Nianze kwa masikitiko makubwa kutoa taarifa juu ya kile kilichojiri kwenye harusi ya ndugu yangu Victor iliyofanyika katika ukumbi wa police jamii hapa dodoma usiku wa kuamkia tarehe 17/11/2012.nilishangazwa sana na tabia iliyofanywa na CCM wanawake+vijana wanaosadikiwa kutoka ngazi ya mkoa kuingia ukumbini kutoa zawadi Kwa bwana na bibi harusi huku zikipigwa nyimbo za Ccm!niwajuavyo hawa ndugu zangu hakuna anayefanya kazi ktk ofisi ya ccm wala kuishabikia ccm!nilijiuliza kulikoni ndipo nikaamua kumsogelea na kumhoji kijana mmoja aliyejitambulisha kama Maltin Nderiwa na kunidokeza kuwa huo ni mojawapo ya mikakati iliyoazimiwa na chama kuwa wajitahidi kujitokeza kwenye HARUSI NA MISIBA na kutoa zawadi na pole mtawalia ambazo wanaamini kuwa lazima zitapokelewa!kwa kufanya hvyo watakuwa wanawateka wengi!ckuwa na uhakika kama watajwa walikuwepo ukumbini muda wote kwani baada ya kukabidh zawadi tu waliondoka!ni wazi kuwa hizi ni dalili za kufilisika hakika na kwa mbinu hz HAMTAFANIKIWA KABISA!Kufanya hvy ni kukaribisha shari na kuharibu sherehe za watu.KWELI HALI YENU NI MBAYA.cuf,chadema nk wakifanya hvyo itakuwaje.KAZI MNAYO!