hivi sasa ni kwamba kamwe hawajachelewa kuchukua hatua kujitenga na uozo na waficha fedha za umma nchini Uswisi.
 
Mada imejaa mantiki haswa!! Wakati mwingine inatisha kufikiria itakuwaje siku CCM ikitakiwa kuondoka pale mogagoni hasa kwa kuangalia jinsi walivyojisahau kwa kukiuka katiba ya chama chao na ya nchi pia. Cha ajabu hawajitambui wala kuona makosa wanayofanya. Wamekuwa wagumu na wazito kusoma alama za nyakati. Watu wa aina hii ni hatari mno. Mchango wangu ni kama ifuatavyo.

Vyama vya upinzani na wananch wenye kutaka mabadiliko wawe kitu kimoja na wajitahidi kufanya yafuatayo mapema kabla ya kipindi cha uchaguzi mkuu ujao:

  • Kuwapatia wananchi elimu ya uzalendo na maana ya kupiga kura
  • Kuchangia kwa bidii mawazo chanya kwenye katiba mpya iweke wazi mambo muhimu ikiwa ni pamoja na jinsi madaraka yatakabidhiwa kutoka chama kimoja kwenda kingine
  • Kufanyia kazi suala la kuwa na tume huru ya uchaguzi inayojumuisha wananchi wenye weledi na wataalam wa kimataifa (SADC) na Commonwealth (hii ni kutokana na nchi za SADC kuhusika katika chaguzi kwenye nchi chini yake na Commonwealth kujikita sana katika dhana ya utawala bora).
  • Kuomba msaada wa kimataifa kusimamia mchakato mzima wa kupiga kura kuanzia daftari la wapiga kura mpaka wakati wa kupiga kura kwa hoja ya kuzuia wizi wa kura ambao kwa Tanzania ni kikwazo kikubwa.
  • Kuwe na matumizi ya teknologia ya habari na mawasilanao kwa kiwango cha juu kabisa wakati wa kupiga kura kwenye maeneo yote yaani vijijini na mijini ili kupunguza kama si kumaliza tatizo la kuiba kura.
 
Wasi wasi wa mleta mada ni wa kweli kabisa, kuna kila dalili kuwa CCM haitakuwa tayari kuondoka Ikulu kwa sanduku la kura.

Mfano mmojawapo mkubwa kabisa ni haya mauaji ya polisi yanayoendelea nchi nzima, kwenye shughuli za CDM, huo ulikuwa mpango mahsusi wa CCM, kutaka kukipakazia Chadema kuwa ni chama cha fujo, ili baadaye vibaraka wa CCM, kina Tendwa wakifute.

Bahati nzuri sana kwa CDM, tukio la picha zilizoonyesha polisi wakimsulubu Mwangosi kule Nyololo, hadi kutoa roho yake, limeiokoa CDM, na mpango huo mchafu, uliokuwa ukiratibiwa kwa karibu na msajili wa vyama.

Ili kuamini kuwa ule ulikuwa mpango mahsusi wa chama tawala, hadi hivi leo, si Kamuhanda wala Mwema, waliokubali kujiuzuru, na bosi wao JK, hajawafukuza kazi ingawa ni dhahiri mauaji yale yalikuwa ya makusudi kabisa.

Kwa maana hiyo, huo ni ushahidi tosha CCM wanajua kabisa, uwezekano wa kushinda uchaguzi wa 2015, ushakuwa finyu sana, sawasawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano. Sasa nini cha kufanya, ni kuongeza awareness kwa wananchi kuwa CCM, hawatakuwa tayari kuondoka Ikulu kirahisi.

Kwa hiyo kazi kubwa ya kufanyika kuanzia sasa hadi 2015, ni kutoa elimu ya hali ya juu ya kulinda kura hadi wakati wa kutangaza matokeo. Ninaamini hata wao wakishajua mbinu zao zote za kubaki madarakani zinajulikana, wataanza kujiandaa kisaikolojia kuondoka Ikulu.

