CCM Chama Cha Waarabu?

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Wanawarudisha kuhodhi ardhi kwa kivuli cha kulima mashamba makubwa ,wanawarudisha kuhodhi ardhi kwa kuwapa sehemu za kati za utajiri wetu kwa kisingizio cha kutega uchumi ,wanawapa mbuga za wanyama kwa ajili ya kuwinda na kuwachukua wanyama hai kwa madazeni ,Kilimanjaro airport inatumika kikamilifu katika kusafirisha wanyama hai wa kila aina ,yaani utafikiri mbuga inahamishwa.Hakuna uwanja wa ndege unaotua midege mikubwa kama wa Kilimanjaro kwa ajili ya kusombea wanyama.

Hawa CCM ndio wanaokaa wakidanganya wengine kuwa CUF inataka kurudisha waarabu ,kuna sehemu Zanziba wameshapewa Waitali na sehemu ingine wamepewa waarabu ,yote haya hufanywa na CCM ,ila watanganyika wakiambiwa CUF ni Chama cha waarabu utadhani wamefungwa shemere za pua na kuvutwa ,wanakubaliana bila ya kuhoji ,lakini sasa unafiki wa CCM unatokeza juu juu ,mwenye macho haambiwi tazama.
 

Labda tuseme kimegeuka kuwa chama cha kinyonyaji, kwani kinasheheni kuanzia mashariki ya mbali hadi magharibi ya mbali kuutoa bila mpango utajiri wa watanzania. Ukiishia kwa waarabu utakuwa umeipunguzi stahiki yake!
 
Wewe ulitaka kulima ukanyimwa ardhi? mnataka wawekezaji wakija, ooh waarabu, mbona hamna mmoja anaesema wazungu wanaohodhi mbuga chungu nzima Tanzania, mashamba yote makubwa na mazuri ni ya wazungu. jee hayo hamuyaoni? mbona hamuhoji? kwa nini msiseme waIslam badala ya Waarabu? mnaficha nini? na huo ndio usongo wenyewe?
 



Whats shemere?
 

Sasa wewe unalinganisha wazungu na warabu,
Mbona vijana wetu hawakimbilii arabuni wanakimbilia kwa hao wazungu.
fujo zilipotokea pemba warabu waliwafuata hao wapemba kuwapeleka arabuni?
Lakini uliona Wazungu waliwachukua wapemba na kuwapeleka Uzunguni kwani warabu hawakuona?

Kwanini akuna warabu wenye asili ya kiafrika ? kwanini waafrika weusi waliopelekwa huko utumwani hawakuzaana? na kuongezeka kama kwa wazungu.
Warabu na utajiri wao wa mafuta wanatuchangia sh ngapi ktk bajet yetu?
Wazungu wanachanga sh ngapi?

mnajua fika tunavyobaguliwa na hao ndugu zenu waarabu ni lini ulisikia mwarabu kaolewa na mweusi binafsi sijawahi kuona hicho kiloja ila Wazungu nimeshuudia ndoa kibao tu! Je utaniambia kuwa vijana wetu hawapendi kuoa wanawake weupe? nadhani hapo majibu unayo.
 
Waswahili wanasema tembea uone usingoje kusimuliwa!


Sheikh Adel ben Salem Al Kalbani
Appointed Imam of Haram Mosque
 
speaking of waarabu...






Saudi Prince Alwaleed buys his own A380 jumbo jet





Saudi Prince Alwaleed buys his own A380 jumbo jet - USATODAY.com
 

Sasa wewe unaona bora wawekezaji wa kizungu kuliko kiarabu?

Vijana wetu hawakimbilii uArabuni? labda hujatembelea nchi za kiarabu! waulize wenzako wanaopita pita Dubai kufanya biashara, ni nani wanaowatembeza Dubai wakiwa wageni? for your information, ni vijana wa hapahapa Tanzania. wamejaa uarabuni, tena nadhani ni wengi kuliko waliopo huko kwa wazungu.

Huna habri kuwa asilimia kubwa ya wa Tanzania wana mashemeji au wajomba wa kiarabu? ni mwarabu yupi anaebaguwa Tanzania, labda wewe hutoki Tanzania hii ninayoishi mimi!

Wazungu kuoa au kuolewa na wa Tanzania si kipimo cha kuridhisha, kwa hilo huna hoja, na hata tukichukuwa hilo bado namba ya wazungu wanao-owa au kuolewa na wa Tanzania ni ndogo sana ukilinganisha na waArabu wafanyao hivyo. Kama unabisha kawaulize wazee wako kama kweli u mTanzania basi waulize kama hauna waJomba au Mashemeji wa kiArabu!

