Lord Denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 23,494
- 57,871
Kama ni mfuatiliaji wa siasa za Tanzania utakubaliana na mimi kuwa nchi hii imekuwa ikikosa viongozi wazuri kwa sababu tu ya rushwa , ushabiki usio na maono na upenzi tu.
Nimepata nafasi ya kuwasikiliza watangaza nia wa chama cha mapinduzi na nafikiri kama hauendeshwi na siasa za ushabiki,upenzi, wivu,chuki na fedha utakubaliana na mimi kuwa wagombea wenye maono na wanaotakiwa kuwekwa na kupambanishwa na chama cha mapinduzi kwenye uchaguzi huu ni Prof Muhongo , January Makamba.
Hapa ninaelezea wagombea walioonyesha kuwa na maono mazuri ya Tanzania tuitakayo huko mbeleni na wamejipambanua vizuri kimpakakati kwenye kuyafikia maono yao kwenye HOW. Nasema hivi kwa sababu nimekuwa mfuatiliaji wa muda mrefu wa siasa za Marekani na sehemu za ulaya na nilichokuja kugundua kwa wale binadamu wenzetu ni kuwa wanaangalia sana how utakavoenda kutekeleza sera zako na sio tu uzuri wa sera. Na hapa ndo nchi nyingi za kiafrika tumekuwa tunafeli siku zote kwa sababu hatuwapimi wagombea kwa njia na mikakati yao ya kutekeleza sera zao bali uzuri tu wa sera zao na uwezo wao wa kuyazungumzia matatizo ya wananchi.
Najua wapenzi wa watangaza nia wengine mtanisema vibaya ila naomba tu leo niwajadili hawa na kutoa hitimisho mwishoni juu ya nani wa kupewa bendera ya chama chao ili akiwakilishe kwenye uchaguzi mkuu.
Kusema ukweli hawa wagombea wote wameonekana kuwa watu wa facts na reality na sio porojo na maneno matamu tu. Wote kwa pamoja wamejitanabaisha kuwa sio watu wa maneno maneno bali ni issues tu.wote kwa pamoja wamejionyesha kuwa wana maono mazuri na wanatumia vizuri exposure yao katika kuitengeneza Tanzania ijayo.
Wote wanaonekana hawana mda na mtu wala visasi na mtu kitu ambacho ni kikubwa sana kwa chama cha mapinduzi kwa wakati huu na ujao. Ka kifupi kama mtu alisikiliza hotuba ya kingunge wakati lowassa anatangaza nia Arusha na maneno yaliyokuwa yanazungumzwa na Membe wakati anatangaza nia huko kwao Lindi atakubaliana na mimi. N I ukweli usiopingika kuwa endapo team lowassa watashika nchi kuna watu lazima watakimbia nchi na likewise Membe akishika nchi ni lazima upande wa pili watafute sehemu ya kwenda. Na kama ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania utagundua ugomvi wa hizi timu mbili ndo zimeupa shida sana utawala wa sasa.
Napenda kumalizia kwa kuonesha wapi ambapo mimi naona Prof Muhongo amemzidi bwana January Makamba. Sehemu pekee ambayo Prof Muhongo amemzidi January Makamba ni kwenye uwezo wa kuongoza, kusimamia mambo kwa weredi wa hali ya juu na utendaji kwa ujumla.
Sisemi hivi ili kumsifia tu Prof Muhongo ila kila mtu anakubali kuwa huyu Prof amekaa kwenye system kwa miaka miwili tu ila alivoisimamia Tanesco hasa kwa miradi ya usambazaji vijijini hadi kufikia asilimia 38 wakati anaondoka huu ni utendaji wa kutukuka na kipekee sana unaomfanya astahili kupewa tuzo ya heshima na raisi. Pili ni alivosimamia sekta ya gesi kwa kipindi hiki kifupi huku akikataa kuwapa watu wababaishaji vitalu na kusimamia upatikanaji wa schoralships kwa watanzania wengi inasemekana zaidi ya 100 kwa ajili tu ya kuifanya nchi ije kuwa na wataalam wa kusimamia hii sekta(hapa napenda kumfananisha na kagame anavofanya Rwanda).
Hizo ndo sifa ambazo Prof Muhongo anaonekana kumzidi January Makamba na January anaitaji kupewa mda kidogo ili aweze kuprove how strong he is kwenye huo upande.
Napenda kusisitiza kuwa watu wa kambi zingine mtanisamehe sana,wengi wagombea wenu wnapata popurarity only kwa kuisemea rushwa tu na kupambana na wala rushwa ila sio kwenye vision ya kuitengeneza Tanzania imara kwenye uchumi na mikakati ya kutekeleza sera zao na kuifikia iyo vision.
Nilisema kwenye post moja humu kuwa CCM iandae timu imara ya kufanya kazi na Prof MUHONGO na kwa kuanzia mwampe Salim Ahmed Salim kuwa makamu wake. Leo napenda kutoa ushauri kwa Prof mwenyewe kuwa Mungu akikubariki uingie magogoni mambo ya nje mpeleke January akajijenge zaidi, na January najua utasoma hii post naomba sana ufanyie kazi ilo eneo nililokuomba ulithibitishe kwa watanzania ili mda ukifika Prof akistep down upewe kijiti uendeleze vision bora kwa taifa la Tanzania.
