CCJ Kulikoni!?

Inawezekana kweli uongozi wa muda wa CCJ ni dhaifu kutokana na kukosa uzoefu wa kisiasa. Hata hivyo, binafsi hupenda kuwaamini sana watu wa aina hiyo ambao siyo professional politicians, at least in the short term.

Kuhusu kuwa na wanachama mamluki, hilo ni tatizo linalowezekana, na njia pekee ya kulitatua na kuleta wanachama zaidi ya hao 200 ili kunyutralaize effect ya mamluki.
 
Watanzania hakuna tunaloliweza; tunashindwa hata kupata watu 200 ambao sio mamluki halafu tunaomba tupewe uongozi wa nchi? Very disapointing!
 
Siamini kama CHADEMA mnapigwa chenga rahisi kiasi hiki...

Nilishasema na bado naona CCJ ni mradi wa CCM kuidhoofisha CHADEMA. Mbona liko dhahiri? Nilisema mwanzoni kuwa upinzani wote anaoonyesha Tendwa kwa CCJ ni blanket la kufunika uhusika wa CCM ktk hiki chama.

Mwanzoni alisema kuwa CCJ is a hoax, baadae within no time akakipa usajili wa kudumu. Baadae akasema hamna fedha za kwenda kuhakiki wanachama wao, within no time amekwenda, na nilisema hapa kuwa Tendwa anageresha tu, atakwenda kuwahakiki CCJ. Jana anasema wanachama wake ni batili, I assure you, within short time Tendwa atakuwa amemaliza na ameridhika na wanachama wa CCJ. The issue is Tendwa anatumika na CCM kuweka vijiupinzani kwa CCJ lakini ili ionekane inachukiwa na mamlaka za dola, na watu waamini kuwa inachukiwa na CCM. CCJ itasajiliwa, itakuwa na fedha nyingi za kwenda kwenye uchaguzi hasa kwa wabunge, itawagawa wanachama wa upinzani kwenye majimbo na at the end CCM itakosa mpinzani thabiti.

If I am to advice oppositions parties in their competition with CCM, I would advice that their proper target now is to fight CCJ. CCM ni wajanja kidogo na katika hili wanaweza kuwabeat CHADEMA kirahiiiisi, I tell you...
 

If CCJ people want to participate in the next GE let them join existing parties. There are 18 parties to join or take over. These people are politically naive my brother.

The easiest way was to take a small party like UMD, JAHAZI ASILIA etc, call the national congress and change the name. They decided to take a long route. Reason? They were not real, they just wanted to threaten their old party CCM so that it accommodates them.

I know the essence of CCJ. I spoke to all people they claim to have especially the ethical elders. These are my wazee and i meet them every weekend. None of them is in CCJ. These guys once upon a time visited some elders, and let the Intelligence system know that, and then declared a party. This CCJ thing is hoax. This CCJ confuses us.

Tupige mstari na kujipanga kwenda mbele. Those in CJJ with liberal minds join CUF, those with conservative minds come CHADEMA, those with socialist orientation join NCCR-M or TLP. Tusipoteze muda, we need more MPs in the house.......
 
Inawezekana kweli uongozi wa muda wa CCJ ni dhaifu kutokana na kukosa uzoefu wa kisiasa

This is true kwa sababu CCM hawawezi kuweka watu makini katika uongozi wa CCJ kwani wanaweza baadae wakawabadilika halafu ikawa balaa...
 
ukweli halisi hakuna chama cha upinzani chenye nia ya kuigomboa nchi yetu kutoka mikononi mwa CCM,wote wapo kwa maslahi yao binafsi na ndio maana imekuwa vigumu sana wapinzani kuungana japo kuwa lengolilitakiwa liwe moja

Wenger...

binafsi napenda sana siku moja chama cha upinzani kichukue nchi kutoka mikononi mwa CCM. Lakini ikiwa italazimu kuunganisha vyama vya upinzani (ambavyo tunajua kwa asili vina sera tofauti), basi bora nchi ibakie mikononi mwa CCM. Tujifunze kutoka Kenya, majirani zetu...
 

Nakuunga mkono Zitto.

Kuna watu humu wanailaumu CCM kwa uzembe ambao mtu yeyote mwenye akili timamu ataona kuwa ni madudu yaliyofanywa na hao wanaojiita viongozi wa hiyo CCJ, it is a joke!!

