Capital Gain Tax ni nini?

Capital Gain Tax ni nini?

Capital gains income is calculated as follows: - Value of consideration received or accruing as a result of the realisation of the interest in land or buildings less cost of acquisition less expenditure incurred on any improvement to the asset less expenditure incurred wholly and exclusively in connection with the realisation.

Capital gain tax inatozwa kutoka kwenye capital gain income.

Capital gain income unaipata kwa kuchukua hela uliopokea ukiuza nyumba au ardhi unatoa ile garama ya kununulia au kujenga unatoa garama ulizotumia kuboresha hiyo nyumba au ardhi unatoa na garama zingine zilizohusiana moja kwa moja na kuuza nyumba au ardhi.

Kwa case yako unatakiwa uchukue hyo mil 80 na kitu uliyopokea unatoa garama ulizotumia kununua ardhi mpka kujenga nyumba na kukamilika unatoa tena garama ulizotumia kuiboresha hiyo nyumba na ardhi yake mpka imefikia kuuzika unatoa na garama nyingine zinazoendana moja kwa moja na hyo nyumba pamoja na ardhi yake. Faida unayopata hapo Ndio inayotozwa kodi ya asilimia 10 capita gain tax.
 
Sema tu labda wanaweza wakakubana kwa kutumia valued amount na wasitumie hyo uliyopokea lakini ni baada ya makato yako yote ndipo unapata faida ambayo inatozwa asilimia 10.
 
Labda kwa nyumba ya juzi juzi, wengine nyumba imejengwa 1997....ukiwachekea tu tra wanakutwanga kisawasawa.
Mie siku hizi nimeishakuwa sugu, wamenisumbua sana kiasi kwamba siwaogopi tena.. unakosa raha kabisa ukiona simu ya TRA ila siku hizi wanapiga simu au kutuma barua nawapiga kabisa na sound.. wao hawajui uharisia wa biashara na pesa zake zaidi ya kuzitaka tu hizo pesa zetu..
 
Mkuu ipo hivi: Kwa mfano ulinunua nyumba kwa 80,000,000 halafu ukaja kuiuza kwa kwa 90,000,000 utapata faida ya 10,000,000. Hivyo capital gain tax ni 10,000,000×10% = 1,000,000. ...Hakikisheni kwenye gharama zenu za kuinunua hiyo nyumba zinakuwa kubwa ili kupunguza faida. Kwa mfano kama mliinunua kwa 80,000,000 lazima kuna gharama zingine mliingia kama vile ukarabati, dalali, etc. Ongezeni hizi gharama kwenye nyumba ili nyumba ionekane iliwacost hela ndefu. Gharama ya ununuzi ikiwa kubwa mtajikuta mmelipa kodi ndogo sana.
Umemaliza mzee

Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
 
Baada ya kupeleka docs TRA , wananiambia capital gain Tax ni 10% ya market value ambapo kwa mimi ni 10% ya mil 134 sawa na Mil 13.

Wakuu hapa nimechanganyikiwa naona kama naibiwa au wanajitisha nitoe rushwa.

Nimejaribu kugoogle napata maana nyingine hata kwa Tanzania na hakuna online calculator kwa Tanzania kujua nahitaji kulipa kiasi gani.

Wakuu Capital Gain Tax ni nini?

Mbona ni kubwa kiasi hiki? Ni afadhali tusingeuza nyumba. Tuibakize iwe ya urithi?

aliekwambia unalipa 10% ya 134M ni mwizi

Itoshe kusema hao maafisa TRA wenyewe hawajui capital gain tax inatozwa vipi na wameumiza watu wengi sana

1/. kusanya gharama ya kununulia kiwanja
2/. kusanya gharama zako za materials na mafundi
3/. thamani ya muda uliotumia kusimamia
4/. jumlisha namba 1-3 hapo juu
5/. pinga iyo 134M with evidence wakupe ushahidi mtu alieuza nyumba kwa bei hyo maeneo hayo: mtafikia bei halisi (market value)
6/. chukua jibu la namba5 toa na jibu la namba4
7/. chukua 10% zidisha na jibu la namba 6

***siku nyingne upeleke jukwaa la elimu huko/ biashara
 
TRA inaongozwa na makanjanja wengi sana aisee, kuna kitu kinaitwa capital gain na capital loss, capital gain tax inatozwa pale mfano ulinunua capital asset kwa million 10 ukaja ukauza kwa million 15 so unafaida ya million 5 kwa capital gain tax utatozwa 10% ya 5 million and not 15 million, pia kama utauza hiyo assets kwa million 8 wakati ulinunua million kumi hapo utakuwa na hasara ya million 2 so itakuwa ni capital loss na hutatozwa hata senti moja ya capital gain. Tuje kwa Hao makanjanja kama walifanya evaluation kwa sasa ni million 134 pia walipaswa waevaluate first time unaanza kumiliki hiyo nyumba ilikuwa na thamani ya shingapi ili ndo waje watoe kwenye hiyo 134m kupata tax base, mfano kama watagundua first time unamiliki ilikuwa na thamani ya million 90 ndo inakuwa 134-90=44 kwa hiyo kodi utakayopaswa kulipa ya capital gain tax ni milioni 4, makenge hao acacia kauza mgodi hayakutoza hata senti moja Leo wewe mnyonge wanakuja kukunyonya utazani ni mrundi hebu tafuta mwanasheria akusimamie
 
Anaepaswa kulipa capital gain tax ni nani? Mnunuzi wa nyumba/kiwanja au ni muuzaji?
 
