Namjua tangu tunasoma nayee pale Kibaha sec,Gambo janja janja sana ile kijana...
CCM inabidi ibadilike kwakweli sa hivi ni mda wa kuweka watu wazalendo na ambao bongo zinachemka ila kukumbatia watu wanaofikiria matumbo yao tu kwa zama hizi za teknolojia hizi aibu hazitatuacha kwakweli
Daaaah mnafrahishagaaa sanaaaWewe ni mnafiki. Polepole ni jiniasi anakuzidi sana kiakili na weledi. CCM ipo pahala pazuri sana kuliko kipindi chochote kwa sasa. Kila mwananchi anaelewa umuhimu wa CCM ya sasa. Yaani huku kitaa ni chereko chereko!
Wewe ni mnafiki. Polepole ni jiniasi anakuzidi sana kiakili na weledi. CCM ipo pahala pazuri sana kuliko kipindi chochote kwa sasa. Kila mwananchi anaelewa umuhimu wa CCM ya sasa. Yaani huku kitaa ni chereko chereko!
Maombi yamedunda kwa jamaaHuwezi nielewa, ingawa natamani sana unielewe, tuna wajibu wa kumwombea kwa sababu ni rais wetu, maamuzi yake yanatuathiri, Kitendo cha Bashite, Clouds na Treatment ya Nape, kinazihirisha kwamba hayupo tayari kusikiliza ushauri wa mtu, there is nothing you can do, HATAKI, PERIOD.
BILA SUPPORT YA POLISI NA VYOMBO VYA USALAMA SSM NI WEPESI KAMA UNYOYAHuko nyuma nilipokuwa naandika mambo humu tena ya Kuikosoa CCM lakini nikiwa na maana moja kubwa tu ambayo kwa bahati mbaya sana ' Wapumbavu ' wachache waliojawa na ' Unafiki ' mkubwa na uliotukuka kabisa walikuwa wakinikejeli, kunitusi, kunikashifu huku wakisema kuwa Mimi GENTAMYCINE ni mwana CHADEMA na nakumbuka kila mara niliwahi kuwaambia kuwa ipo siku ' mtanielewa ' na ' mtanikumbuka ' na hatimaye sasa yametimia.
Nilishamwambia hadi Mwenyekiti wetu Taifa kuwa awe makini sana kwani humo humo ndani ya CCM yetu kuna ' Mamluki ' wengi ambao wanamchafua na kumuharibia ili baadae aharibikiwe na waje kumcheka hakunisikia.
Nilishawahi kueleza mapungufu kabisa ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye sifichi na sioni aibu kusema kuwa ni mmoja kati ya Watu ninaowajua in and out na kuna siku nilisema humu humu JF kuwa kama kuna Mtu ambaye tokea ' Teuzi ' za CCM za Wagombea Urais 2015 alikuwa hampendi, hamtaki na akimdhihaki sana Mgombe wa Urais Rais wa sasa wa JMT Dkt. Magufuli alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha na kuna siku moja tukiwa nae katika Nyumba jirani na ilipo Hotel ya Kebby's Mwenge alionge a' Kauli ' moja ambayo siku niliposikia ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa na JPM nilianza kumuonea mno ' huruma ' JPM kwani nilianza kujua nini kitakuja.
Nilishawahi kusema humu humu tena kwamba kuna Wana CCM wenzetu wanadhani kumpamba, kumsifu na kumpa matumaini hewa Mwenyekiti wetu Rais Dkt. Magufuli kutakisaidia Chama chetu lakini pia kutawasaidia Wao kuendelea kula ' bata ' ndani ya Chama wakati ukweli ni kwamba akina Sisi GENTAMYCINE ambao tunakosoa baadhi ya mambo yawezekena ndiyo tukawa na ' uchungu ' wa kweli kabisa na CCM yetu na Magufuli wetu ila kila mara ' Mwanamume ' nabaki kuambulia ' Kashfa ' na ' Kejeli ' kumbe wakiwa wamesahau kuwa Mimi ndiyo ' Malaika ' mwema wa Mungu niliyepo duniani Kukomboa, Kurekebisha na Kunyoosha.
Nilishawahi humu humu kuandika kwamba hakuna Kipindi ambacho Chama chetu Tawala cha CCM kimepata Msemaji ' goi goi ' kama sasa na nikatoa sababu zangu nyingi sana za Kitaaluma na Kiuweledi kwamba Bwana Hamphrey Polepole ' hatoshei ' hapo na kuna siku ' ataharibu ' na ' kuboronga ' zaidi lakini kama kawaida nikapuuzwa na kukejeliwa lakini alichokifanya Polepole majuzi baada ya kuwasikia akina Nassari na Lema juu ya ' Kashfa ' ya aibu katika Chama sasa ndiyo ' kimeigharimu ' CCM kwani kama Polepole angekuwa ' ameiva ' hasa Kimawasiliano, Kipropaganda na Kimkakati ' asingekurupuka ' kuwajibu vile akina Nassari na Lema ambao nao sasa wakaamua kumwaga kila kitu hadharani na sasa tunaaibika.
Nasikia leo kuna ' Mpuuzi ' mmoja hivi anajiandaa kuzungumza na Press ili eti kufanya ' counter ' juu ya walichosema akina Nassari na Lema hivyo nichukue nafasi hii kumwambia tu kwamba asipoteze huo muda na hizo juhudi bali labda kikubwa ambacho anatakiwa kukifanya ni kuandika haraka sana Barua ya Kujiuzuru ' madaraka ' yake lakini pia upesi sana aende mwenyewe Ofisi za TAKUKURU ili ' mashtaka ' rasmi dhidi yake yaanze ili muda wowote tuwe tunaenda kumsalimia / kumsabahi akiwa Gerezani anatumikia ' Kifungo ' chake.