Na wao hawatakuwa wa kwanza kukabidhi nchi kwa upinzani. Jirani zetu Zambia wamefanya hivyo, hivi karibuni. Ghana, Kenya, Malawi, weshawahi kufanya hivyo. Sioni kwa nini isiwezekane kwa wa-TZ.

La muhimu ni wananchi kujipanga tayari kwa kupokea mabadiliko. MUNGU IBARIKI TANZANIA
.

Kwa kuongezea tu, Kikwete ametia pamba masikioni na kushona mdomo wake kuhusu matukio haya huku akiendelea kutalii duniani kama hakuna jambo zito litokealo nchini mwake.
 
Only way ni kulinda kura,mbona Arumeru wananchi walilinda kura,nadhani kila jimbo watu wakilinda kura zao ccm itakosa pakutokea
 
Tushirikiane kuandaa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi kama vile uongozi wa vitongoji, vijiji, mitaa, madiwani na wabunge mapema kabla ya 2014 au 2015. Kisha waandaliwe kushindana na kushinda katika mzingira ya aina yoyote. Tukiwajua mapema tutaweza kujilinda dhidi ya mapandikizi na wauza majimbo kwa wana CCM wanaotaka kupita bila kupingwa.
 
Ni vigumu sana kuzuia jambo ambalo wakati wake umewadi. Mabadiliko nchini kamwe hayazuiliki ila yanatarajiwa kwa faida ya wote hadi wana-CCM wa leo.


Nadhani wewe Watanzania huwajui, wakipata msukumo usiombe kukutana nao, waulize Arusha ilikuwaje pressure kwenye halimashauri ??? Siku hiyo mtu ajaribu kudhulumu haki za kura za Watanzania aone moto utakao waka sijui ni nani atauzima, sema tu CCM wawe wastaarabu wakishindwa wakabidhi nchi kwa wenyewe!!!

 
Only way ni kulinda kura,mbona Arumeru wananchi walilinda kura,nadhani kila jimbo watu wakilinda kura zao ccm itakosa pakutokea

Tatizo sio chadema kushinda, Tatizo ushindi wa jumla kuu wa uraisi unavyochakachuliwaga na kutangazwa na Tume ya uchaguzi ambayo ndio yenye mamlaka pekee ya kumtangaza mshindi.HAPO NDO KUNA MZIKI MKUBWA BADO
 
Tatizo sio chadema kushinda, Tatizo ushindi wa jumla kuu wa uraisi unavyochakachuliwaga na kutangazwa na Tume ya uchaguzi ambayo ndio yenye mamlaka pekee ya kumtangaza mshindi.HAPO NDO KUNA MZIKI MKUBWA BADO
tatizo hakuna tume huru,tume iko mfukuni wa mtu
 

nadhani wewe watanzania huwajui, wakipata msukumo usiombe kukutana nao, waulize arusha ilikuwaje pressure kwenye halimashauri ??? Siku hiyo mtu ajaribu kudhulumu haki za kura za watanzania aone moto utakao waka sijui ni nani atauzima, sema tu ccm wawe wastaarabu wakishindwa wakabidhi nchi kwa wenyewe!!!


njia ni rahisi sana haitakiwi damu yeyote ya mtanzania kumwagika mimi nawashauri cdm wafanye yafuatayo:

1. Watafute database ya polisi wote wa ngazi za chini wanaopelekwa front kwa majina na koo zao alafu wao wawatumie ndugu na jamaa zao kuwaeleza siku moja kabla ya kupiga kura kuwa wanawategemea kusaidia mabadiliko bila ya kumwaga damu na kuwalinda wananchi dhidi ya dhuluma.

2.kutumia uzoefu wa vituo vya kupigia kura na kubashiri ongezeko ili kuhakikisha maeneo hayo yankuwa na matawi ambapo watu watakuwa wanahamasishana juu ya kusimamia kura mpaka zitangazwe.

3. Kuhahukisha wabunge wanakuwa wengi ni silaha kubwa kuliko hata ya kuwa na rais, hivyo ni vizuri wawaandae wabunge 250 watakaoshinda ubunge na sio kushiriki tu.
 
Back
Top Bottom