MUNGU ibariki TANZANIA na WATANZANIA WOTE.
MUNGU wabariki Prof Muhongo na January Makamba.
Nimepata nafasi ya kuwasikiliza watangaza nia wa chama cha mapinduzi na nafikiri kama hauendeshwi na siasa za ushabiki,upenzi, wivu,chuki na fedha utakubaliana na mimi kuwa wagombea wenye maono na wanaotakiwa kuwekwa na kupambanishwa na chama cha mapinduzi kwenye uchaguzi huu ni Prof Muhongo , January Makamba.
Hapa ninaelezea wagombea walioonyesha kuwa na maono mazuri ya Tanzania tuitakayo huko mbeleni na wamejipambanua vizuri kimpakakati kwenye kuyafikia maono yao kwenye HOW. Nasema hivi kwa sababu nimekuwa mfuatiliaji wa muda mrefu wa siasa za Marekani na sehemu za ulaya na nilichokuja kugundua kwa wale binadamu wenzetu ni kuwa wanaangalia sana how utakavoenda kutekeleza sera zako na sio tu uzuri wa sera. Na hapa ndo nchi nyingi za kiafrika tumekuwa tunafeli siku zote kwa sababu hatuwapimi wagombea kwa njia na mikakati yao ya kutekeleza sera zao bali uzuri tu wa sera zao na uwezo wao wa kuyazungumzia matatizo ya wananchi.
Najua wapenzi wa watangaza nia wengine mtanisema vibaya ila naomba tu leo niwajadili hawa na kutoa hitimisho mwishoni juu ya nani wa kupewa bendera ya chama chao ili akiwakilishe kwenye uchaguzi mkuu.
Kusema ukweli hawa wagombea wote wameonekana kuwa watu wa facts na reality na sio porojo na maneno matamu tu. Wote kwa pamoja wamejitanabaisha kuwa sio watu wa maneno maneno bali ni issues tu.wote kwa pamoja wamejionyesha kuwa wana maono mazuri na wanatumia vizuri exposure yao katika kuitengeneza Tanzania ijayo.
Wote wanaonekana hawana mda na mtu wala visasi na mtu kitu ambacho ni kikubwa sana kwa chama cha mapinduzi kwa wakati huu na ujao. Ka kifupi kama mtu alisikiliza hotuba ya kingunge wakati lowassa anatangaza nia Arusha na maneno yaliyokuwa yanazungumzwa na Membe wakati anatangaza nia huko kwao Lindi atakubaliana na mimi. N I ukweli usiopingika kuwa endapo team lowassa watashika nchi kuna watu lazima watakimbia nchi na likewise Membe akishika nchi ni lazima upande wa pili watafute sehemu ya kwenda. Na kama ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania utagundua ugomvi wa hizi timu mbili ndo zimeupa shida sana utawala wa sasa.
Napenda kumalizia kwa kuonesha wapi ambapo mimi naona Prof Muhongo amemzidi bwana January Makamba. Sehemu pekee ambayo Prof Muhongo amemzidi January Makamba ni kwenye uwezo wa kuongoza, kusimamia mambo kwa weredi wa hali ya juu na utendaji kwa ujumla.
Sisemi hivi ili kumsifia tu Prof Muhongo ila kila mtu anakubali kuwa huyu Prof amekaa kwenye system kwa miaka miwili tu ila alivoisimamia Tanesco hasa kwa miradi ya usambazaji vijijini hadi kufikia asilimia 38 wakati anaondoka huu ni utendaji wa kutukuka na kipekee sana unaomfanya astahili kupewa tuzo ya heshima na raisi. Pili ni alivosimamia sekta ya gesi kwa kipindi hiki kifupi huku akikataa kuwapa watu wababaishaji vitalu na kusimamia upatikanaji wa schoralships kwa watanzania wengi inasemekana zaidi ya 100 kwa ajili tu ya kuifanya nchi ije kuwa na wataalam wa kusimamia hii sekta(hapa napenda kumfananisha na kagame anavofanya Rwanda).
Hizo ndo sifa ambazo Prof Muhongo anaonekana kumzidi January Makamba na January anaitaji kupewa mda kidogo ili aweze kuprove how strong he is kwenye huo upande.
Napenda kusisitiza kuwa watu wa kambi zingine mtanisamehe sana,wengi wagombea wenu wnapata popurarity only kwa kuisemea rushwa tu na kupambana na wala rushwa ila sio kwenye vision ya kuitengeneza Tanzania imara kwenye uchumi na mikakati ya kutekeleza sera zao na kuifikia iyo vision.
Nilisema kwenye post moja humu kuwa CCM iandae timu imara ya kufanya kazi na Prof MUHONGO na kwa kuanzia mwampe Salim Ahmed Salim kuwa makamu wake. Leo napenda kutoa ushauri kwa Prof mwenyewe kuwa Mungu akikubariki uingie magogoni mambo ya nje mpeleke January akajijenge zaidi, na January najua utasoma hii post naomba sana ufanyie kazi ilo eneo nililokuomba ulithibitishe kwa watanzania ili mda ukifika Prof akistep down upewe kijiti uendeleze vision bora kwa taifa la Tanzania.
MUNGU ibariki TANZANIA na WATANZANIA WOTE.
MUNGU wabariki Prof Muhongo na January Makamba.