Mwisho nimwombe sana Mheshimiwa Mwenyekiti wetu Taifa wa CCM na Rais wangu Mpendwa kabisa wa JMT Dkt. Magufuli kwamba siku zingine awe anaingia humu JamiiForums na angalau basi aweze kuona Sisi akina GENTAMYCINE, wana CCM makini, wakweli na wawazi wenzangu bila kusahau hata wale Watanzania wenye mapenzi mema nae na kwa nchi wanasema nini au wanamshauri nini. Humu Jamvini JF kuna Watu wana maono ya mbali na wanajua mambo pengine hata kuliko hao ambao wako nae karibu ila ' tunadharaulika ' wakati kiukweli haya tunayoyaibua wala hatutaki tulipwe au tupewe fadhila yoyote bali tumekomazwa na ' Uzalendo ' wa ukweli kwa nchi na taifa.
" hata Kichaa au Mwendawazimu kuna wakati huwa anaongea mambo ya msingi na ambayo yanaweza pia kukuoa au kukusaidia katika maisha yako hivyo tuache kuwadharau kwa sababu tu ya hali zao kwani kila Mtu yupo hapa duniani kwa makusudi yake Mwenyezi Mungu "
Sijui GENTAMYCINE nitaficha wapi Mimi ' aibu ' hii ya Arusha!
Nawasilisha.
Mimi kwa ukweli wa moyo wangu sitofautishi walivhofanya wakina Gambo, Mnyeti, na Yale anayoyafanya malaika mtukufu.
Staili waliyoitumia wakina Mnyeti na Gambo kina tofauti gani na zile rushwa za vyeo zinazotolewa na mtukufu?
Rejea rushwa ya vyeo ambayo kingereza inaitwa patronage corruption ilivyofanya kazi kwa
1; Anna Mghwira
2: Kitila mkumbo
3: lyatonga Mrema
4: Humphrey pole pole
5; Ibrahim Lipumba
Na hao ni kwa uchache. Jamani naomba tofauti kama mnaziona
KAMA ALIVYO BABA NDIVYO WALIVYO WATOTO.
Mm ni CCM, but to speak the TRUTH, evidences za videos tena zina sauti ni mbaya sana sanaaaa... Nassary aka Dogo Janja hapa naona kacheza muziki wa dunia ya kwanza, ushauri wangu kwa Mh. Rais wangu JPM, fukuza RC Arusha, DC na Mkurugenzi Arumeru, hapo utaonekana umepinga rushwa kwa vitendo, and this will PROVE kwa wananchi na wana CCM wenzangu kuwa uzembe hautakiwi ktk kazi..
Sbb hapo kuna uzembe mkubwa sana from RC, DC Arumeru, Mkurugenzi Arumeru wote wazembe kabisa na kiukweli wamekidhalilisha sana Chama chetu CCM.. THIS IS MY FEELINGS.. Fukuza hawa, and uaminifu na uzalendo wako kwa wananchi wetu Mh. Rais utapanda kwa kasi drastically, siasa ni mchezo so Mh. Rais huu ni ushauri wangu..
Fukuza hawa, wametuchafua wazi wazi, CCM mpya ya sasa haitaki uzembe wa aina yoyote.. and utaona jinsi HILI LITASAIDIA MNO MNO 2020
Mungu mbariki Mh. Rais wetu, Mungu ibariki CCM yetu..
Hawawezi tia Mguu leo humu ndani.
tafuta miwani labda una shida ya macho. au wewe ni " Mnyeti" kaacha Nyeti za ccm wazi .pwaahhhhhMtu hata kama humpebndi gambo au mnyeti huwezi taka mtu ajiuzulu kwa tuhuma za vi photoshop vya kutengeneza kwenye vyoo vya ofisi za chadema Arusha.Ushahidi wa mahakama au takukuru ndio waweza mtia hatiani mtu.Watu wanasema walipewa mamilioni !!! Na watu wengine humu wanasema ndiyo walipewa!! Uliziona hizo pesa wakipewa? Hata hivyo viphoto shop koko vya Lema na Nassari havionyeshi.Watu wanadakia humu walipewa!!!! Gambo and Munyeti are there to stay.Hatoki mtu ng`ooo.CCM tuachieni wenyewe wengine akina team lowasa mlio chadema endeleeni na yenu.Kama mnataka kurudi CCm rudini tu lakini mambo ya photoshop za chadema waacheni wenyewe.ya ngoswe mwachie ngoswe.
Magamba yanaruka na kukanyaganaMtu hata kama humpebndi gambo au mnyeti huwezi taka mtu ajiuzulu kwa tuhuma za vi photoshop vya kutengeneza kwenye vyoo vya ofisi za chadema Arusha.Ushahidi wa mahakama au takukuru ndio waweza mtia hatiani mtu.Watu wanasema walipewa mamilioni !!! Na watu wengine humu wanasema ndiyo walipewa!! Uliziona hizo pesa wakipewa? Hata hivyo viphoto shop koko vya Lema na Nassari havionyeshi.Watu wanadakia humu walipewa!!!! Gambo and Munyeti are there to stay.Hatoki mtu ng`ooo.CCM tuachieni wenyewe wengine akina team lowasa mlio chadema endeleeni na yenu.Kama mnataka kurudi CCm rudini tu lakini mambo ya photoshop za chadema waacheni wenyewe.ya ngoswe mwachie ngoswe.