Anaepaswa kulipa capital gain tax ni nani? Mnunuzi wa nyumba/kiwanja au ni muuzaji?
Anayetakiwa kutoa ni muuzaji wa bidhaa na si mnunuzi. Kwa sababu mnunuaji hapati faida,
Au mfanye makubaliano kuwa tuandike bei ndogo badala ya 80,000,000, tuandike 60,000,000 na au gharama za capital gain tax zitakuwa zako, au gharama za uhamishashaji wa umiliki wa mali zitakuwa za mnunuzi

Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
 
KWA kifupi dada angu kama hauna uzoefu au elimu ktk maswala hayo mtafute mtalamu either muhasibu au mwanasheria akusaidie kulisolve hilo Mana tra unavyopinga wanataka uje na evidence na maelezo ya kutosha.... unless watakuliza tu hao hicho kiwango walichokwambia ni ujanja tuu..

Mtafute mtaalamu ata kwa kumlipa mtengeneze mazingira uonekane umepata loss au gain iwe ndogo sanaa.

Mana kwa elimu yangu nilioipata capital gains utachajiwa endapo utakizi vigezo vya kuchajiwa yaani kama VAT payable muuzaji atalipa au kurudishiwa kama amekidhi vigezo (yaani kuna kiasi cha mauzo ukifikia ndo unaambiwa ulipe Kodi)...miongoni mwa vigezo vya kukatwa capital gains ni.

Hyo gain iwe imezidi kiasi cha sh 15M na hyo nyumba iwe imemilikiwa kwa zaidi ya miaka 3 au zaidi.

Sasa mtu una gain ya laki moja apo unachajiwa capital gains ya nini,ni sawa tu unapata mauzo ya duka lako sh. 5M kwa mwaka afu unaambiwa ulipe Kodi si kufirisiana uku..

Ushauri wangu mtafute mtaalamu mlipe akufanyie hyo kazi apo kuna uwezekano usilipe ata hyo capital gains labda makato mengine ya halmashauri tuu...
TRA sio watu wazuri ukiwa hujui sheria wanakushambulia Sana kuna muda watu wenye kujitambua huwafkisha adi high court na kupata haki zao.
 
Hapana sio hivyo mkuu. Capital gain ni 10% ya net profit. Kwa mfano gharama halisi ya kununua nyumba ni 3,000,000 halafu ikauzwa kwa 4,000,000, faida yake ni 1,000,000. Capital gaini ni 1,000,000×10% = 100,000.
kwanini ukichukua salers les cost unapata nini? kunatafuauti gani ulichoandika na kile nimeandika
 
TRA wamechukua the Higher of Selling price and market value (Valuation ndio market value ya tra)
Sasa huwa haiendi hivyo mkuu. Kinachotakiwa kutumika ni actual sales sio market value. Hawezi kutozwa kodi kwa hela ambayo hajaipokea. Naongea kwa kujiamini kwa sababu hii taaluma ya kodi ndio inayoniweka mjini.
 
Sasa huwa haiendi hivyo mkuu. Kinachotakiwa kutumika ni actual sales sio market value. Hawezi kutozwa kodi kwa hela ambayo hajaipokea.
Sasa huwa haiendi hivyo mkuu. Kinachotakiwa kutumika ni actual sales sio market value. Hawezi kutozwa kodi kwa hela ambayo hajaipokea. Naongea kwa kujiamini kwa sababu hii taaluma ya kodi ndio inayoniweka mjini.
kila mtu akianza kuleta kisomo si hatari, poa mkuu
 
Mie sielewi,sasa nyumba umeuza milioni 80,hiyo market value ya milion 134 inatoka wapi?,
Halafu mbona hawajatoa gharama za ujenzi ili ile faida,ambao ndo capital gain wakate asilimia 10?
 
kila mtu akianza kuleta kisomo si hatari, poa mkuu
Nikuulize swali fikirishi kidogo tu mkuu. Hivi kwa mfano una nyumba yako ambayo thamani yake ni 50,000,000 lakini kwa sababu una shida let's say unauguliwa na mtoto, ukajikuta umeiuza hiyo nyumba kwa 30,000,000 ili upate hela haraka kwa ajili ya matibabu. Unadhani kati ya 50ml na 30ml ni wapi basis ya kodi itaangukia? ...50ml ni market value, 30ml ni actual sales.
 
Back
Top Bottom