Hoja zako dhaifu, tafuta jingine!
 
Mbuga na mashamba wanauziwa wenye pesa zao, serekali haitazami mwarabu wala mzungu, inatazama noti tu, Hata wewe unae jiona mzawa ungepata chance ya kuuza wanyama nje ungeuza wote. Mashirika ya umma, mbuga za wanyama,mashamba,yote yamefilisiwa na nani? Warabu? acha ubaguzi wewe, We unajua wazungu wangapi hapa bongo walio olewa na mzawa?
Na hata kama mnapata msaada kutoka kwa wazungu je unajua masharti yake? Internet unayo mbona usisearch misaada inayo toka uarabuni? Je unajua kwamba Kuwait inatoa misaada mingapi Tanzania na je unajua kwamba Oman Imatoa Msaada wa bilioni 35 tsh mwaka huu pekeyake tena bila masharti yeyote. We pia kama unauwezo nenda kainvest uarabuni, hukatazwi.
 
Sehemu ya hotuba ya bajeti 2009/10 Waziri wa Fedha:Mheshimiwa Spika, napenda kuwatambua na kuwashukuru
washirika wetu wote wa maendeleo kwa misaada yao ambayo
imechangia mafanikio yetu katika sekta mbalimbali za uchumi
wetu. Naomba niwataje mbele ya bunge lako tukufu kama
ifuatavyo: Belgium, Canada, China, Denmark, United
Kingdom, Finland, France, Germany, India, Ireland, Italy,
Japan, South Korea, Kuwait, The Netherlanda, Norway, Spain,
Sweden, Switzerland, United States of America, African
Development Bank, BADEA, European Union, Global Funds,
International Monetary Fund, Kuwait Fund, Nordic Fund, Opec
Fund, Saudi Fund, United Nations Agencies na The World
Bank. Tunawashukuru sana.
MIKOPOstafa Mkullo :
 
ukoloni mbaya sana, mpaka leo bado watanzania wengine wanaona hakuna mtu bora kama mzungu. Kwa habari yako wazungu ndio wanatumaliza. Mbona hujazungumzia machimbo ya almasi,dhahabu na tanzanite, kitu gani wewe wewe mlala hoi unachopata?
 
Duh! mwaka juzi nlisikia kuwa nchi za Afrika zilifanya mkutano Afrika kusini na nchi za kizungu ili kuwadai hao wazungu fidia ya Utumwa,nikashangaa kwanini wasiwadai waarabu kama tunavosema sisi waswahili,hapo ndio nikapata ile picha halisi wanaozungumza wazee wetu kuwa utumwa ulifanywa na wazungu sio waarabu, na ndo mana wazungu wana jikosha ktk nchi zetu za kiAfrika lkn hapo hapo ktk kufatilia nikagundua bado hawa wazungu ndio wanatumaliza kulio walivotufanya watumwa,kwani kwa jinsi wanavochuku mali zetu siku zote na ushahidi upo wazi kabisa,lkn hapo hapo nikagundua hata ile misaada wanayotupa ina faida kubwa kwao kuliko kwetu,na hasa ukiangalia ina masharti makubwa saana.. kwa kweli na huko znz ninavojua ni hao ccm ndio wanajikusanyia mali,na hapo hapo mimi nina marafiki zangu wawili wa kiarabu wamechukuliwa mashamba yao na serikali hii ya Amani karume,na wamejaribu kudai hakki yao wamegonga ukuta,hao wawili ninaowajua sijui nisiowajua wangapi? Dhana ya uarabu inaletwa na wazungu ili kujificha wao kwa uchafu wao..
Cuf ni ya wananch wa Tz na ccm ni ya mafisadi wa Tz..
 
Nikikusaidia waarabu hawakufanya biashara ya utumwa ila walikuwa na soko la watumwa ,kwaana soko la kariakoo ni la serikali lakini huwezi kusema serikali inauza mboga.
Kununua ,kumiliki,kuuza ni mambo tofauti sana. La kujiuliza watumwa wakipelekwa na nani hapo sokoni Unguja ?
 

Soko na jela ya watumwa Unguja iko ndani ya Kanisa, ulishajiuliza ilifikaje? na Jee haujawahi kusikia Kanisa likikiri biashara ya utumwa na kuomba msamaha baada ya miaka mingi kupita? Au hayo makanisa ni ya waArabu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…