Ni wakati watanzania tuanze kuangalia vitu kwa umakini badala ya kuwa kila siku ni kutafuta nani wa kulaumu kwa matatizo yetu...hii ni hulka mbaya sana. Mi sijaona wala kusikia hapa hoja yeyote ya nguvu ambayo kweli inaonesha kuna mkono wa mtu kwa huu uzembe na kama upo hauingii akilini; sababu kuu mbili:

1. CCJ walidai wanazaidi ya wanachama 2,000 Dar sasa kwenye Habarileo wanadai watu waliofika mwembeyanga hawazidi 150, wakati wanahitajika 200 na kujigamba kwenye vyombo vya habari kuwa wako tayari na kumwita Tendwa tena hata kama hana hela wanampa za kwao. Sasa ni CCM ndio iliyodai kuwa CCJ ina wanachama 2,000 au CCJ wenyewe?

2. Inakuwaje hata viongozi wa chama kweli wakose kadi? Hawa kweli ndio viongozi tutegemee waje kutukomboa labda wagombee serikali za mtaa sio taifa.

Msimamo wangu ni uleule tayari kuna vyama vingi Tz tuangalie namna ya kuconsolidate hivi ili tupate upinzani bora na si bora upinzani. Uwingi si hoja hoja ni quality yao...

Zitto kama ulivyosema mwanzo nyie angalieni namna ya kushirikiana na vyama vilivyopo ili tuongeze upinzani bungeni na njia mojawapo ni kushirikiana na wapinzani wengine na kuanisha majimbo ambayo kila mmoja ana nguvu na kusaidiana ili angalau wabunge wa upinzani wafike angalau theluthi moja ya wabunge au hata robo( let be realistic here...) kutoka namba ya sasa ambayo ni chini ya 15%
 

well kwa style hio basi itachukua mda au haitowahi kutokea kwani wanachofanya sasa hivi ni wapinzani wanajigawanya wenyewe kwa wenyewe tu.
 

Kuna nchi nyingi tuu zinaongwa na vyama vyenye mseto bila kubadili majina wala sera zao...mifano SA (ANC, COSATU na SACP), UK (tories na Libdem), Germany, Israel, Belgium na Uholanzi na nchi nyingine kibao tu...Kwa hiyo hili si suala jipya tayari nchi nyingi zinatumia huo mfumo. Tukitaka kusubiri mpaka Chadema wawe na nguvu peke yao au CUF basi tutasubiri muda mrefu sana, mi sioni kwa nini washindwe kushirikiana ni ubinafsi tu..wakiweka ubinafsi kando inawezekana hiyo.
Hata Kenya unakosema huo mseto wao ndio umepunguza matatizo ya mwanzo kuhivo ni solution sio tatizo same with Zim
 

Zitto

Nakuunga mkono kwa asilimia 100 katika hili, Tatizo la CCJ ni kujiona wanaweza kufanya mambo yote bila kujifunza kwa vyama vingine. Kujisifu kwingi bila matendo. Walipaswa kuheshimu yote yaliyofanywa na vyama vya upinzani tangu mfumo wa vyama vingi uanze.

Ngoja wapate joto la jiwe ndipo watakapojifunza kuwa siasa si maneno maneno ila ni mipango na mikakati
 


Nakubaliana na wewe 100 kwa 100. Hakuna haja ya kuendeleza mada na hawa hoax sisi tuanze kujipanga kwa vita kuu na CCM. Hivi Chicago kuna nini jamani?
 
Zitto,

Kula tano kaka, mboan simu yangu hupokei? Nataka kubadilishana mawazao kidogo nawe kwa manufaa ya chama chetu.
 

Kuwa mkweli kaka kwani wao ccj ndio waliolazimisha Tendwa kufanya uhakiki sasa iweje useme eti wamestukizwa,semeni tuu kuwa Mmefulia
 
minadhani ccj hawakujipanga vizuri waliharakisha mambo bila kuwa makini kwa kukosea kuweka kumbukumbu za namba vizuri
 
Usitulazimishe kukubali tusichotaka,ukweli mmefulia tuu,tunakukaribisha Chadema kwani Mtei ameshatoa salamu kwenu.teh teh teh
 
Tujipe muda kwanza ila hali hii haimfurahishi yeyote anayekipenda chama cha upinzani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…